Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 1,096
- 4,948
Kuna vijana wapo kwenye taasisi za kibiashara ambao kwa ujumla hawana exposure. Kuna mambo yanafanywa na taasisi za umma ambayo naamini siyo shirikishi.
Zanzibar Insurance wametoa tangazo kukataza wageni kuingia Zanzibar kuanzia Oktoba bila Insurance. Katika tangazo husika hakuna Sehemu wametaja hiyo mamlaka wamepata kwenye sheria gani ya nchi au kimataifa.
Hawa watu wa bima wameshindwa kufahamu kwamba wageni wanaomba visa kuja Tanzania na Duniani hakuna visa ya Zanzibar. Maana yake unapoweka masharti mapya yakuingia Zazibar masharti hayo lazima yazingatie sheria ikiwemo Katiba.
Wanaweza wakawa na wazo la kibiashara lakini si haki kwao kufanya maamuzi na kutangaza Duniani bila kupitishwa na Wizara ya Mambo ya Nje, Mwanasheria Mkuu wa Tanzania na hata Bunge.
Suala la kuingia Tanzania naamini lipo kwenye mambo ya Muungano. Wanaoruhusu kuingiza watu nchini ambao ni Uhamiaji watuambie wanaruhusu wageni kuingia Zanzibar kwa masharti tofauti na bara?
Lakini pia kiasi cha dola 40 kilichowekwa ni vigumu kulipwa na wageni wanaotoka nchi jirani au za Afrika. Je wamewalenga wazungu pekee au hata Waafrika? Ni nchi gàni Afrika ambayo bila Insurance huruhusiwi kuingia?
Kwa upande wa pili huduma za bima Tanzania ni mkataba kati ya mtoa bima na watoa huduma. Tunao mgogoro wa NHIF kushindwa kutoa huduma. Je, Zanzibar Insurance wanatumia watoa huduma gani kutoa matibabu na huduma nyingine wanazojinadi kuzitoa?
Je, mgeni anapotaka hizo huduma mifumo ya bima inaruhusu? Najaribu kupitia masharti ya bima hii bima ya sasa sioni ilipotajwa.
Niwaombe wasomi wetu waache hisia kwenye hoja zinazogusa diplomasia. Wakae ndani wafanye utafiti kwanza.
Tusipokuwa makini hiki kinachoitwa bima kwa wageni kinakwenda kuharibu mahusiano yetu na nchi nyingi. Wageni watagoma kwenda Zanzibar au wataingia Tanzania bara na kupewa ruhusa kisha wataenda Zanzibar kwa boti. Je, watazuiwa kuingia Zanzibar wakati Zanzibar ipo ndani ya Tanzania? Upo uwezekano Tanzania ikashrakiwa kwa kumzuia mgeni kutembea baadhi ya maeneo ya Tanzania .
Visiwa ni maeneo delicate Sana na vinapaswa kabla yakujiamulia jambo lazima liwe limepitiwa na wasomi na watu wenye busara.
Mwanasheria Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje mjadala unaoendelea huku nje kwenye safari za utalii ni mkubwa sana jitahidini kutoa ufafanuzi na kuthibitisha kwamba Tangazo husika ni halali.
Lakini najiuliza maswali kadhaa
Tangazo halipo kwenye website ya Wizara ya Mambo ya nje, Uhamiaji wala website za Balozi zetu nje. Tuelezeni je Tangazo ni halali?
Masharti na sheria zinakubaliana na tangazo husika au mtu wa bima kaandika kama anajiandikia yeye?
Lakini pia mamlaka yakuandika kwamba lazima ulipe Zanzibar Insyarance kuipata kwa nani? Monopolization?
Je, leo tukitaka kuja Tanzania tutakuwa kusubiri kupitishiwa viza au tutasubiri tupate insurance ?
Je, tukilipia insurance tukakataliwa visa nani atarejesha hizi fedha?
Je, makampuni makubwa yanayotoa huduma kama credit cards wanawatambua Zazibar Insurance?
Je, policy za credit cards zinakubaliana na policy ya hii insurance?
Natamani Wasomi na wanadiplomasia walisome Tangazo husika kwa muktadha wa Muungano na watuambie ni sheria gani imetoa hizi mamlaka? Linatekelezeka?
Zanzibar Insurance wametoa tangazo kukataza wageni kuingia Zanzibar kuanzia Oktoba bila Insurance. Katika tangazo husika hakuna Sehemu wametaja hiyo mamlaka wamepata kwenye sheria gani ya nchi au kimataifa.
Hawa watu wa bima wameshindwa kufahamu kwamba wageni wanaomba visa kuja Tanzania na Duniani hakuna visa ya Zanzibar. Maana yake unapoweka masharti mapya yakuingia Zazibar masharti hayo lazima yazingatie sheria ikiwemo Katiba.
Wanaweza wakawa na wazo la kibiashara lakini si haki kwao kufanya maamuzi na kutangaza Duniani bila kupitishwa na Wizara ya Mambo ya Nje, Mwanasheria Mkuu wa Tanzania na hata Bunge.
Suala la kuingia Tanzania naamini lipo kwenye mambo ya Muungano. Wanaoruhusu kuingiza watu nchini ambao ni Uhamiaji watuambie wanaruhusu wageni kuingia Zanzibar kwa masharti tofauti na bara?
Lakini pia kiasi cha dola 40 kilichowekwa ni vigumu kulipwa na wageni wanaotoka nchi jirani au za Afrika. Je wamewalenga wazungu pekee au hata Waafrika? Ni nchi gàni Afrika ambayo bila Insurance huruhusiwi kuingia?
Kwa upande wa pili huduma za bima Tanzania ni mkataba kati ya mtoa bima na watoa huduma. Tunao mgogoro wa NHIF kushindwa kutoa huduma. Je, Zanzibar Insurance wanatumia watoa huduma gani kutoa matibabu na huduma nyingine wanazojinadi kuzitoa?
Je, mgeni anapotaka hizo huduma mifumo ya bima inaruhusu? Najaribu kupitia masharti ya bima hii bima ya sasa sioni ilipotajwa.
Niwaombe wasomi wetu waache hisia kwenye hoja zinazogusa diplomasia. Wakae ndani wafanye utafiti kwanza.
Tusipokuwa makini hiki kinachoitwa bima kwa wageni kinakwenda kuharibu mahusiano yetu na nchi nyingi. Wageni watagoma kwenda Zanzibar au wataingia Tanzania bara na kupewa ruhusa kisha wataenda Zanzibar kwa boti. Je, watazuiwa kuingia Zanzibar wakati Zanzibar ipo ndani ya Tanzania? Upo uwezekano Tanzania ikashrakiwa kwa kumzuia mgeni kutembea baadhi ya maeneo ya Tanzania .
Visiwa ni maeneo delicate Sana na vinapaswa kabla yakujiamulia jambo lazima liwe limepitiwa na wasomi na watu wenye busara.
Mwanasheria Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje mjadala unaoendelea huku nje kwenye safari za utalii ni mkubwa sana jitahidini kutoa ufafanuzi na kuthibitisha kwamba Tangazo husika ni halali.
Lakini najiuliza maswali kadhaa
Tangazo halipo kwenye website ya Wizara ya Mambo ya nje, Uhamiaji wala website za Balozi zetu nje. Tuelezeni je Tangazo ni halali?
Masharti na sheria zinakubaliana na tangazo husika au mtu wa bima kaandika kama anajiandikia yeye?
Lakini pia mamlaka yakuandika kwamba lazima ulipe Zanzibar Insyarance kuipata kwa nani? Monopolization?
Je, leo tukitaka kuja Tanzania tutakuwa kusubiri kupitishiwa viza au tutasubiri tupate insurance ?
Je, tukilipia insurance tukakataliwa visa nani atarejesha hizi fedha?
Je, makampuni makubwa yanayotoa huduma kama credit cards wanawatambua Zazibar Insurance?
Je, policy za credit cards zinakubaliana na policy ya hii insurance?
Natamani Wasomi na wanadiplomasia walisome Tangazo husika kwa muktadha wa Muungano na watuambie ni sheria gani imetoa hizi mamlaka? Linatekelezeka?