Immortal Consulting Co
Member
- Jun 15, 2021
- 6
- 14
Katika ulimwengu wa biashara, ni kazi ngumu kuifanya biashara idumu na kukua kuliko kuianzisha hata kama ulianzisha kwa mabilioni ya pesa. Biashara nyingi huanzishwa kila siku na biashara nyingi zinakufa kila siku kwa sababu mbalimbali ambazo tutazijali siku nyingine. Katika makala ya leo, nitazjadili dalili saba ambazo zinaashiria hatari ya kifo kwa biashara husika. Safiri nami katika uzi huu tujali pamoja.
I: Kukimbiwa na wafanyakazi
I: Kukimbiwa na wafanyakazi
Jambo la kuondoka wafanyakazi ni la kawaida katika biashara yoyote, lakini kama mwendendo huo umekuwa mkubwa basi jua kuna jambo linalohatarisha uhai wa biashara. Maana inawezekana kabisa wafanyakazi hawaoni future yoyote katika ofisi yako na morali wao wa kazi umekwisha kabisa. Chukua hatua haraka.
II: Kupungua kwa pesa iliyo katika mzunguko
Hii ni dalili mbaya sana, maana itakufanya ushindwe hata kilipia gharama mbalimbali za uendeshaji wa biashara. Biashara iliyochangamka maana yake ni pesa inaingia na kutoka kwa kasi. Pesa ikiingia na kuchelewa kutoka ni tatizo na pesa ikitoka na kuchelewa kuingia ni tatizo kubwa zaidi. Ikitokea pesa zinapungua katika mzunguko wa biashara yako, kaa chini jiulize tatizo ni nini? Inawezekana bei zako ni kubwa sana hivyo hupati wateja au inawezekana bei ni ndogo sana inakula mtaji. Pengine kuna shida kwenye marketing au kuna wezi ndani ya ofisi na wakati mwingine ni matumizi mabaya ya pesa ndani ya ofisi. Hakikisha unajua chanzo ni nini na tafuta suluhu ya tatizo hilo.
III: Matatizo ya dharula yasiyoisha kwenye biashara
Ni kawaida kwa biashara yoyote kuwa na matatizo ya hapa na pale, lakini hapa tunazungumzia matatizo ambayo yamefugwa au yameachwa kwa muda mrefu mpaka imefikia mwisho inabidi utatuzi wake uwe ni wa dhalula kama kuzima moto. Kukiwa na matukio hayo ya kujirudia sana, ni ishara kwamba biashara inapambana (struggling) kujiendesha, na inaweza kufa muda wowote.
IV: Kupotea kwa wateja
Huduma mbaya katika biashara hukimbiza wateja, na biashara bila wateja sio biashara tena, ni hobby. Katika biashara ogopa sana kumpoteza mteja, katika sanaa ya biashara mteja ndio boss mkuu. Biashara inayopoteza wateja ni biashara inayojihukumu hukumu ya kifo. Jenga utamaduni wa kujua mrejesho wa wateja wanasemaje kuhusu huduma na bidhaa zenu. Maana itakugharimu sana kuwarudisha wateja walioondoka.
V: Kupoteza hamu/shauku (passion) na biashara yako
Dunia ina mengi hususani katika kada ya biashara. Yawezekana likatokea jambo litakalokufanya uchukie au upoteze hamu ya kufanya biashara unayoifanya. Jambo ambalo kila ukiiona biashara yako inakukumbusha uchungu wa jambo hilo. Ikifikia hapo biashara hiyo iko mashakani sana, itahitajika cancelling kubwa kwa mtu huyo ili kuirudisha hamu yake ya kufanya biashara hiyo.
VI: Kufanya makosa ya kujirudia
Kila mtu anafanya makosa, hakuna aliye mkamilifu kwenye biashara. Kama si leo basi kesho utafanya makosa fulani. Lakini kwa biashara ambayo ina makosa yanayojirudia rudia ni dalili ya kuonyesha kwamba biashara hiyo ina matatizo ya msingi ambayo yasipotatuliwa yanahatarisha uhai wa biashara. Jambo la kwanza ni kujitahidi kuzuia makosa ya kizembe, na endapo kosa lolote likitokea kuwe na mifumo ya kutambua makosa haraka na kuyapatia ufumbuzi kabla athari zake hazijasambaa sana.
VII: Biashara inayosahaulika au isiyozungumzwa na watu
Biashara isiyozungumzwa ni biashara mfu ama biashara bubu. Ndio maana makampuni mbalimbali yako tayari kuwekeza mabilion ya pesa kwenye matangazo ili biashara zao zizungumzwe na watu. Biashara isipozungumzwa inasahaulika na matokeo yake haraka sana utayaona kwenye mauzo. Kwa hiyo matangazo hayana mwisho, yanaendelea katika kipindi chote cha uhai wa biashara.
Karibu tujadili pamoja, karibu kwa maswali, maoni na ushauri ili tuelimike kwa pamoja. mimi ni mchokoza maada, nategema kupata maoni zaidi kutoka kwenu. Katika makala ijayo tutazungumzia hatua tano za ukuaji wa biashara.
......... Karibuni sana! ............
II: Kupungua kwa pesa iliyo katika mzunguko
Hii ni dalili mbaya sana, maana itakufanya ushindwe hata kilipia gharama mbalimbali za uendeshaji wa biashara. Biashara iliyochangamka maana yake ni pesa inaingia na kutoka kwa kasi. Pesa ikiingia na kuchelewa kutoka ni tatizo na pesa ikitoka na kuchelewa kuingia ni tatizo kubwa zaidi. Ikitokea pesa zinapungua katika mzunguko wa biashara yako, kaa chini jiulize tatizo ni nini? Inawezekana bei zako ni kubwa sana hivyo hupati wateja au inawezekana bei ni ndogo sana inakula mtaji. Pengine kuna shida kwenye marketing au kuna wezi ndani ya ofisi na wakati mwingine ni matumizi mabaya ya pesa ndani ya ofisi. Hakikisha unajua chanzo ni nini na tafuta suluhu ya tatizo hilo.
III: Matatizo ya dharula yasiyoisha kwenye biashara
Ni kawaida kwa biashara yoyote kuwa na matatizo ya hapa na pale, lakini hapa tunazungumzia matatizo ambayo yamefugwa au yameachwa kwa muda mrefu mpaka imefikia mwisho inabidi utatuzi wake uwe ni wa dhalula kama kuzima moto. Kukiwa na matukio hayo ya kujirudia sana, ni ishara kwamba biashara inapambana (struggling) kujiendesha, na inaweza kufa muda wowote.
IV: Kupotea kwa wateja
Huduma mbaya katika biashara hukimbiza wateja, na biashara bila wateja sio biashara tena, ni hobby. Katika biashara ogopa sana kumpoteza mteja, katika sanaa ya biashara mteja ndio boss mkuu. Biashara inayopoteza wateja ni biashara inayojihukumu hukumu ya kifo. Jenga utamaduni wa kujua mrejesho wa wateja wanasemaje kuhusu huduma na bidhaa zenu. Maana itakugharimu sana kuwarudisha wateja walioondoka.
V: Kupoteza hamu/shauku (passion) na biashara yako
Dunia ina mengi hususani katika kada ya biashara. Yawezekana likatokea jambo litakalokufanya uchukie au upoteze hamu ya kufanya biashara unayoifanya. Jambo ambalo kila ukiiona biashara yako inakukumbusha uchungu wa jambo hilo. Ikifikia hapo biashara hiyo iko mashakani sana, itahitajika cancelling kubwa kwa mtu huyo ili kuirudisha hamu yake ya kufanya biashara hiyo.
VI: Kufanya makosa ya kujirudia
Kila mtu anafanya makosa, hakuna aliye mkamilifu kwenye biashara. Kama si leo basi kesho utafanya makosa fulani. Lakini kwa biashara ambayo ina makosa yanayojirudia rudia ni dalili ya kuonyesha kwamba biashara hiyo ina matatizo ya msingi ambayo yasipotatuliwa yanahatarisha uhai wa biashara. Jambo la kwanza ni kujitahidi kuzuia makosa ya kizembe, na endapo kosa lolote likitokea kuwe na mifumo ya kutambua makosa haraka na kuyapatia ufumbuzi kabla athari zake hazijasambaa sana.
VII: Biashara inayosahaulika au isiyozungumzwa na watu
Biashara isiyozungumzwa ni biashara mfu ama biashara bubu. Ndio maana makampuni mbalimbali yako tayari kuwekeza mabilion ya pesa kwenye matangazo ili biashara zao zizungumzwe na watu. Biashara isipozungumzwa inasahaulika na matokeo yake haraka sana utayaona kwenye mauzo. Kwa hiyo matangazo hayana mwisho, yanaendelea katika kipindi chote cha uhai wa biashara.
Karibu tujadili pamoja, karibu kwa maswali, maoni na ushauri ili tuelimike kwa pamoja. mimi ni mchokoza maada, nategema kupata maoni zaidi kutoka kwenu. Katika makala ijayo tutazungumzia hatua tano za ukuaji wa biashara.
......... Karibuni sana! ............