Sikirimimimasikini
JF-Expert Member
- Dec 27, 2019
- 2,926
- 15,634
Zelensky na Pro-NATO akili zao wanazijua wao wenyewe aisee...Eti walisherehekea kupewa kifuta jasho cha kilomita za mraba 6,000 sawa na asilimia 4.8 tu, toka kwa kilomita za mraba 125,000 zilizokuwa zimekaliwa na Urusi (kwa maneno mengine Urusi imebakia na asilimia 95.2 ya eneo hilo).
Sasa kichekesho zaidi ni kuwa walikuwa wakijifariji kuwa eti walitumia siku sita tu kurejesha kilomita za mraba 3,000 (katika hizo 6,000 walizopewa). Kwa akili zao finyu wakahisi huo ni muda mfupi sana wametumia!
Wakasahau kuwa wanadaiwa kurejesha eneo lote (kilomita za mraba 125,000! Kama tukijaalia Urusi ingeamua kufanya vile vile, kuwapa maeneo pasi na kupigana vita, basi ingewachukua Ukraine jumla ya siku 250 (zaidi ya miezi 8) kurejesha kilomita za mraba zote 125,000 zilizokaliwa na Urusi! (nimeambatanisha hesabu yake hapo chini)
Bahati mbaya sasa Urusi inayachukua rasmi maeneo hayo kupitia kura za wananchi wa maeneo husika (referendums). Maeneo hayo yanakuwa rasmi ardhi ya Urusi, na Urusi imeapa kuyalinda hata kwa silaha za nyuklia. Pia imetangaza kuwa kidudu mtu atakayejaribu kuyashambulia maeneo hayo, atakuwa kashambulia ardhi ya Urusi...maangamivu yatamuhusu.
Hesabu hazidanganyi!
Sasa kichekesho zaidi ni kuwa walikuwa wakijifariji kuwa eti walitumia siku sita tu kurejesha kilomita za mraba 3,000 (katika hizo 6,000 walizopewa). Kwa akili zao finyu wakahisi huo ni muda mfupi sana wametumia!
Wakasahau kuwa wanadaiwa kurejesha eneo lote (kilomita za mraba 125,000! Kama tukijaalia Urusi ingeamua kufanya vile vile, kuwapa maeneo pasi na kupigana vita, basi ingewachukua Ukraine jumla ya siku 250 (zaidi ya miezi 8) kurejesha kilomita za mraba zote 125,000 zilizokaliwa na Urusi! (nimeambatanisha hesabu yake hapo chini)
Bahati mbaya sasa Urusi inayachukua rasmi maeneo hayo kupitia kura za wananchi wa maeneo husika (referendums). Maeneo hayo yanakuwa rasmi ardhi ya Urusi, na Urusi imeapa kuyalinda hata kwa silaha za nyuklia. Pia imetangaza kuwa kidudu mtu atakayejaribu kuyashambulia maeneo hayo, atakuwa kashambulia ardhi ya Urusi...maangamivu yatamuhusu.
Hesabu hazidanganyi!