Zanzibar wanatupa wakati mgumu sana kwenye uandaaji wa katiba hii

Zanzibar wanatupa wakati mgumu sana kwenye uandaaji wa katiba hii

Kimbakuli

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2013
Posts
408
Reaction score
435
Walishatengeneza Katiba inayokiuka Katiba ya JMT, Nchi yao ndogo(ni wachache sana) hatuwezi kugawana madaraka sawa
 
Walishatengeneza Katiba inayokiuka Katiba ya JMT, Nchi yao ndogo(ni wachache sana) hatuwezi kugawana madaraka sawa

Sio katiba tu, wana Jeshi lao, Rais wao, Bunge lao, mipaka ya nchi yao imelezwa bayana,
 
Kuna mambo ni kujitakia!
Kwanini watanganyika wasiandamane kuukataa muungano??????
 
Hata mi nashangaa sana Bw Masha Watanganyika tunapelekeshwa sana na hawa jamaa afu tumenyamaza tu 4what, c'mon tumechoka
 
bila shaka wewe ulisoma political science pale udsm tena nahisi umefundishwa na prof samuel mushi (r.i.p.) tena yaonesha ulimsoma vizuri nnoli ukwudiba

Sovereignity is not determined by neither demography nor territory
 
Kuna mambo ni kujitakia!
Kwanini watanganyika wasiandamane kuukataa muungano??????

Katika makala yake yaitwayo "Nyerere Alitunusuru" yaliyochapishwa katika Gazeti la Sura ya Mtanzania la kuanzia 10/10/13 Comred Ali Sultan ameandika:

Karume hakuwapenda ‘Wasomi', na hakuwa akiwaamini kabisa. Hata ukiangalia wengi wa Viongozi wa ASP waliofungwa na Karume walikuwa ni wale Wasomi, kama Othman Shariff.

Hapana shaka kuwa Comred Ali Sultan alimjua vizuri Karume kwani alikuwa naye katika "Baraza la Mapinduzi" na aliwahi hata kuwa Waziri wa Ilimu wakati wa utawala wa Karume.

La muhimu hapa ni kuwa Raisi Karume alikuwa hakusoma, hakuwapenda wasomi na hakutaka ushauri wa wasomi hata juu ya mambo ambayo yaliwahitajia wasomi kuyasoma kuyachambua, kubadilisha na hata Kumshauri Rais ayakatae iwapo wanayaona yataleta athari mbaya kwa Zanzibar.

Si Ali Sultani tu bali muhimu kwa Wazanzibari ni kuwa Nyerere pia aliujua upungufu huu wa Karume na kuutumilia upungufu huo kumtilisha saini mambo ambayo Karume, kwa hakika hakuyajua athari zake baadaye. Nyerere kwa ilimu yake na kwa ujanja wake, kwanza alifanya mazingaombwe ili Karume amwondoshe Dorado, ambaye alikuwa Mwanasharia mkuu wa Serikali ya Zanzibar, asihudhurie mikutano muhimu na hivyo kumnyima Karume usia mwema na wa lazima katika mikataba yote muhimu, na huu wa muungano ndio uliokuwa muhimu kabisa wakati huo.

Nyerere alimtumilia Karume saikolojia kumtilisha sahihi mambo aliyokuwa hakuwa na kipawa cha kuelewa athari zake siku za siku za mbele. Haya mawili pekee yanatosha kuufanya mswada wote wa muungano "nul and void" yaani batil, au kuwa hauna uhalali wowote mbele mahkama yenye kufuata sharia za haki na uadilifu.

Hapana shaka yoyote, ukipeleka kwenye mahakama yenye kuamua kwa haki na uadilifu, ni mara moja itaamua kuwa yote aliyoyasaini Karume kuwa ni batil. Kila mwana sharia anayeelewa maana ya haki na uadilifu anayaelewa haya.



Ukiongeza pia kuwa Karume hakupata idhini ya Wazanzibari kwa kura ya maoni kuiunganisha Zanzibar na Tanganyika ndiyo kabisa aliyoyatia saini yake hayakuwa na uhalali.

Nchi huunganishwa kwa njia mbili, moja ni ya kuulizwa wananchi kama wanautaka muungano ama la. Wasipoutaka, muungano hauwezi kuwa.

Wazanzibari hawakushauriwa na hili pia linaufanya mkataba wa muungano na muungano wenyewe "nul and void" kisharia.

Njia ya pili ni ya kuiteka nchi kijeshi, na njia hii pia haikubaliki kisharia.

Njia ya tatu ni ya Kinyerere na wafuasi wake, ya kuiteka nchi kwa ghilba, kidogokidogo kama panya anavyokula nyama ya aliyelala kwa kutafuna na kupuliza. Hili pia halikubaliki.



Kwa Wazanzibari kuzungumzia kipengee cha mkataba batil kama kwamba mkataba wenyewe una uhalali ni kujitia katika mitego ya Nyerere na wafuasi wake.

Iwapo tunakubaliana kuwa Karume hakufahamu alichokisaini, hakujua athari zake, na mawakili wake waliokuwa na uwezo wa kuelewa na kumshauri ipasavyo walifanyiwa mazingaomwe na Nyerere hata wakatolewa kwenye mikutano ili ipatikane saini ya Karume kwa wepesi inaufanya mkataba huo kuwa batil.

Na mkipeleleza mtaona pia baada ya hapo pia sehemu nyingi za kuinyima Zanzibar haki zake ziliongezwa kinyemela.

Wafuasi wa Nyerere wanategemea kuwa madamu kuna mswada na ndani yake kuna sharia hizo, basi sharia hizo ni za kihalali hata iwapo zimepatikana kwa udanganyifu na ghilba.

Ni juu ya Wazanzibari na waliondugu zao wa kweli walioko Tanganyika kuhoji na kuukataa mkataba ulipatikana kwa ghilba na bila ya kushauriwa wananchi wahusika.



Jaribu ufikirie kuna nduguyo ambaye hakusoma na ana shamba lake anakodisha na anategemea kupata pato la kumwendeshea maisha yake kutokana na mali yake hiyo; akaja mtu akamvuta pembeni na kumwambia mimi nitakupa shilingi kadha wa kadha unikodishe shamba lako lakini sharti yangu uutie saini yako mkataba huu, bila ya kumshauri nduguyo aliyesoma kwani nduguyo mkorofi sana na hakutakii kheri, ni mimi ninayekutakia kheri na utafaidika pakubwa ukitia dole lako kama ni saini ya kuukubali mkataba huu.

Jee, wewe nduguye ukaja ukamwona nduguyo anafukarika kwa kunyang'anywa kwa ghilba mali yake na mjanja kwa sababu kamtilisha saini yake huku hajui kuwa mkataba ulikuwa na vipengee vya kumyang'anya nduguyo haki zake, utaukubali mkataba kama huo uliojaa dhulma uliosainiwa na nduguyo aliyekuwa hakusoma na hakufahamu sawasawa nini anachokisaini?

Jee, mktaba huo utakubaliwa katika mahkama yenye kufuatilia haki na uadilifu? Lakini hivyo ndivyo wanavyoshikilia maloya wa Nyerere katika kutaka kudhulumu haki na mali za Zanzibar

. Si mnawaona wanakakania kuwa maliasilia ni haki ya Tanzania na si ya Zanzibar ingawa mali hayo yako Zanzibar!
 
Katika makala yake yaitwayo "Nyerere Alitunusuru" yaliyochapishwa katika Gazeti la Sura ya Mtanzania la kuanzia 10/10/13 Comred Ali Sultan ameandika:

Karume hakuwapenda ‘Wasomi', na hakuwa akiwaamini kabisa. Hata ukiangalia wengi wa Viongozi wa ASP waliofungwa na Karume walikuwa ni wale Wasomi, kama Othman Shariff.

Hapana shaka kuwa Comred Ali Sultan alimjua vizuri Karume kwani alikuwa naye katika "Baraza la Mapinduzi" na aliwahi hata kuwa Waziri wa Ilimu wakati wa utawala wa Karume.

La muhimu hapa ni kuwa Raisi Karume alikuwa hakusoma, hakuwapenda wasomi na hakutaka ushauri wa wasomi hata juu ya mambo ambayo yaliwahitajia wasomi kuyasoma kuyachambua, kubadilisha na hata Kumshauri Rais ayakatae iwapo wanayaona yataleta athari mbaya kwa Zanzibar.

Si Ali Sultani tu bali muhimu kwa Wazanzibari ni kuwa Nyerere pia aliujua upungufu huu wa Karume na kuutumilia upungufu huo kumtilisha saini mambo ambayo Karume, kwa hakika hakuyajua athari zake baadaye. Nyerere kwa ilimu yake na kwa ujanja wake, kwanza alifanya mazingaombwe ili Karume amwondoshe Dorado, ambaye alikuwa Mwanasharia mkuu wa Serikali ya Zanzibar, asihudhurie mikutano muhimu na hivyo kumnyima Karume usia mwema na wa lazima katika mikataba yote muhimu, na huu wa muungano ndio uliokuwa muhimu kabisa wakati huo.

Nyerere alimtumilia Karume saikolojia kumtilisha sahihi mambo aliyokuwa hakuwa na kipawa cha kuelewa athari zake siku za siku za mbele. Haya mawili pekee yanatosha kuufanya mswada wote wa muungano "nul and void" yaani batil, au kuwa hauna uhalali wowote mbele mahkama yenye kufuata sharia za haki na uadilifu.

Hapana shaka yoyote, ukipeleka kwenye mahakama yenye kuamua kwa haki na uadilifu, ni mara moja itaamua kuwa yote aliyoyasaini Karume kuwa ni batil. Kila mwana sharia anayeelewa maana ya haki na uadilifu anayaelewa haya.



Ukiongeza pia kuwa Karume hakupata idhini ya Wazanzibari kwa kura ya maoni kuiunganisha Zanzibar na Tanganyika ndiyo kabisa aliyoyatia saini yake hayakuwa na uhalali.

Nchi huunganishwa kwa njia mbili, moja ni ya kuulizwa wananchi kama wanautaka muungano ama la. Wasipoutaka, muungano hauwezi kuwa.

Wazanzibari hawakushauriwa na hili pia linaufanya mkataba wa muungano na muungano wenyewe "nul and void" kisharia.

Njia ya pili ni ya kuiteka nchi kijeshi, na njia hii pia haikubaliki kisharia.

Njia ya tatu ni ya Kinyerere na wafuasi wake, ya kuiteka nchi kwa ghilba, kidogokidogo kama panya anavyokula nyama ya aliyelala kwa kutafuna na kupuliza. Hili pia halikubaliki.



Kwa Wazanzibari kuzungumzia kipengee cha mkataba batil kama kwamba mkataba wenyewe una uhalali ni kujitia katika mitego ya Nyerere na wafuasi wake.

Iwapo tunakubaliana kuwa Karume hakufahamu alichokisaini, hakujua athari zake, na mawakili wake waliokuwa na uwezo wa kuelewa na kumshauri ipasavyo walifanyiwa mazingaomwe na Nyerere hata wakatolewa kwenye mikutano ili ipatikane saini ya Karume kwa wepesi inaufanya mkataba huo kuwa batil.

Na mkipeleleza mtaona pia baada ya hapo pia sehemu nyingi za kuinyima Zanzibar haki zake ziliongezwa kinyemela.

Wafuasi wa Nyerere wanategemea kuwa madamu kuna mswada na ndani yake kuna sharia hizo, basi sharia hizo ni za kihalali hata iwapo zimepatikana kwa udanganyifu na ghilba.

Ni juu ya Wazanzibari na waliondugu zao wa kweli walioko Tanganyika kuhoji na kuukataa mkataba ulipatikana kwa ghilba na bila ya kushauriwa wananchi wahusika.



Jaribu ufikirie kuna nduguyo ambaye hakusoma na ana shamba lake anakodisha na anategemea kupata pato la kumwendeshea maisha yake kutokana na mali yake hiyo; akaja mtu akamvuta pembeni na kumwambia mimi nitakupa shilingi kadha wa kadha unikodishe shamba lako lakini sharti yangu uutie saini yako mkataba huu, bila ya kumshauri nduguyo aliyesoma kwani nduguyo mkorofi sana na hakutakii kheri, ni mimi ninayekutakia kheri na utafaidika pakubwa ukitia dole lako kama ni saini ya kuukubali mkataba huu.

Jee, wewe nduguye ukaja ukamwona nduguyo anafukarika kwa kunyang'anywa kwa ghilba mali yake na mjanja kwa sababu kamtilisha saini yake huku hajui kuwa mkataba ulikuwa na vipengee vya kumyang'anya nduguyo haki zake, utaukubali mkataba kama huo uliojaa dhulma uliosainiwa na nduguyo aliyekuwa hakusoma na hakufahamu sawasawa nini anachokisaini?

Jee, mktaba huo utakubaliwa katika mahkama yenye kufuatilia haki na uadilifu? Lakini hivyo ndivyo wanavyoshikilia maloya wa Nyerere katika kutaka kudhulumu haki na mali za Zanzibar

. Si mnawaona wanakakania kuwa maliasilia ni haki ya Tanzania na si ya Zanzibar ingawa mali hayo yako Zanzibar!
Huo mkataba wa muungano ni dhulma iliyopitiliza kiasi kwamba hata binamu zetu walioko tanganyika nao hawautaki pamoja na muswada huu wa rasimu ya katiba mpya wa ghiliba unaotaka kupenyezwa tena!
 
"Sovereignity is not determined by neither demography nor territory" Supported 101% Nawaomba msome ujumbe wa Raza kwa Wabara au Watanganyika wote: Mohamed Raza (Mwakilishi wa Jimbo La Uzini) wakati wamkutano wake na wandishi katika ukumbi wa Grand Palace Hotel Malindi MjiniZanzibar. (Picha na Makame Mshenga-Maeleza Zanzibar).
Na Maelezo Zanzibar 13/10/2013
Wazanzibari wameombwa kuendelea kuungana katikakupigani maslahi ya Zanzibar katika Muungano, na kwamba Zanzibar bado inayonafasi ya kuwa huru kiuchumi kupitia mchakato wa Katiba Mpya.
Wito huo umetolewa na Mwananchi mzalendo, MohamedrazaHassan Dharamsi alipokuwa akizungumza na Wanahabari kuhusu mambo mbalimbaliyanayohusu Zanzibar katika mkutano alioufanya Hoteli ya Grand Palace Forodhanimjini Zanzibar.
Amesema yeye anaamini katika Muungano na sio Utenganona kudai kuwa kama Muundo wa Serikali mbili umeshindikana ni vyema ukawepoMfumo mpya wa Muundo wa Serikali tatu.
Ameongeza kuwa kinachotakiwa na Wazanzibari waliowengi ni kuona nchi yao ya Zanzibar inakuwa huru kujiamulia mambo yake yaKiuchumi bila kuitegemea Tanganyika.
"Sisi tupo huru lakini hatupo huru kiuchumitunataka Zanzibar ijiamulie mambo yake yote yanayohusu uchumi, kuwa na Benderahaitoshi kuwa huru Uchumi ndio uhuru" Aliongeza Raza.
Kuhusu Mchakato wa Katiba mpya unavyoendelea, Razaamemshauri Rais Shein kuwaita Wasaidizi wake Makamu wa Kwanza Maalim Seif naMakamu wa Pili Balozi Seif kushauriana na kuwa na Kauli moja juu ya hatma yaZanzibar.
"Mi namuomba Rais wangu Dkt. Shein akutane naMaalim Seif na Balozi Seif wajifungie Chumbani wajadiliane vyakutosha kishatupate pakusimamia sio kila mtu kusema vyake kuhusu Katiba Mpya"
Akizungumzia kuhusu Kisiwa cha Fungu Mbaraka, amesemaKisiwa hicho ni mali ya Zanzibar kama maelezo yalivyotolewa na Mwanasheria Mkuuwa Zanzibar na kwamba asilani Tanganyika haina uwezo wa kukihodhi kisiwa hicho.
"Ndugu zangu waandishi ushahidi upo wa kutoshakuwa Fungu Mbaraka ni Mali ya Zanzibar lakini kwa vile kisiwa hicho kipo kwenyekitalu namba nane cha Mafuta ndugu zetu Wabara wanadai ni Kisiwa chao, hiihaikubaliki maisha" alisisitiza Raza.
Amesema inashnagaza kila Zanzibar inavyotakakujikwamua kiuchumi baadhi ya viongozi wa Tanganyika wamekuwa wakiwekapingamizi jambo ambalo si jema kwa mustakabali wa Muungano na Taifa kiujula.
Ameongeza kuwa hivi karibuni kuna Kiongozi alidai RaisShien kavunja Sheria kwa kusaini Mkataba wa Kuchimba Mafuta, na kuongeza kuwakiongozi huyo alipaswa kumuomba Radhi Rais Shein.
"Huyu alipaswa kumuomba Radhi Rais Shein,kwani waowamevunja Sheria mara ngapi? Leo kusaini Mafuta jambo ambalo limekubaliwa ndioimekuwa tatizo" alihoji Raza ambaye pia ni Mwakilishi wa Uzini.
Raza ameongeza kuwa ataendelea kupigania Maslahi yaZanzibar bila kuogopa Vitisho vyovyote kwa kufuata misingi ya Katiba na Sheriaza nchi.
Kuhusu Tozo ya Kodi ya simu, amesema Kodi ni jambo lamsingi kwa maendeleo ya nchi lakini kodi hiyo inapaswa iinufaishe Zanzibar nasiyo Tanzania bara.
Mohammed Raza ambaye pia ni Mwakilishi wa Jimbo laUzini aliweka wazi kuwa aliyoyasema ni maoni yake binafsi kama Mwananchi nasiyo mawazo ya Mwakilishi wa Uzini.
IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

 
Back
Top Bottom