Zanzibar: Kifo cha utata cha Katibu wa ACT-Wazalendo Jimbo la Chaani chaibua minong'ono

Zanzibar: Kifo cha utata cha Katibu wa ACT-Wazalendo Jimbo la Chaani chaibua minong'ono

Informer

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2006
Posts
1,606
Reaction score
6,672
ACT-Wazalendo wataka uchunguzi ufanyike.

Chama Cha ACT Wazalendo, Tunalitaka Jeshi la Polisi Kuhakikisha, Linawakamata na Kuwafikisha Katika Vyombo Vya Sheria, Wote Waliohusika na Kifo Cha Katibu wa ACT Wazalendo, Jimbo la Chaani, Ndugu ALI BAKARI ALI
Chama cha ACT Wazalendo, tumepokea kwa huzuni na masikitiko makubwa kitendo cha kutekwa, kushambuliwa na kutupwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi na kupelekea umauti kwa katibu wa Chama chetu wa Jimbo la Chaani Ndugu, ALI BAKARI ALI

Ndugu Ali Bakari Ali amekutwa na Umauti Usiku wa kuamkia jana tarehe 29/03/2024 katika Hospitali ya Rufaa ya Mnazimmoja, kutokana na Majeraha aliyoyapata baada ya kutekwa, kupigwa na kutupwa na watu wanaosaidikiwa kuwa ni Majambazi.

Mazingira ya kifo cha Ndugu Ali Bakar ni muendelezo wa vitendo vya uhalifu ambavyo vimekuwa vikitokea katika Mji wa Zanzibar na viunga vyake. Kama tulivyowahi kusema hapo siku za nyuma kwamba vitendo vya uhalifu wa kikatili vinavyotokea Zanzibar ni wa aina na mbinu mpya za kihalifu ambao haujazoeleka Zanzibar.

Kuendelea kwa vitendo hivyo kunaashiria uwepo wa vikundi vya kihalifu ambavyo vinajiimarisha kila siku bila Jeshi la Polisi kuonesha uwezo wa kuvidhibiti kwa kukinga au kufanya upelelezi unaopelekea wahusika kutiwa hatiani.

Kwa sababu tulizoeleza hapo juu, Chama Cha ACT Wazalendo, tumepokea taarifa hii kwa uzito wake, na tunalitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua za haraka za kuhakikisha wanawakamata wahusika wote wa tukio hili la kinyama la kukatisha uhai wa mtu na kuwafikisha wahalifu hao katika vyombo vya sheria.

Kutokana na matokeo ya uhalifu ya kutekwa, kupigwa na kuumizwa raia wasio na hatia na makundi ya
kihalifu yaliyoripotiwa hivi karibuni, yanatia mashaka na hali ya wasisawasi kwa usalama wa watu na mali

zao. Matokeo haya hayaoneshi taaswira njema kwa nchi na yanatia kila aina ya wasiwasi na mashaka kwa Wananchi wa Zanzibar. Hivyo basi Chama chetu tunalitaka jeshi la Polisi na Serikali kufanya yafuatayo:

1. Jeshi la Polisi kuimarisha kitengo chake cha ufuatiliaji wa matokeo kihalifu: Matokeo kama haya yaliyoripotiwa hivi karibuni yote yanaonesha Jeshi la Polisi kutokuwa na taarifa za Kientelijensia na badala yake yanawakuta matokeo haya kama ajali na kugeuka kuwa chombo cha dharura cha kuokoa kuliko chombo cha kuzuia matokeo ya uhalifu na ulinzi wa raia.

2. Tunalitaka Jeshi la Polisi kutoa taarifa kwa Umma baada ya Uchunguzi na kuwakamata wahalifu na Taarifa walizochukua.

3. Tunalitaka Jeshi la Polisi, kutoa ushauri wa kipolisi kwa raia (Police Advisory) juu ya aina za uhalifu uliopo na namna ya kuchukua hatua za kukinga uhalifu huo.

4. Tunaitaka Serikali iyachukulie matokeo haya yanayoripotiwa kwa uzito wake kwa kuimarisha vitengo vyote vya ulinzi ili kuweka ulinzi katika maeneo yote ya Zanzibar hasa katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na Skukuu ya Pasaka.

Chama cha ACT Wazalendo, tunalitaka jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi, katika maeneo yote ya Zanzibar kutokana na matukio ya kihalifu na kinyama yanayoendelea kufanyika na kuripotiwa hivi karibuni katika maeneo mbali mbali ya Zanzibar.

Imetolewa na:
Actrimariy Salim A. Bimani,
Katibu wa Habari, Uenezi, Mawasiliano na Umma,
Chama cha ACT-Wazalendo
30/03/2024

pages.jpg

page2.jpg
 
Katibu wa Jimbo la Chaani kutoka ACT Wazalendo Mkoa wa Kaskazi Unguja, Ali Bakari Ali (62) ameuawa kwa kuchomwa kisu.

ACT- Wazalendo kupitia Katibu wa Habari, Uenezi, Mawasiliano na Umma wa Chama cha ACT-Wazalendo, Salim Biman, wandai Ali ameuawa na majambazi, wakati Polisi mkoani humo wamedai waliofanya kitendo hiko wafanyabiashara wenzake ambao tayari wamekamatwa.

“Mazingira ya kifo cha Ali Bakari ni mwendelezo wa vitendo vya uhalifu ambavyo vimekuwa vikitokea katika mji wa Zanzibar, kuendela kuwepo vitendo hivyo kunaashiria vikundi vya kihalifu bila kudhibitiwa,” amesema Bimani na kulitaka jeshi la polisi kuhakikisha wahusika wanakamtwa na kuchukuliwa hatua.

Upande wa pili, Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Gaudianus Kamugisha akizungumza na Mwananchi Digital amesema waliomuua walikuwa wanafanya naye biashara hivyo walitofautiana kulipana madeni.

Kamanda Kamugisha amesema tukio hilo lilitokea Alhamisi ya Machi 28, 2024 eneo la Chaani stendi saa 11:30 jioni wilaya Kaskazini A.

Kwa mujibu wa kamanda Kamugisha waliotenda kosa hilo ni mfanyabiashara Khamis Nyange Omar (35) kwa kushirikiana na Feisali Makame Khamis (19) ambao kwa pamoja walimshambulia kwa kumkata na kitu chenye ncha kali mkono wake wa kulia na shingoni.

“Chanzo cha tukio hilo Bakari (marehemu) alikuwa anadaiwa na Khamis Nyange Sh1 milioni aliyomkopesha Februari ambapo wote walikuwa wakisambaza vyakula katika hoteli moja iliyopo maeneo ya Pwani Mchangani,” amesema Kamanda Kamugisha.
 
Katibu wa Jimbo la Chaani kutoka ACT Wazalendo Mkoa wa Kaskazi Unguja, Ali Bakari Ali (62) ameuawa kwa kuchomwa kisu.

ACT- Wazalendo wandai Ali ameuawa na majambazi, wakati Polisi mkoani humo wamedai waliofanya kitendo hiko wafanyabiashara wenzake ambao tayari wamekamatwa.

Taarifa ya kifo chake iliyotolewa leo Jumamosi Machi 30, 2024 na Katibu wa Habari, Uenezi, Mawasiliano na Umma wa Chama cha ACT-Wazalendo, Salim Biman, na kwamba Ali alifariki wakati akiendelea kupokea matibabu baada ya kutekwa, kupigwa na kutupwa na watu wanaosadikika kuwa majambazi.

“Mazingira ya kifo cha Ali Bakari ni mwendelezo wa vitendo vya uhalifu ambavyo vimekuwa vikitokea katika mji wa Zanzibar, kuendela kuwepo vitendo hivyo kunaashiria vikundi vya kihalifu bila kudhibitiwa,” amesema Bimani.

Amelitaka Jeshi la Polisi kuhakikisha wanalifuatilia tukio hilo la kinyama na wahusika wanakamatwa na kuchukuliwa hatua.

Wakati Bimani akisema hivyo, Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Gaudianus Kamugisha akizungumza na Mwananchi Digital amesema waliomuua walikuwa wanafanya naye biashara hivyo walitofautiana kulipana madeni.

Kamanda Kamugisha amesema tukio hilo lilitokea Alhamisi ya Machi 28, 2024 eneo la Chaani stendi saa 11:30 jioni wilaya Kaskazini A.

Kwa mujibu wa kamanda Kamugisha waliotenda kosa hilo ni mfanyabiashara Khamis Nyange Omar (35) kwa kushirikiana na Feisali Makame Khamis (19) ambao kwa pamoja walimshambulia kwa kumkata na kitu chenye ncha kali mkono wake wa kulia na shingoni.

“Chanzo cha tukio hilo Bakari (marehemu) alikuwa anadaiwa na Khamis Nyange Sh1 milioni aliyomkopesha Februari ambapo wote walikuwa wakisambaza vyakula katika hoteli moja iliyopo maeneo ya Pwani Mchangani,” amesema Kamanda Kamugisha.

Amesema, siku ya tukio watuhumiwa walikuwa na gari aina ya Noah walimfuata Bakari mjini alipokwenda kuchukua fedha ili walipane lakini walipofika Chaani hawakuweza kulipana na ndipo walimchoma kisu na kumtoa kwenye gari wakamtelekeza na kukimbia.

Hivyo, marehemu alikimbizwa hospitalini kutokana na majeraha hayo lakini alifariki dunia jana Machi 29, 2023 akiwa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Mnazi Mmoja.

Kwa mujibu wa maelezo ya Kamanda Kamugisha, gari la watuhumiwa lilichomwa moto na wananchi wenye hasira.

Licha ya watuhumiwa hao kukimbia baada ya kutenda kosa
2023. .................ndo wanasemaga Ramadan kareem
 
Katibu wa Jimbo la Chaani kutoka ACT Wazalendo Mkoa wa Kaskazi Unguja, Ali Bakari Ali (62) ameuawa kwa kuchomwa kisu.

ACT- Wazalendo kupitia Katibu wa Habari, Uenezi, Mawasiliano na Umma wa Chama cha ACT-Wazalendo, Salim Biman, wandai Ali ameuawa na majambazi, wakati Polisi mkoani humo wamedai waliofanya kitendo hiko wafanyabiashara wenzake ambao tayari wamekamatwa.

“Mazingira ya kifo cha Ali Bakari ni mwendelezo wa vitendo vya uhalifu ambavyo vimekuwa vikitokea katika mji wa Zanzibar, kuendela kuwepo vitendo hivyo kunaashiria vikundi vya kihalifu bila kudhibitiwa,” amesema Bimani na kulitaka jeshi la polisi kuhakikisha wahusika wanakamtwa na kuchukuliwa hatua.

Upande wa pili, Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Gaudianus Kamugisha akizungumza na Mwananchi Digital amesema waliomuua walikuwa wanafanya naye biashara hivyo walitofautiana kulipana madeni.

Kamanda Kamugisha amesema tukio hilo lilitokea Alhamisi ya Machi 28, 2024 eneo la Chaani stendi saa 11:30 jioni wilaya Kaskazini A.

Kwa mujibu wa kamanda Kamugisha waliotenda kosa hilo ni mfanyabiashara Khamis Nyange Omar (35) kwa kushirikiana na Feisali Makame Khamis (19) ambao kwa pamoja walimshambulia kwa kumkata na kitu chenye ncha kali mkono wake wa kulia na shingoni.

“Chanzo cha tukio hilo Bakari (marehemu) alikuwa anadaiwa na Khamis Nyange Sh1 milioni aliyomkopesha Februari ambapo wote walikuwa wakisambaza vyakula katika hoteli moja iliyopo maeneo ya Pwani Mchangani,” amesema Kamanda Kamugisha.
Kamanda kapumzike maelezo yamejitosheleza!
 
ACT-Wazalendo wataka uchunguzi ufanyike.

Chama Cha ACT Wazalendo, Tunalitaka Jeshi la Polisi Kuhakikisha, Linawakamata na Kuwafikisha Katika Vyombo Vya Sheria, Wote Waliohusika na Kifo Cha Katibu wa ACT Wazalendo, Jimbo la Chaani, Ndugu ALI BAKARI ALI
Chama cha ACT Wazalendo, tumepokea kwa huzuni na masikitiko makubwa kitendo cha kutekwa, kushambuliwa na kutupwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi na kupelekea umauti kwa katibu wa Chama chetu wa Jimbo la Chaani Ndugu, ALI BAKARI ALI

Ndugu Ali Bakari Ali amekutwa na Umauti Usiku wa kuamkia jana tarehe 29/03/2024 katika Hospitali ya Rufaa ya Mnazimmoja, kutokana na Majeraha aliyoyapata baada ya kutekwa, kupigwa na kutupwa na watu wanaosaidikiwa kuwa ni Majambazi.

Mazingira ya kifo cha Ndugu Ali Bakar ni muendelezo wa vitendo vya uhalifu ambavyo vimekuwa vikitokea katika Mji wa Zanzibar na viunga vyake. Kama tulivyowahi kusema hapo siku za nyuma kwamba vitendo vya uhalifu wa kikatili vinavyotokea Zanzibar ni wa aina na mbinu mpya za kihalifu ambao haujazoeleka Zanzibar.

Kuendelea kwa vitendo hivyo kunaashiria uwepo wa vikundi vya kihalifu ambavyo vinajiimarisha kila siku bila Jeshi la Polisi kuonesha uwezo wa kuvidhibiti kwa kukinga au kufanya upelelezi unaopelekea wahusika kutiwa hatiani.

Kwa sababu tulizoeleza hapo juu, Chama Cha ACT Wazalendo, tumepokea taarifa hii kwa uzito wake, na tunalitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua za haraka za kuhakikisha wanawakamata wahusika wote wa tukio hili la kinyama la kukatisha uhai wa mtu na kuwafikisha wahalifu hao katika vyombo vya sheria.

Kutokana na matokeo ya uhalifu ya kutekwa, kupigwa na kuumizwa raia wasio na hatia na makundi ya
kihalifu yaliyoripotiwa hivi karibuni, yanatia mashaka na hali ya wasisawasi kwa usalama wa watu na mali

zao. Matokeo haya hayaoneshi taaswira njema kwa nchi na yanatia kila aina ya wasiwasi na mashaka kwa Wananchi wa Zanzibar. Hivyo basi Chama chetu tunalitaka jeshi la Polisi na Serikali kufanya yafuatayo:

1. Jeshi la Polisi kuimarisha kitengo chake cha ufuatiliaji wa matokeo kihalifu: Matokeo kama haya yaliyoripotiwa hivi karibuni yote yanaonesha Jeshi la Polisi kutokuwa na taarifa za Kientelijensia na badala yake yanawakuta matokeo haya kama ajali na kugeuka kuwa chombo cha dharura cha kuokoa kuliko chombo cha kuzuia matokeo ya uhalifu na ulinzi wa raia.

2. Tunalitaka Jeshi la Polisi kutoa taarifa kwa Umma baada ya Uchunguzi na kuwakamata wahalifu na Taarifa walizochukua.

3. Tunalitaka Jeshi la Polisi, kutoa ushauri wa kipolisi kwa raia (Police Advisory) juu ya aina za uhalifu uliopo na namna ya kuchukua hatua za kukinga uhalifu huo.

4. Tunaitaka Serikali iyachukulie matokeo haya yanayoripotiwa kwa uzito wake kwa kuimarisha vitengo vyote vya ulinzi ili kuweka ulinzi katika maeneo yote ya Zanzibar hasa katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na Skukuu ya Pasaka.

Chama cha ACT Wazalendo, tunalitaka jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi, katika maeneo yote ya Zanzibar kutokana na matukio ya kihalifu na kinyama yanayoendelea kufanyika na kuripotiwa hivi karibuni katika maeneo mbali mbali ya Zanzibar.

Imetolewa na:
Actrimariy Salim A. Bimani,
Katibu wa Habari, Uenezi, Mawasiliano na Umma,
Chama cha ACT-Wazalendo
30/03/2024

Vitendo vya kihalifu vimeripotiwa kwa wingi sana Zanzibar
 
ACT-Wazalendo wataka uchunguzi ufanyike.

Chama Cha ACT Wazalendo, Tunalitaka Jeshi la Polisi Kuhakikisha, Linawakamata na Kuwafikisha Katika Vyombo Vya Sheria, Wote Waliohusika na Kifo Cha Katibu wa ACT Wazalendo, Jimbo la Chaani, Ndugu ALI BAKARI ALI
Chama cha ACT Wazalendo, tumepokea kwa huzuni na masikitiko makubwa kitendo cha kutekwa, kushambuliwa na kutupwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi na kupelekea umauti kwa katibu wa Chama chetu wa Jimbo la Chaani Ndugu, ALI BAKARI ALI

Ndugu Ali Bakari Ali amekutwa na Umauti Usiku wa kuamkia jana tarehe 29/03/2024 katika Hospitali ya Rufaa ya Mnazimmoja, kutokana na Majeraha aliyoyapata baada ya kutekwa, kupigwa na kutupwa na watu wanaosaidikiwa kuwa ni Majambazi.

Mazingira ya kifo cha Ndugu Ali Bakar ni muendelezo wa vitendo vya uhalifu ambavyo vimekuwa vikitokea katika Mji wa Zanzibar na viunga vyake. Kama tulivyowahi kusema hapo siku za nyuma kwamba vitendo vya uhalifu wa kikatili vinavyotokea Zanzibar ni wa aina na mbinu mpya za kihalifu ambao haujazoeleka Zanzibar.

Kuendelea kwa vitendo hivyo kunaashiria uwepo wa vikundi vya kihalifu ambavyo vinajiimarisha kila siku bila Jeshi la Polisi kuonesha uwezo wa kuvidhibiti kwa kukinga au kufanya upelelezi unaopelekea wahusika kutiwa hatiani.

Kwa sababu tulizoeleza hapo juu, Chama Cha ACT Wazalendo, tumepokea taarifa hii kwa uzito wake, na tunalitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua za haraka za kuhakikisha wanawakamata wahusika wote wa tukio hili la kinyama la kukatisha uhai wa mtu na kuwafikisha wahalifu hao katika vyombo vya sheria.

Kutokana na matokeo ya uhalifu ya kutekwa, kupigwa na kuumizwa raia wasio na hatia na makundi ya
kihalifu yaliyoripotiwa hivi karibuni, yanatia mashaka na hali ya wasisawasi kwa usalama wa watu na mali

zao. Matokeo haya hayaoneshi taaswira njema kwa nchi na yanatia kila aina ya wasiwasi na mashaka kwa Wananchi wa Zanzibar. Hivyo basi Chama chetu tunalitaka jeshi la Polisi na Serikali kufanya yafuatayo:

1. Jeshi la Polisi kuimarisha kitengo chake cha ufuatiliaji wa matokeo kihalifu: Matokeo kama haya yaliyoripotiwa hivi karibuni yote yanaonesha Jeshi la Polisi kutokuwa na taarifa za Kientelijensia na badala yake yanawakuta matokeo haya kama ajali na kugeuka kuwa chombo cha dharura cha kuokoa kuliko chombo cha kuzuia matokeo ya uhalifu na ulinzi wa raia.

2. Tunalitaka Jeshi la Polisi kutoa taarifa kwa Umma baada ya Uchunguzi na kuwakamata wahalifu na Taarifa walizochukua.

3. Tunalitaka Jeshi la Polisi, kutoa ushauri wa kipolisi kwa raia (Police Advisory) juu ya aina za uhalifu uliopo na namna ya kuchukua hatua za kukinga uhalifu huo.

4. Tunaitaka Serikali iyachukulie matokeo haya yanayoripotiwa kwa uzito wake kwa kuimarisha vitengo vyote vya ulinzi ili kuweka ulinzi katika maeneo yote ya Zanzibar hasa katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na Skukuu ya Pasaka.

Chama cha ACT Wazalendo, tunalitaka jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi, katika maeneo yote ya Zanzibar kutokana na matukio ya kihalifu na kinyama yanayoendelea kufanyika na kuripotiwa hivi karibuni katika maeneo mbali mbali ya Zanzibar.

Imetolewa na:
Actrimariy Salim A. Bimani,
Katibu wa Habari, Uenezi, Mawasiliano na Umma,
Chama cha ACT-Wazalendo
30/03/2024

Wapuuzi tu hawa siwalikuwa wanasema Magufuli ndiye alikuwa anateka na kuuwa watu, Sasahivi hicho kitu amna Sasa matamko ya nini kama Sasahivi maisha ni raha mstarehe, Maana aliyekuwa anawauwa hayupo tena?Ogopa wanasiasa matapeli akina Zitto Cop wameona akuna anayewazungumzia wanaanza swaga.
 
Wapuuzi tu hawa siwalikuwa wanasema Magufuli ndiye alikuwa anateka na kuuwa watu, Sasahivi hicho kitu amna Sasa matamko ya nini kama Sasahivi maisha ni raha mstarehe, Maana aliyekuwa anawauwa hayupo tena?Ogopa wanasiasa matapeli akina Zitto Cop wameona akuna anayewazungumzia wanaanza swaga.
Kila siku mimi huwa nawaambia kipindi cha JPM kila mwanasiasa akifa walisema kauliwa na JPM! Wabongo wengi ni zero brain na wepesi sana kuaminishwa ujinga! Saizi ngoja Zitto na ACT waje kuongea kama utasikia wanamshutumu Samia!
 
Kila siku mimi huwa nawaambia kipindi cha JPM kila mwanasiasa akifa walisema kauliwa na JPM! Wabongo wengi ni zero brain na wepesi sana kuaminishwa ujinga! Saizi ngoja Zitto na ACT waje kuongea kama utasikia wanamshutumu Samia!
Watakuambia njama zilianza 2017

Sent from my Nokia C10 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom