Zanzibar 2020 Zanzibar: Hafla ya kuapishwa Rais mteule Awamu ya Nane, Dkt. Hussein Mwinyi Uwanja wa Amaan

Zanzibar 2020 Zanzibar: Hafla ya kuapishwa Rais mteule Awamu ya Nane, Dkt. Hussein Mwinyi Uwanja wa Amaan

CCM Damu

Member
Joined
Oct 29, 2007
Posts
15
Reaction score
28
Leo Rais Mteule wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi anaapishwa kuyatwaa Rasmi madaraka ya kuingoza Zanzibar akimrithi Dr. Ali Mohamed Shein. Kwa sasa tayari wananchi na viongozi wameshawasili ikiwemo marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Dkt. Jakaya Kikwete.

=======

3:35 Asubuhi: Amewasili mkuu wa majeshi Tanzania, Venance Mabeyo. Pia amewasili Balozi Seif Ali Iddi, makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar.

3:47 Asubuhi: Amewasili waziri mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa. Pia amewasili makamu wa Rais Muungano, Mama Samia Suluhu.

4:03 Asubuhi: Amewasili Dkt. Hussein Mwinyi na yanafanyika maandamano kuelekea jukwaa la kiapo yanayoongozwa na Jaji mkuu wa Zanzibar.

KIAPO(4:50 Asubuhi)
Jaji mkuu anasoma kifungu kinachomlazimu Rais mteule kula kiapo kabla ya kuchukua madaraka ya Rais kuiongoza Zanzibar. Baada ya hapo Dkt. Mwinyi anasoma kiapo na kuwa Rais wa awamu ya nane wa serikali ya mapinduzi Zanzibar.

Dkt. Mwinyi: Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia Afya na kunirudhuku dhima hii kubwa iliyo mbele yangu ya kuwaongoza na kuwatumikia wananchi wenzangu wa #Zanzibar

Naipongeza Tume ya Uchaguzi Zanzibar kwa kukamilisha majukumu yake ya Kikatiba na Kisheria

Dkt. Mwinyi: Natambua wajibu unaoambatana na dhima hii ni kuwaongoza Wazanzibari kwa misingi ya haki, uadilifu na usawa

Kama nilivyozungumza wakati wa kupokea matokeo leo naomba nirudie, lengo letu ni kuijenga #Zanzibar. Zanzibar mpya inajengwa na sisi bila kujali tofauti zetu

Dkt. Hussein Mwinyi: Kujitokeza kwenu kwa wingi kupiga kura ni kielelezo cha kukomaa kisiasa na kidemokrasia na kutambua kuwa Uchaguzi ndiyo njia sahihi ya kupata Viongozi wa nchi

Rais Magufuli ameniagiza nifikishe salamu zake za pongezi kwa kufanikisha uchaguzi kwa usalama
 
Kwa yanayoendelea Maalim Seif kwa sasa hawezi tena kukataa cheo cha Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar.

Funzo alilipata mwaka 2015 baada ya kugomea uchaguzi wa marudio akitegemea serikali ya Mapinduzi Zanzibar itakwama.

Yaani kwa sasa atawatosa ACT-Wazalendo kama watamshinikiza asiwe sehemu ya serikali ya Dkt. Mwinyi.
 
Hivi Maalim Sefu yuko wap anaruhusu vipi jamaa kuapishwa kirahisi.
 
Hongera sana Rais Dr. H Mwinyi

Nimemkumbuka mdau humu aliandikaga majanga.. sijui aliyatoa wapi akitaka watu wanachama wasimpitishe kugombea.. leo hii lazima analia.. maana alijisema kabisa yeye ni nani.. mahasira yalikuwa kibao..

💚💛💚💛💚
 
Asante, tunafuatilia kwa makini, na haswa hotuba yake ya leo, itaponya vidonda vyote vilivyosababishwa na uchaguzi huu, japo makovu yataendelea kubaki.
P
Una subiri u DC .njaa hizi[emoji28][emoji28][emoji28]
 
Paskal Mayalla!

umeshaiona hotuba yake?
Mkuu gango2 , no sijaiona hotuba yake, ila mimi ni trends reader mzuri. Huyu Dr. Mwinyi namfahamu kitambo toka tukiwa Shule pale Tambaza, ni muungwana sana na mstaarabu sana.

Hivyo kwa hali ya Zanzibar, atafanya tuu uungwana, atamteua Maalim Seif kuwa Makamu, na kwa vile ACT haina wajumbe wa kutosha kuunda GNU, atawateulia wawakilishi 5 wa ACT kuwa mawaziri wa GNU!.
P
 
Huna lolote. Kaa na ukabila wako wa kishamba. MAKOVU ya ZANZIBAR hayatibiki.
No hakuna makovu yanayotibika, ukiona kovu ujue kidonda kimeishapona!.

Vimepona vidonda vya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, na yamebaki makovu tuu, itakuwa hii michubuko tuu?.
p
 
No hakuna makovu yanayotibika, ukiona kovu ujue kidonda kimeishapona!.
Vimepona vidonda vya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, na yamebako makovu tuu, itakuwa hii michubuko tuu?.
p
Huna unachoelewa SNITCH mkubwa. Nakudaharau sana pamoja na umri mkubwa ulionao umebaki omba omba usiye na mbele wala nyuma. Mama yake Erick ataendelea kukucharaza laana hadi siku ya kiyama.
 
Vidonda vinatoka wapi na mtu ameshinda kwa kishindo? Tuendelee kuchapa kazi
Asante, tunafuatilia kwa makini, na haswa hotuba yake ya leo, itaponya vidonda vyote vilivyosababishwa na uchaguzi huu, japo makovu yataendelea kubaki.
P
 
Back
Top Bottom