Zanzibar yatangaza ongezeko la Wagonjwa 29 wa COVID19. Jumla ya visa visiwani humo yafikia 134 (Mei 07, 2020)

Zanzibar yatangaza ongezeko la Wagonjwa 29 wa COVID19. Jumla ya visa visiwani humo yafikia 134 (Mei 07, 2020)

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Wizara ya Afya Zanzibar imetangaza ongezeko la wagonjwa wapya 29 wa #COVID19 na kufanya idadi ya maambukizi visiwani humo kufikia 134. Wagonjwa wote waliotangazwa leo ni Watanzania

Pamoja na ongezeko hilo, Wizara pia imesema wagonjwa wengine watano wamefariki dunia na 11 wamepona na kufanya idadi ya waliopona kufika 16

Waliolazwa katika vituo vya kutolea huduma ni 41 na hali zao ni nzuri. Utaratibu wa kuwatibia nyumbani wagonjwa wenye dalili chache na ambao hawana matatizo mengi ya kiafya unaendelea na sasa wagonjwa 72 wanatibiwa nyumbani

Wizara hiyo imeendelea kuwahimiza wananchi kuvaa barakoa wanapokuwa katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu


E7C911FC-6FA2-4DE0-8D96-E96B1E1AD677.jpeg
 
Hivi kwanini Tanganyika tunakuwa roho mbaya namna hii?! Yaani wakati sisi tumefanikiwa kudhibiti hili gonjwa kwa 100% na hivi sasa hatuna kabisa maambukizi lakini tunashindwa kuwasaidia ndugu zetu Wazanzibar ili na wao wasiwe na maambukizi kama sisi?!

Ama kweli kikulacho kinguoni mwako!

Sema na nyinyi Wazanzibar mmezidi ubishi... yaani ubishi wa CCM na CUF mnataka kuuleta hadi kwenye serious issues!
Ndugu zenu tumewambia muanze kupiga nyungu dozi kutwa mara tatu lakini hamsikii!!

Shauri yenu, wenzenu tunapeta tu, na kwa ushenzi tu hivi sasa ile mimashine yao ya kupimia tushaisokomeza mifenesi na miparachichi... dadeki; sisi hao!! Hapana chezea vijukuu vya Kamanda Kinjekitile Ngwale wewe!!
 
safi sana SMZ endeleeni kutoa hizi update ni muhimu sana kwa wananchi na nchi kwa ujumla ...

bara wao bado ila mtambue tu who watakuja kutoa vyeti kwa nchi zote zilizotoa ushilikiano kipindi cha janga hili na hapo ndio tutatafutana maana hakuna mtalii au msaada utaupata bila ya kuwa na certificate yao.
 
safi sana smz endeleeni kutoa hizi update ni muhimu sana kwa wananchi na nchi kwa ujumla ...

bara wao bado ila mtambue tu who watakuja kutoa vyeti kwa nchi zote zilizotoa ushilikiano kipindi cha janga hili na hapo ndio tutatafutana maana hakuna mtalii au msaada utaupata bila ya kuwa na certificate yao.
Kwa hiyo nchi yenye kesi nyingi ndo itakayopata watalii wengi.
 
Takwimu za maambukizi mapya huku Tanganyika mbona hazitolewi tena?
 
Back
Top Bottom