Zanzibar: Padri auawa kwa kupigwa Risasi!

Zanzibar: Padri auawa kwa kupigwa Risasi!

Status
Not open for further replies.

dada white

JF-Expert Member
Joined
Feb 22, 2012
Posts
1,228
Reaction score
514
Padri Evarist Mushi, ambaye ni paroko wa parokia ya Minara Miwili - Mtoni Zanzibar amepigwa risasi na watu wasiojulikana leo mida ya saa moja asubuhi akielekea kanisani kuongoza ibada.

Source: Radio Wapo
---
Padre E. Mushi Paroko wa parokia ya Minara Miwili Mtoni Zanzibar ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiofahamika asubuhi hii.

Ameuawa wakati akijiandaa kuingia kanisani akitokea kwenye gari yake ambapo ghafla ilitokea gari ndogo na waliokuwamo ndani ya gari ile wakamrushia risasi.

Kwa siku za hivi karibuni kumekuwako na vitisho vya wazi wazi dhidi ya wakristu huko visiwani Zanzibar ambapo inaelezwa kuwa jeshi la polisi halijafanya juhudi yoyote kuzuia tishio hili. Kumekuwapo na vipeperushi vinavyodai kuwa kupigwa risasi kwa padre Ambrose sio mwisho wa mapambano.

Taarifa hizi zimeripotiwa direct toka Zanzibar.

PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Nitazidi kuwapa updates kadri navyozidi kuwapa data.
 
Mungu ampe pumziko la amani,na wahusika watafutwe na kukamatwa na kupelekwa mbele ya sheria
 
Padri Mushi ambaye ni paroko wa parokia ya Minara Miwili - Zanzibar amepigwa risasi na watu wasiojulikana leo mida ya saa moja asubuhi akielekea kanisani.

Source: Radio Wapo ya jijini Dar es Salaam
 
Eeh Mwenyezi Mungu tusaidie tuondokane na vita hii inayowalenga watumishi wako. Mpunzishe kwa anami mtumishi wako Padre Mushi. Pole kwa ndugu wa marehemu na kanisa katoliki Tanzania na duniani nzima.
 
Mungu atusaidie kwenye hili wimbi la viongozi wa dini kupigwa risasi
 
Ni padre Mushi wa parokia ya mirara miwili Zanzibar. Amepigwa risasi akiwa anashuka kwenye gari tayari kwa kusalisha.
.
 
Wakubwa:

Taarifa zilipatika sasa hivi ni kuwa Paroko wa Kanisa la Katoliki Minara Mirefu Zanzibar, Evarist Mushi amefariki dunia baada ya kupigwa risasi saa 1.00 asubuhi na kufariki kabla hajafika hospitali ya Minazi Mirefu. Paroko huyu amepigwa risasi akishuka katika gari lake wakati akienda kuendesha ibada ya saa 3.00 leo.
 
padri wa kanisa katoliki la parokia la minara miwili amepigwa risasi na kuwawa..na watu wasiofahamika....na kumuuwa fadher evelist mushi....

tukio hiloo...limetokea asubuhi hii wakati father evarist mushi akielekea ...kanisani kwenda kusalishaa ghafla alivamiwa na kumpiga risasi na kuuwawa......

source:wapo redio.....breaking news kipindi cha patapata
 
Nimesikia wapo Radio ni kweli.Mungu ailaze Mahala pema peponi Padre Mushi.Hata mimi uzalendo umenishinda kabisa na inaniuma sana.
 
Alazwe mahali pema.....kisa cha kuuawa ni nini?
 
Tatizo ni nini hasa?kikwete ametufikisha pabaya sasa?wale dada zetu walio olewa na waislam waanze kudai talaka mapema

Tatizo umeshalitaja mbele ya swali lako au unataka upewe tatizo gani tena?
Tatizo ni kuwa waislamu hawatupendi na wana vita na chuki kubwa sana juu ya ukristo at the same time wakristo wanaendelea kulala usingizi fofofo wakizani hawa jamaa ni ndugu zetu.
 
Huu ni mpango maalumu naona,ngoja tuone mwisho wake
 
tuna hali mbaya kuliko tunavyojiona, tupo mbali sana....viongozi hawaijali nchi yetu wala hawafikirii vizazi vijavyo vitaishi kwenye mazingira gani, wanachowaza wao kutawala tu.!!!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom