Vitendo
JF-Expert Member
- Oct 23, 2009
- 582
- 103
NI miaka miwili sasa tangu nilipomsifia Balozi Ali Abeid Karume (Balozi Karume) kwa hatua yake ya kutangaza kugombea urais wa Zanzibar wakati utakapofika.
Wakati akiwa nchini kwa kazi maalum ya kiserikali Januari 2008, Balozi Karume ambaye anawakilisha Tanzania nchini Italia, alitangaza rasmi kuwa atagombea urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa 2010.
Katika tamko lake hilo, alisema wazi kuwa ameamua kutangaza mapema ili kuwapa wananchi muda wa kutosha kutafakari kwani anaamini ni haki yao kufanya uchambuzi kwa yeyote anayetaka kuwa kiongozi wao.
Hakueleza hasa ni mambo gani atayapa kipaumbele iwapo chama chake cha CCM kitamuidhinisha kugombea nafasi hiyo na atakapochaguliwa na wananchi.
Lakini alieleza kwamba jambo kubwa analoona halikwepeki kwa sasa akichaguliwa kuwa rais, ni kuunda serikali ya umoja wa kitaifa. Lengo ni pamoja na kuondoa siasa za chuki na kujumuisha kila mwananchi katika serikali ili iungwe mkono katika majukumu yake.
Wapo watu waliomshangaa Balozi Karume kwa tamko lake la kutaka kugombea urais. Wana sababu zao. Lakini nilimuunga mkono na kumfanyia mahojiano maalum.
Katika makala niliyoandika baada ya mahojiano naye yaliyofanyika mjini Dar es Salaam, nilisema alifanya jambo jema na kutangaza mapema nia yake ya kuja kuomba ridhaa ya wananchi wa Zanzibar.
Nilihimiza ule ulikuwa ni wakati mzuri kwa kila Mzanzibari kujipima uwezo wake na iwapo anadhani ana hamu ya kuongoza serikali ajitangaze mapema.
Faida ya mtu kujitokeza mapema na kutangaza nia yake ya kutafuta uongozi ambao unahitaji ridhaa ya wananchi ni moja kubwa: wananchi watamjadili kwa mapana na siku ya kuchagua watakuwa wameshafanya uamuzi.
Nilihimiza na kuhamasisha watu kujitokeza kumfuata Balozi Karume kwa sababu uchaguzi ni hatua inayopaswa kufanyika kwa uwazi na kwa mujibu wa taratibu.
Itakuwa uhuni mtu kukaa kimya kwa muda wote halafu akaja kujitokeza dakika za mwisho ambapo atakuwa amewanyima wananchi fursa ya haki ya kumchambua alivyo.
Isitoshe, ni kitendo cha ushetani mtu aliyetia nia ya kuja kugombea wadhifa mkubwa kama wa urais au ubunge na uwakilishi akanyamaza kimya asijitangaze hadharani mapema nia yake hiyo; kumbe chinichini anafanya kampeni.
Tunapoeleza mambo haya yanayohusu umma, huwa tumeshaangalia mbali kwa kuzingatia mazingira mbalimbali. Tunajua mienendo ya wanasiasa wa kileo na hasa hawa tuliowazoea.
Kwanza, inasikitisha kuwa hadi naandika makala hii miaka miwili kamili tangu wakati ule ni Balozi Karume peke yake aliyeweka wazi dhamira yake ya kuwania urais.
Pili, sijapata kusikia chama chochote cha siasa kilichopiga marufuku wanachama wake kujitangaza kwa yule anayetaka kugombea uongozi unaopiganiwa wakati wa uchaguzi mkuu wa taifa.
Kama kipo basi viongoz iwake watakuwa hawajui maana ya kuwapa fursa wanachama kujitangaza kwa wananchi au wanajua lakini chama kinataka kuja kuvuruga wapiga kura dakika za mwisho kwa kuwashtukiza na kuwalazimisha wachague hata jiwe.
Uzoefu unaonyesha vipo vyama vinavyonyonga wanachama wake dakika za mwisho kwa kuwakata pande na kuteua wengine kinyume na matakwa ya wapiga kura. Hii inadhoofisha demokrasia, ikiwemo ya kuridhia maoni ya watu.
Bahati njema Balozi Karume anaishi nje ya Zanzibar na Tanzania. Ni mara chache anakuja nchini kwa shughuli za kikazi au kwa likizo. Hafaidi sana uwanja wa siasa wa nyumbani kama wanavyofaidi wanasiasa wenzake.
Hivi kwa kujitangaza mapema si ameshajadiliwa na wapiga kura? Ametoa nafasi kwa wananchi kumchunguza tangu utotoni kwake hadi nafasi alipo sasa.
Tayari wananchi wanajua uwezo wake. Wanajua uadilifu wake. Wanajua namna anavyoingiliana na watu wa nchini kwake na wa kimataifa. Watu wanamjua Balozi Karume kwa mbivu na mbichi kufikia sasa.
Hivi yeye aliyejitangaza mapema na wale wana CCM kadhaa wanaotajwa tu katika vyombo vya habari kuwa watagombea urais, wakiwemo waliokana kutia nia hiyo wanapoulizwa na waandishi, yupi bora?
Hiyo haitoshi. Balozi Karume anajulikana amekuwa kiongozi kwa muda mrefu sasa hivyo kuwa katika nafasi ya mtu kuweza kukadiria mapato yake.
Sasa wale waliokaa kimya na wengine walioulizwa na kujibu kuwa ingali mapema lakini wamekuwa wakikusanya fedha hata nje ya nchi, nani ana afadhali hapa?
Ukiacha Balozi Karume, orodha ya wenye shauku ya kutafuta urais kwa Zanzibar wanapata kumi. Wote hawajatangaza hadharani lakini harakati zao zinathibitisha wanaunyatia urais.
Na ni hawa wanaofanya kampeni chafu zinazohusisha na mipango ovu ya kugawa wanachama wa CCM ili kutimiza dhamira zao za kutaka kiti cha Ikulu.
Umma unashuhudia namna watu wenye shauku ya urais wanavyopita kwenye mikusanyiko na kugawa fedha bila ya kusema ni za nini.
Zipo taarifa kwamba kuna makada wa CCM wamefika hadi Uarabuni kutembeza bakuli kwa wahisani wao ili kuja kuzitapanya kwa watu na kutumainia kuungwa mkono. Tayari wameanza kuzigawa kwa makada wenzao.
Wapo baadhi ya makada wanaotafuta urais wanawatumia waandishi wa habari wenzangu kuwatajataja magazetini na katika televisheni ili kujikurubisha na wapiga kura.
Makada walio mawaziri wanajiundia ziara kila siku za Pemba na wanalipa waandishi wa habari fedha mchezo tu kufuatana nao kwa ajili ya kuwapamba waonekane wanafanya kazi za wananchi.
Ukweli ni kwamba makada wengi sasa wanazunguka nchi kujijenga kisiasa kwa ajili ya tamaa ya urais. Katika kujijenga huko wanadiriki kuchafua wenzao bila ya aibu.
Kwa bahati mbaya sana, wanafanya hivyo kwa kutumia fedha za wananchi, magari ya serikali na muda waliopaswa kutumikia wananchi. Huku ni kutenda haramu, jambo lisilokubalika.
Nilipomsikia Waziri Kiongozi Shamsi Vuai Nahodha anasisitiza watu waache kufikiria urais, naye akigoma kutangaza kuwa anautaka urais, nilicheka. Lakini nilihuzunika kwa kuwa ninayoyasikia kumhusu yeye yanachefua.
Makada wengi wa CCM wanaoutaka urais wanafanya kampeni za kibaguzi na kimajimbo na kupoteza raslimali za umma na hakuna anayegomba.
Hata pale rais anapokemea mtindo huu hakuna anayejali. Wanaendelea huku wakisema, Hana analo, anamaliza muda wake aondoke.
Makada wanaotajwa sana kuwania urais ni pamoja na Shamsi, mtangulizi wake, Dk. Mohamed Gharib Bilal, Muhammed Seif Khatib, Haroun Ali Suleiman, Ali Juma Shamhuna na Dk. Hussein Mwinyi.
Wananchi wawatie adabu makada wa aina hii. Wakatae kununuliwa kwa fedha au kwa kitu kingine chochote. Uadilifu wa kiongozi lazima utokane na historia yake ya utendaji na siyo uadilifu wa kutengeneza ukingoni kabla ya uchukuaji fomu za kuomba uteuzi kuanza.
Zanzibar inahitaji kiongozi aliyetukuka. Awe mwema kwa maneno na vitendo. Atambuwe na kuthamini wajibu wake kwa atakaokuja kuwaongoza.
Zanzibar inahitaji kiongozi mpenda nchi na watu wake; mwenye uchungu itokeapo shida; mshirika siyo mtenganishi; anayetoa uongozi unapotakiwa; anayefikiria maendeleo ya watu siyo ya familia yake na rafiki zake.
Source :MWanahalisi by Jabir Idrisa.
Wakati akiwa nchini kwa kazi maalum ya kiserikali Januari 2008, Balozi Karume ambaye anawakilisha Tanzania nchini Italia, alitangaza rasmi kuwa atagombea urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa 2010.
Katika tamko lake hilo, alisema wazi kuwa ameamua kutangaza mapema ili kuwapa wananchi muda wa kutosha kutafakari kwani anaamini ni haki yao kufanya uchambuzi kwa yeyote anayetaka kuwa kiongozi wao.
Hakueleza hasa ni mambo gani atayapa kipaumbele iwapo chama chake cha CCM kitamuidhinisha kugombea nafasi hiyo na atakapochaguliwa na wananchi.
Lakini alieleza kwamba jambo kubwa analoona halikwepeki kwa sasa akichaguliwa kuwa rais, ni kuunda serikali ya umoja wa kitaifa. Lengo ni pamoja na kuondoa siasa za chuki na kujumuisha kila mwananchi katika serikali ili iungwe mkono katika majukumu yake.
Wapo watu waliomshangaa Balozi Karume kwa tamko lake la kutaka kugombea urais. Wana sababu zao. Lakini nilimuunga mkono na kumfanyia mahojiano maalum.
Katika makala niliyoandika baada ya mahojiano naye yaliyofanyika mjini Dar es Salaam, nilisema alifanya jambo jema na kutangaza mapema nia yake ya kuja kuomba ridhaa ya wananchi wa Zanzibar.
Nilihimiza ule ulikuwa ni wakati mzuri kwa kila Mzanzibari kujipima uwezo wake na iwapo anadhani ana hamu ya kuongoza serikali ajitangaze mapema.
Faida ya mtu kujitokeza mapema na kutangaza nia yake ya kutafuta uongozi ambao unahitaji ridhaa ya wananchi ni moja kubwa: wananchi watamjadili kwa mapana na siku ya kuchagua watakuwa wameshafanya uamuzi.
Nilihimiza na kuhamasisha watu kujitokeza kumfuata Balozi Karume kwa sababu uchaguzi ni hatua inayopaswa kufanyika kwa uwazi na kwa mujibu wa taratibu.
Itakuwa uhuni mtu kukaa kimya kwa muda wote halafu akaja kujitokeza dakika za mwisho ambapo atakuwa amewanyima wananchi fursa ya haki ya kumchambua alivyo.
Isitoshe, ni kitendo cha ushetani mtu aliyetia nia ya kuja kugombea wadhifa mkubwa kama wa urais au ubunge na uwakilishi akanyamaza kimya asijitangaze hadharani mapema nia yake hiyo; kumbe chinichini anafanya kampeni.
Tunapoeleza mambo haya yanayohusu umma, huwa tumeshaangalia mbali kwa kuzingatia mazingira mbalimbali. Tunajua mienendo ya wanasiasa wa kileo na hasa hawa tuliowazoea.
Kwanza, inasikitisha kuwa hadi naandika makala hii miaka miwili kamili tangu wakati ule ni Balozi Karume peke yake aliyeweka wazi dhamira yake ya kuwania urais.
Pili, sijapata kusikia chama chochote cha siasa kilichopiga marufuku wanachama wake kujitangaza kwa yule anayetaka kugombea uongozi unaopiganiwa wakati wa uchaguzi mkuu wa taifa.
Kama kipo basi viongoz iwake watakuwa hawajui maana ya kuwapa fursa wanachama kujitangaza kwa wananchi au wanajua lakini chama kinataka kuja kuvuruga wapiga kura dakika za mwisho kwa kuwashtukiza na kuwalazimisha wachague hata jiwe.
Uzoefu unaonyesha vipo vyama vinavyonyonga wanachama wake dakika za mwisho kwa kuwakata pande na kuteua wengine kinyume na matakwa ya wapiga kura. Hii inadhoofisha demokrasia, ikiwemo ya kuridhia maoni ya watu.
Bahati njema Balozi Karume anaishi nje ya Zanzibar na Tanzania. Ni mara chache anakuja nchini kwa shughuli za kikazi au kwa likizo. Hafaidi sana uwanja wa siasa wa nyumbani kama wanavyofaidi wanasiasa wenzake.
Hivi kwa kujitangaza mapema si ameshajadiliwa na wapiga kura? Ametoa nafasi kwa wananchi kumchunguza tangu utotoni kwake hadi nafasi alipo sasa.
Tayari wananchi wanajua uwezo wake. Wanajua uadilifu wake. Wanajua namna anavyoingiliana na watu wa nchini kwake na wa kimataifa. Watu wanamjua Balozi Karume kwa mbivu na mbichi kufikia sasa.
Hivi yeye aliyejitangaza mapema na wale wana CCM kadhaa wanaotajwa tu katika vyombo vya habari kuwa watagombea urais, wakiwemo waliokana kutia nia hiyo wanapoulizwa na waandishi, yupi bora?
Hiyo haitoshi. Balozi Karume anajulikana amekuwa kiongozi kwa muda mrefu sasa hivyo kuwa katika nafasi ya mtu kuweza kukadiria mapato yake.
Sasa wale waliokaa kimya na wengine walioulizwa na kujibu kuwa ingali mapema lakini wamekuwa wakikusanya fedha hata nje ya nchi, nani ana afadhali hapa?
Ukiacha Balozi Karume, orodha ya wenye shauku ya kutafuta urais kwa Zanzibar wanapata kumi. Wote hawajatangaza hadharani lakini harakati zao zinathibitisha wanaunyatia urais.
Na ni hawa wanaofanya kampeni chafu zinazohusisha na mipango ovu ya kugawa wanachama wa CCM ili kutimiza dhamira zao za kutaka kiti cha Ikulu.
Umma unashuhudia namna watu wenye shauku ya urais wanavyopita kwenye mikusanyiko na kugawa fedha bila ya kusema ni za nini.
Zipo taarifa kwamba kuna makada wa CCM wamefika hadi Uarabuni kutembeza bakuli kwa wahisani wao ili kuja kuzitapanya kwa watu na kutumainia kuungwa mkono. Tayari wameanza kuzigawa kwa makada wenzao.
Wapo baadhi ya makada wanaotafuta urais wanawatumia waandishi wa habari wenzangu kuwatajataja magazetini na katika televisheni ili kujikurubisha na wapiga kura.
Makada walio mawaziri wanajiundia ziara kila siku za Pemba na wanalipa waandishi wa habari fedha mchezo tu kufuatana nao kwa ajili ya kuwapamba waonekane wanafanya kazi za wananchi.
Ukweli ni kwamba makada wengi sasa wanazunguka nchi kujijenga kisiasa kwa ajili ya tamaa ya urais. Katika kujijenga huko wanadiriki kuchafua wenzao bila ya aibu.
Kwa bahati mbaya sana, wanafanya hivyo kwa kutumia fedha za wananchi, magari ya serikali na muda waliopaswa kutumikia wananchi. Huku ni kutenda haramu, jambo lisilokubalika.
Nilipomsikia Waziri Kiongozi Shamsi Vuai Nahodha anasisitiza watu waache kufikiria urais, naye akigoma kutangaza kuwa anautaka urais, nilicheka. Lakini nilihuzunika kwa kuwa ninayoyasikia kumhusu yeye yanachefua.
Makada wengi wa CCM wanaoutaka urais wanafanya kampeni za kibaguzi na kimajimbo na kupoteza raslimali za umma na hakuna anayegomba.
Hata pale rais anapokemea mtindo huu hakuna anayejali. Wanaendelea huku wakisema, Hana analo, anamaliza muda wake aondoke.
Makada wanaotajwa sana kuwania urais ni pamoja na Shamsi, mtangulizi wake, Dk. Mohamed Gharib Bilal, Muhammed Seif Khatib, Haroun Ali Suleiman, Ali Juma Shamhuna na Dk. Hussein Mwinyi.
Wananchi wawatie adabu makada wa aina hii. Wakatae kununuliwa kwa fedha au kwa kitu kingine chochote. Uadilifu wa kiongozi lazima utokane na historia yake ya utendaji na siyo uadilifu wa kutengeneza ukingoni kabla ya uchukuaji fomu za kuomba uteuzi kuanza.
Zanzibar inahitaji kiongozi aliyetukuka. Awe mwema kwa maneno na vitendo. Atambuwe na kuthamini wajibu wake kwa atakaokuja kuwaongoza.
Zanzibar inahitaji kiongozi mpenda nchi na watu wake; mwenye uchungu itokeapo shida; mshirika siyo mtenganishi; anayetoa uongozi unapotakiwa; anayefikiria maendeleo ya watu siyo ya familia yake na rafiki zake.
Source :MWanahalisi by Jabir Idrisa.