Zeyana Seif wa BBC afariki


Wa kwanza kulia
Kwa mujibu wa BBC swahili web site. Kifo chake kimetokea ghafla siku ya Jumatatu.

Zeyana alikuwa mwanamke wa kwanza kabisa kusoma habari kwenye redio, katika BBC.

Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili, Solomon Mugera kwa niaba ya shirika la Utangazaji la Uingereza BBC ametoa pole kwa ndugu na jamaa za marehemu.

Akimzungumzia marehemu, Bw. Solomon amesema alikuwa mcheshi na mchangamfu, na daima alikuwa tarari kutoa msaada wowote katika fani ya utangazaji.

Alistaafu mwaka 2005.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema.
 

Attachments

  • 200706221150553.jpg
    21.1 KB · Views: 230
Sikuona hii thread befor.......RIP
 
Pole kwa ndugu wote wa mama yetu huyu...R.I.P Zeyana Seif
 
Sisi ni wa M/Mungu na kwake tutarejea.....Wadau tuangalie madhambi yetu
 
Zeyana Seif azikwa London

Mtangazaji wa siku nyingi wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Bi Zeyana Seif amezikwa nchini Uingereza.Bi Zeyana aliaga dunia tarehe 29 Disemba 2008 mjini London.
Baada ya kuswaliwa katika msikiti mkuu ujulikanao kama East London Mosque huko Whitechapel, mwili wa Bi Zeyana ulipelekwa katika makaburi ya Gardens of Peace, Essex kwa mazishi - Jumamosi ya tarehe tatu 2009.

Miongoni mwa watu waliofika msikitini kumswalia Bi Zeyana ni ndugu, jamaa na marafiki kutoka sehemu mbali mbali duniani akiwemo balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Bi Mwanaidi Sinare Maajar.

Bi Zeyana alianza kazi ya utangazaji katika Idhaa ya Kiswahili ya BBC London mnamo mwaka 1965 na kustaafu mwaka 2005.
BBCSwahili.com | Habari | Zeyana Seif azikwa London
 
mungu amlaze pema peponi

sisi tulimpenda ila bwana alimpenda zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…