Ziara ya Pelosi katika sehemu ya Taiwan yaleta hasara kwa pande zote

Ziara ya Pelosi katika sehemu ya Taiwan yaleta hasara kwa pande zote

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
VCG111394685555.jpg


Spika wa Baraza la Wawakilishi la Bunge la Marekani Nancy Pelosi hivi karibuni alifanya ziara Taiwan, China, na kuongeza hali ya wasiwasi ya kikanda na ya kimataifa. Kitendo hiki cha kisiasa kinacholeta hasara kwa pande zote kimeonyesha kuwa, mfumo wa kisiasa wa Marekani ni kama mgonjwa.

Kwanza kabisa, ziara ya Pelosi katika sehemu ya Taiwan imeiumiza China. Suala la Taiwan ni moja ya maslahi makuu ya China. Nchi 181 duniani zimeanzisha uhusiano wa kidiplomasia na China kwa kufuata kanuni ya kuwepo kwa China moja, ambayo inaonyesha kuwa kanuni hiyo ni makubaliano ya pamoja ya jumuiya ya kimataifa. Akiwa kiongozi namba tatu wa serikali ya Marekani, Pelosi amekiuka kanuni hiyo kwa kutembelea Taiwan bila ya kujali kupingwa vikali na China. Kitendo chake kimeharibu mamlaka na ukamilifu wa ardhi ya China, na kuumiza uhusiano wa China na Marekani na hisia za watu wa China.

Ziara hiyo pia imedhuru zaidi maslahi ya Taiwan. Baadhi ya watumiaji wa mtandao wa Taiwan wamesema kuwa, Pelosi amecheza na moto bila kujali usalama wa watu milioni 23 wa Taiwan. Taiwan ni sehemu isiyotengeka ya China, lakini sasa Marekani inaitumia kama silaha ya kuzuia maendeleo ya China. Ziara ya Pelosi imezidisha mvutano kati ya pande hizo mbili katika suala la Taiwan, na kuongeza uwezekano wa kutokea kwa migogoro katika mlangobahari wa Taiwan.

Ziara ya Pelosi katika sehemu ya Taiwan pia inakwenda kinyume na maslahi ya Marekani. Hivi sasa Marekani inakabiliwa na mfumuko wa bei uliokuwa mbaya zaidi tangu mingo kadhaa iliyopita, na mzozo wa Russia na Ukraine. Licha ya hitaji la kushirikiana na China ili kukabiliana na changamoto hizo, kuikasirisha China na kuzusha migogoro mipya bila shaka hakulingani maslahi ya Marekani.

Tukitafuta manufaa ya zaira hiyo, labda ni kwake yeye tu binafsi. Lengo la wazi la ziara ya Pelosi katika sehemu ya Taiwan ni kuharibu maslahi makuu ya China, ili kuongeza uwekezano wa ushindi kwa Chama chake cha Kidemokrasia kwenye uchaguzi utakaofanyika miezi mitatu ijayo. Lakini ukweli ni kwamba, Pelosi anazingatia zaidi maslahi yake binafsi na ya kisiasa. Licha ya hayo, mbunge wa Marekani Marjorie Green alidokeza kuwa, safari ya Pelosi katika Taiwan haswa ni kwa ajili ya kumsaidia mume wake kufanya uwekezaji katika sekta ya Chips. Hata hivyo, mchezo huu wa kisiasa ambao kwa hakika utaleta hasara kwa pande zote zinazohusika hatimaye umefanyika, hali ambayo inathibitisha kuwa mfumo wa kisiasa wa Marekani ni kama mgonjwa.

Kabla ya safari ya Pelosi, mkurugenzi wa Shirika la Ujasusi la Marekani, Mwenyekiti wa Mkutano wa Viongozi Waandamizi, na timu nzima ya usalama wa taifa nchini Marekani walitoa pingamizi kwa pamoja. Ingawa Rais Joe Biden wa Marekani hakutoa tamko la wazi, lakini alinukuu maoni ya jeshi, kwamba Pelosi kutembelea Taiwan si wazo nzuri. Jambo la kushangaza ni kwamba kutokana na mfumo wa kisiasa wa Marekani, hakuna nguvu yoyote iliyomzuia Pelosi.

Kama kiongozi wa ustaarabu wa kisiasa wa Magharibi, Marekani inajivunia sana na mfumo wake wa kisiasa. Lakini katika miaka ya hivi karibuni, kutoka kwa ghasia za Capitol Hill, hadi kukwama kwa sera ya kudhibiti bunduki, na kisha ziara hiyo ya Pelosi kwenda Taiwan, mambo hayo yote yanaonesha kuwa mfumo wa kisiasa wa Marekani umekumbwa na shida na haufanyi kazi vizuri, na sasa ni wakati wa kuutiba kama mgonjwa.
 
View attachment 2313746

Spika wa Baraza la Wawakilishi la Bunge la Marekani Nancy Pelosi hivi karibuni alifanya ziara Taiwan, China, na kuongeza hali ya wasiwasi ya kikanda na ya kimataifa. Kitendo hiki cha kisiasa kinacholeta hasara kwa pande zote kimeonyesha kuwa, mfumo wa kisiasa wa Marekani ni kama mgonjwa.---
Taiwan ni taifa huru, kinachomsumbua China ni tamaa za mali za watu. Afadhali ukomunisti ulikufa kwani ni mfumo uliozalisha viongozi wabovu kabisa.
 
Wakuu dunia inayotawaliwa na USA ni bora mara trillion kuliko ile itakayotawaliwa na China au Russia.
Wakati wa ukomunisti wa Kisoviet tuliona kila kulikokuwa na siasa za Kisoshalist/Kijamaa mambo yalienda hovyo na sasa nchi zote hizo ama wanafuata ubepari au wako liberal

Hata ukomunist wa sasa wa China nifake na kwa sasa China ni nchi ya Kibepari kwa 100%
 
View attachment 2313746

Spika wa Baraza la Wawakilishi la Bunge la Marekani Nancy Pelosi hivi karibuni alifanya ziara Taiwan, China, na kuongeza hali ya wasiwasi ya kikanda na ya kimataifa. Kitendo hiki cha kisiasa kinacholeta hasara kwa pande zote kimeonyesha kuwa, mfumo wa kisiasa wa Marekani ni kama mgonjwa...
Mbona hujaongelea mfumo wa siasa wa ccm unaongelea wa USA. Hata hivyo inamaana una akili kuliko huyo bibi Hadi useme mfumo wao ni mbaya? Wewe mtanzania wa tandahimba kweli unaweza kosoa mfumo wa USA kua ni mbaya
 
China kasema mazoezi no siku 3 , wameizunguka Taiwan, na hakuna ndege wala meli kutoka au kuingia.
 
Mkuu,ukisema hivyo,hata wao watakwambia Donbass hawaitaki Ukraine..,[emoji848]
Mmepiga kura huko Donbas ? ila Taiwan inajitegemea tangu kitambo , made in Taiwan zipo Afrika kitambi hata kabla ya ujio wa wachina
 
Kama ambavyo Donensk na Luhansk haiwataki Ukraine na wanataka kuwa mataifa huru!
Taiwan inajitegemea kila kitu hadi mfumo wa siasa ni tofauti na China , Donbas na Luhansk ni majimbo ya Ukraine na wachache ndo wanaunga mkono Urusi
 
Taiwan inajitegemea kila kitu hadi mfumo wa siasa ni tofauti na China , Donbas na Luhansk ni majimbo ya Ukraine na wachache ndo wanaunga mkono Urusi
Unajua wamekufa watu wengi huko Donbas kisa wanataka kujitenga na Ukraine na kuwa Mataifa huru yaani Luhansk na Donensk republic!
Ukraine Ilikuwa sehemu ya Urusi,walipiga kura ya kujiondoa kwenye USSR,kwanini Donbas wasipewe haki hiyo ya kufanyika mchakato wa kura na wengi wape badala yake watu wamekuwa wakiuwawa na US kapiga kimya Kwa mingi tu!
 
Back
Top Bottom