Zanzibar yenye taswira ya Lee Kuan Yew, ipo tayari chini ya Utashi, maono na Falsafa za Rais Hussein Mwinyi

Zanzibar yenye taswira ya Lee Kuan Yew, ipo tayari chini ya Utashi, maono na Falsafa za Rais Hussein Mwinyi

Deogratias Mutungi

Senior Member
Joined
Oct 1, 2019
Posts
140
Reaction score
181
Salaam Wana JF.
Kama mzalendo wa taifa hili kuna jambo nimeliona la kipekee kutokana na utawala mpya wa rais wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi, Utashi, sera na falsafa zake zinazofanyika kwa sasa bila shaka zinaweza kuivusha Zanzibar katika daraja la uchumi imara na bora kwa Afrika na dunia kwa ujumla, Ukirejea historia ya Lee Kuan Yew miaka ya 1956 wakati anaingia madarakani alikuwa na falsafa, maono na utashi wa kuifanya Singapore kuwa taifa la kipekee lenye nguvu za kiuchumi duniani, wapo waliopinga sera zake lakini badae wakakubaliana na matokeo ya sera na mifumo yake kiutawala.

Ukweli upo wazi kuwa mwanzo wa Dkt. Hussein Mwinyi katika utumishi wake kwa Watu wa Zanzibar ni wa kimapinduzi na wenye fikra za kiuchumi kama alivyokuwa Lee kwa taifa lake la Singapore, tutegemee uchumi imara wa vitu na watu ndani ya watu wa Zanzibar, Mantiki kuu ikiwa ni falsafa za utendaji aliouonyesha hadi sasa, Dhamira ya Mwinyi ni chanya katika utumishi wa watu wa Zanzibar, ni imani ya andiko hili kuwa kwa kipindi cha miaka mitano tutaiona Zanzibar yenye neema na fursa za kiuchumi na hivyo kuwa kivutio cha watu wa bara na duniani kote kuja kuwekeza Zanzibar, Naiona Zanzibar salama mikononi mwa Mwinyi, Kama ilivyokuwa Singapore salama mikononi mwa Lee Kuan Yew.
 
Binafsi sina chama lakini ninae raisi. Hussein Mwinyi ni kiongozi ambae nakubali sana mienendo yake na miamala yake na wafanyakazi wake wa chini.
 
Acheni longongo za madini na mafuta, mwananchi wanahitaji tume huru, sasa hata hamuoni kama ingekuwepo tume huru hamjaingia madarakani kwa kufa mtu furaha yake ingekuwaje na nyinyi mngeliweza kutembea bila ya kuweka bataliani za ulinzi ?

Yaani CCM tungelishinda bila ya mauzauza yaliyojitokeza tungekuwa huru sana ,bungeni wabunge mchanganyiko japo ccm watakuwa wengi harikazalika barani pale pa wawakilishi napo kungekuwa na mchanganyiko wa kahawa na karafuu ,mbona mambo yangekuwa supa ,hakuna senene senene,sijui kwanini CCM hatukujiamini kufanya uchaguzi bila ya mapepe.
 
Eti nawe ni CCM!
Acheni longongo za madini na mafuta, mwananchi wanahitaji tume huru ,sasa hata hamuoni kama ingekuwepo tume huru hamjaingia madarakani kwa kufa mtu furaha yake ingekuwaje na nyinyi mngeliweza kutembea bila ya kuweka bataliani za ulinzi ?

Yaani CCM tungelishinda bila ya mauzauza yaliyojitokeza tungekuwa huru sana ,bungeni wabunge mchanganyiko japo ccm watakuwa wengi harikazalika barani pale pa wawakilishi napo kungekuwa na mchanganyiko wa kahawa na karafuu ,mbona mambo yangekuwa supa ,hakuna senene senene,sijui kwanini CCM hatukujiamini kufanya uchaguzi bila ya mapepe.
 
Mwinyi ameikopi idea ya Maalim Seif ya kuifanya Zanzibar Singapore ile sera ya Uchumi wa bluu ya CUF mwaka 2015.

Tatizo ni chama chake kitambana na vile vile Upande wa Muungano.

Ndio kwanza nasikia leo kala kiapo cha kuwa Waziri wa JMT mbele ya Rais Magufuli.

Zanzibar inabanwa na mfumo wa Muungano
 
Mwinyi ameikopi idea ya Maalim Seif ya kuifanya Zanzibar Singapore ile sera ya Uchumi wa bluu ya CUF mwaka 2015.

Tatizo ni chama chake kitambana na vile vile Upande wa Muungano.

Ndio kwanza nasikia leo kala kiapo cha kuwa Waziri wa JMT mbele ya Rais Magufuli.

Zanzibar inabanwa na mfumo wa Muungano
Kinachonishangaza zaidi ni kuwa kama akileta maendeleo znz inamaana ameleta maendeleo sehemu ya T'nia lakini kwa nn hawataki sehemu yao ya T'nia ipate maendeleo? Lengo la kupinga maendeleo znz ni nini au ndio roho ya mtu mweusi
 
Lee Kuan Yew alikuwa na falsafa ipi na maono gani ambayo yaliifikisha Singapore ilipo sasa?

Amandla...
 
Mwinyi ameikopi idea ya Maalim Seif ya kuifanya Zanzibar Singapore ile sera ya Uchumi wa bluu ya CUF mwaka 2015.

Tatizo ni chama chake kitambana na vile vile Upande wa Muungano.

Ndio kwanza nasikia leo kala kiapo cha kuwa Waziri wa JMT mbele ya Rais Magufuli.

Zanzibar inabanwa na mfumo wa Muungano
Ingekuwa vyema wangeweka wazi njia wanayotarajia kufuata ili kuifikia Singapore au hata Mauritius. Kusema tu bila mipango thabiti hakusaidii kitu.

Amandla...
 
Kipaumbele cha Raisi Lee-Kuan-Yew kilikuwa ni ELIMU, Raisi Mwinyi Kipaumbele chake ni kipi ?
Halafu Lee-Kuan-Yew alikuwa ni msomi mwenye fikra huru, alishirikiana hadi na mabeberu.
Kweli kabisa. Mpaka sasa sijawasikia wakisema kama wana mpango wa kuwekeza kwenye elimu. Nadhani imani ni kuwa wakiwakaribisha watu, watu watakuja na hao ndio wataigeuza Zanzibar kuwa Mauritius au Singapore. Labda wamesema lakini sikuwasikia.

Amandla...
 
Lee Kwan Yew alitiliya mkazo elimu na teknolojia. Muhimu zaidi hakuvumilia ufisadi.
Zanzibar baada ya CAG wao kubainisha wizi mkubwa zilifata ngonjera za Mh Rais na baadaye shughuli kama kawaida.
 
Back
Top Bottom