John Magongwe
Member
- Jan 4, 2024
- 71
- 119
Zijue Faida za Kuwahi Kwenye Ibada
Kutofika Kwenye Ibada kwa Wakati
Imekuwa ni desturi au tabia ya watu wengi kutokufika sehemu fulani kwa wakati. Hili tunaliona katika maisha yetu ya kila siku. Wapo ambao kila siku ni kuchelewa sehemu zao za kazi.
Wengine kuchelewa nyumba za ibada na sehemu nyingine zilizoamriwa kukutana. Watu wanawekeana mihadi wakutane muda fulani, lakini ni wachache ambao wanaweza kutii na kuwa na nidhamu ya muda.
Mara nyingi pale unapokuwa umechelewa sehemu, ukafika na kukuta wenzako wamewahi, unajihisi ni kama fedheha, na unaweza kujiambia kesho nitawahi, kuchelewa mwisho leo. Lakini unakuta wimbo wa kuchelewa unabaki ni ule ule kila siku, hubadiliki.
Si rahisi kufika kwa wakati siku zote, kwani huenda tukahitaji kukabiliana na matatizo kama vile kusafiri mbali, msongamano mkubwa wa magari, na ratiba zenye shughuli nyingi. Hata hivyo, kufika kwa wakati ni jambo la muhimu, kwa sababu mambo lazima yaende kwa ratiba, ili muda ya kufanya mambo mengine usigongane.
Mtu anayefika kazini kwa wakati anaonwa kuwa mtu mwenye kutegemewa na mwenye bidii. Kwa upande mwingine, mtu ambaye anafika akiwa amechelewa anaweza kuvuruga kazi za wengine na kupunguza ubora wa kazi au huduma.
Mwanafunzi anayechelewa anaweza kukosa vipindi fulani vya masomo na hilo linaweza kumzuia kufanya vizuri shuleni. Vile vile, kuchelewa kufika kumwona daktari kunaweza kufanya upokee matibabu yasiyofaa.
Jambo la kushangaza ni kuwa watu wengine hawaoni kufika kwa wakati kuwa ni jambo la maana sana. Katika mazingira hayo, ni rahisi sana kuwa na mazoea ya kuchelewa. Kwa hali hiyo, ni muhimu kusitawisha tamaa ya kufika kwa wakati.
Tukithamini umuhimu wa kufika kwa wakati, bila shaka hilo litatusaidia kutochelewa. Tuna sababu gani za kufika kwa wakati? Tunaweza kufanya nini ili tufike kwa wakati? Na ni faida gani tunazoweza kupata tukifika kwa wakati?
YEHOVA NI MUNGU ANAYEFUATA WAKATI.
Sababu kuu zaidi ambayo inatufanya tuwe na mazoea ya kuwahi kwenye ibada ni kwamba tunataka tumuige Mungu tunayemuabudu.
Katika Waefeso 5:1, Yehova anaweka mifano bora kabisa katika kufuata wakati. Hachelewi kamwe. Anafuata kikamili ratiba zake ili atimize makusudi yake.
1. Yehova alipoamua kuuharibu ulimwengu usiomwogopa Mungu, alimwambia Noa hivi: “Jifanyie safina ya mti wenye utomvu.” Mwisho ulipokuwa ukikaribia, Yehova alimwambia Noa aingie ndani ya safina na kumweleza hivi: “Baada ya siku 7 nitanyesha mvua duniani, siku 40 mchana na usiku; nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kitu kilichoko ambacho nimekifanya”. Kisha, kwa wakati unaofaa kabisa, “siku saba baadaye, maji ya gharika yakaja juu ya dunia” (Mwanzo 6:14; 7:4, 10).
Hebu fikiria jambo ambalo huenda lingetokea ikiwa Noa na familia yake wangechelewa kuingia ndani ya safina. Walihitaji kufuata wakati, kama Mungu waliyemwabudu alivyofuata wakati.
2. Miaka 450 hivi baada ya gharika, Yehova alimwambia mzee wa ukoo, Abrahamu, kwamba angepata mwana ambaye kupitia kwake uzao ulioahidiwa ungetokea. Katika Mwanzo 17:15-17, Mungu alisema kwamba Isaka angezaliwa “wakati huu uliowekwa mwaka ujao.” Je, ndivyo ilivyotokea? Maandiko yanatuambia hivi: “Sara akapata mimba, kisha akamzalia Abrahamu mwana katika umri wake wa uzee, kwa wakati uliowekwa, ambao Mungu alikuwa amemwambia” (Mwanzo 17:21; 21:2).
3. Biblia ina mifano mingi inayoonesha kwamba Mungu anafuata wakati (Yer 25:11-13; Dan 4:23-25; 9:25). Biblia inatuambia tuendelee kungojea siku ya Yehova inayokuja ya hukumu. Hata ingawa wanadamu wanaona kwamba ‘inakawia,’ tunahakikishiwa kwamba ‘haitachelewa’ (Hab 2:3).
4. Wanaume wote Waisraeli walipaswa kufika kwa wakati mahali palipochaguliwa kwa ajili ya “sherehe za majira za Yehova” (Law 23:2-7). Pia, Mungu aliweka nyakati ambazo dhabihu fulani zilipaswa kutolewa (Kut 29:38-39; Law 23:37). Je, hilo halionyeshi kwamba Mungu anataka watumishi wake wafuate wakati katika ibada yao?
5. Katika karne ya kwanza, mtume Paulo aliwapa Wakorintho maagizo kuhusu jinsi mikutano ya Kikristo inavyopaswa kuongozwa. Aliwahimiza hivi: “Mambo yote na yatendeke kwa adabu na kwa mpango” (1Kor 14:40). Kwa hiyo, mikutano ya wakristo ya ibada ilipaswa kuanza kwa wakati uliowekwa.
6. Maoni ya Yehova kuhusu kufuata wakati, hayajabadilika (Mal 3:6).
Tufanye nini ili tufike kwa wakati kwenye ibada
Tuangalie mifano michache.
Watu wengine wanaona kwamba kufanya matayarisho mapema kunasaidia sana (Meth 21:5). Kwa mfano, ikiwa tunahitaji kusafiri umbali fulani ili tufike kwa wakati fulani uliowekwa, je, si ni jambo la hekima kutenga wakati wa kutosha, kusafiri na kufika huko kwa wakati kamili?
Ni jambo la busara kuhakikisha kwamba tuna dakika za ziada ili tusichelewe, hata tukipatwa na “tukio lisilotazamiwa” njiani” (Mhu 9:11). Jambo ambalo linaweza kumsaidia mtu yeyote afike kwa wakati ni kujua vizuri muda wa kusafiri, ambao anahitaji,
Watu wengine wanahitaji kufanya mipango inayofaa ili kuondoka kazini mapema vya kutosha, na hivyo kufika kwenye mikutano ya Kikristo kwa wakati mzuri.
Ikiwa tuna watoto wachanga, ni vigumu zaidi kufika kwa wakati kwenye mikutano. Kwa kawaida, mama ndiye anayeachiwa jukumu la kuwatayarisha watoto, lakini washiriki wengine wa familia wanapaswa kumsaidia, ili wote waondoke kwa wakati kwenda kenye ibada.
Familia iweke muda wa kuondoka nyumbani, ili waondoke kwa wakati na kufika kwa wakati.
Zijue faida za kufika kwa wakati kwenye Ibada
1. Kutafakari kuhusu baraka ambazo tunapata tunapofika kwenye ibada ya Kikristo kwa wakati kunaweza kuimarisha tamaa na azimio letu la kufanya yote tunayoweza ili tusichelewe.
2. Kubadilishana uzoefu na waumini wengine
Mtu mmoja mwenye mazoea ya kufika kwenye ibada na mikutano kwa wakati, anasema hivi: “Ninachofurahia kuhusu kufika mapema ni kwamba ninapata nafasi ya kuwasalimu ndugu na dada, kuongea nao, na kuwafahamu vizuri zaidi”. Tunapofika mapema kwenye Jumba la Ufalme, tunaweza kufaidika kwa kusikia kuhusu uvumilivu na utumishi wa uaminifu wa wengine ambao wamehudhuria. Tunapohudhuria mikutano kwa wakati na kuzungumza nao mambo yenye kujenga, tunaweza kuwatia moyo ndugu na dada zetu na ‘kuwachochea katika upendo na matendo mazuri’ (Ebr. 10:24-25).
3. Kushiriki kwenye nyimbo na sala za kufungua ibada
Wimbo na sala ya kufungua ibada ni sehemu ya maana sana ya ibada (Zab 149:1). Nyimbo zinamsifu Yehova, na kutukumbusha sifa ambazo tunapaswa kusitawisha, na nyimbo zinatutia moyo kushiriki kwa shangwe katika huduma.
Namna gani sala ya kufungua? Katika nyakati za kale, Yehova aliliita hekalu ‘nyumba yake ya sala’ (Isa 56:7). Leo, tunakusanyika ili kusali kwa Mungu katika ibada zetu. Sala ya kufungua inamwomba Yehova, atuongoze na kutupatia roho takatifu. Tunapaswa kuazimia kufika kwenye ibada zetu kwa wakati, ili tushiriki wimbo na sala ya kufungua ibada.
4. Hakuna anayeimba na kumsifu Mungu, na kuomba kwa niaba ya muumini mwingine. Hivyo, hakuna anayepokea thawabu kutoka kwa Mungu, kwa kuimba na kuomba, kwa niaba ya muumini mwingine. Thawabu kutoka kwa Mungu ni ya muumini binafsi; hivyo, ni muhimu kuwahi kwenye ibada ili kupokea thawabu hizo.
5. Kujiandaa kiakili, mawazo na kiroho, tayari kwa kushiriki kwenye ibada
Inatayarisha akili na mioyo yetu kupokea habari ambazo zitazungumziwa.
6. Kuwahi kwenye sehemu ya ibada kabla ya wakati, NI USHINDI WA KWANZA, na kuchelewa kufika ni dalili ya kupoteza ushindi wako mapema kwenye ibada. Kuchelewa ni fedheha ambayo inakumaliza nguvu ya kiroho ya kwenda kufanya mambo makubwa.
Tumeona faida zinazopatikana kwa kuwahi kufika kwenye ibada. Hivyo, usikose kupata faida hizo, kutokana tu na kuchelewa kufika kwenye ibada.
Tumeona pia kuwa Mungu mwenyewe anafanya mambo kwa kufuata muda alioweka. Je iweje sisi, tunakwenda kwenye ibada ya Mungu tukiwa tumechelewa. Tujitahidi kusitawisha mazoea ya kufuata muda, katika kwenda kwenye ibada ya Mungu, ili tufike kwa wakati.
Kutofika Kwenye Ibada kwa Wakati
Imekuwa ni desturi au tabia ya watu wengi kutokufika sehemu fulani kwa wakati. Hili tunaliona katika maisha yetu ya kila siku. Wapo ambao kila siku ni kuchelewa sehemu zao za kazi.
Wengine kuchelewa nyumba za ibada na sehemu nyingine zilizoamriwa kukutana. Watu wanawekeana mihadi wakutane muda fulani, lakini ni wachache ambao wanaweza kutii na kuwa na nidhamu ya muda.
Mara nyingi pale unapokuwa umechelewa sehemu, ukafika na kukuta wenzako wamewahi, unajihisi ni kama fedheha, na unaweza kujiambia kesho nitawahi, kuchelewa mwisho leo. Lakini unakuta wimbo wa kuchelewa unabaki ni ule ule kila siku, hubadiliki.
Si rahisi kufika kwa wakati siku zote, kwani huenda tukahitaji kukabiliana na matatizo kama vile kusafiri mbali, msongamano mkubwa wa magari, na ratiba zenye shughuli nyingi. Hata hivyo, kufika kwa wakati ni jambo la muhimu, kwa sababu mambo lazima yaende kwa ratiba, ili muda ya kufanya mambo mengine usigongane.
Mtu anayefika kazini kwa wakati anaonwa kuwa mtu mwenye kutegemewa na mwenye bidii. Kwa upande mwingine, mtu ambaye anafika akiwa amechelewa anaweza kuvuruga kazi za wengine na kupunguza ubora wa kazi au huduma.
Mwanafunzi anayechelewa anaweza kukosa vipindi fulani vya masomo na hilo linaweza kumzuia kufanya vizuri shuleni. Vile vile, kuchelewa kufika kumwona daktari kunaweza kufanya upokee matibabu yasiyofaa.
Jambo la kushangaza ni kuwa watu wengine hawaoni kufika kwa wakati kuwa ni jambo la maana sana. Katika mazingira hayo, ni rahisi sana kuwa na mazoea ya kuchelewa. Kwa hali hiyo, ni muhimu kusitawisha tamaa ya kufika kwa wakati.
Tukithamini umuhimu wa kufika kwa wakati, bila shaka hilo litatusaidia kutochelewa. Tuna sababu gani za kufika kwa wakati? Tunaweza kufanya nini ili tufike kwa wakati? Na ni faida gani tunazoweza kupata tukifika kwa wakati?
YEHOVA NI MUNGU ANAYEFUATA WAKATI.
Sababu kuu zaidi ambayo inatufanya tuwe na mazoea ya kuwahi kwenye ibada ni kwamba tunataka tumuige Mungu tunayemuabudu.
Katika Waefeso 5:1, Yehova anaweka mifano bora kabisa katika kufuata wakati. Hachelewi kamwe. Anafuata kikamili ratiba zake ili atimize makusudi yake.
1. Yehova alipoamua kuuharibu ulimwengu usiomwogopa Mungu, alimwambia Noa hivi: “Jifanyie safina ya mti wenye utomvu.” Mwisho ulipokuwa ukikaribia, Yehova alimwambia Noa aingie ndani ya safina na kumweleza hivi: “Baada ya siku 7 nitanyesha mvua duniani, siku 40 mchana na usiku; nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kitu kilichoko ambacho nimekifanya”. Kisha, kwa wakati unaofaa kabisa, “siku saba baadaye, maji ya gharika yakaja juu ya dunia” (Mwanzo 6:14; 7:4, 10).
Hebu fikiria jambo ambalo huenda lingetokea ikiwa Noa na familia yake wangechelewa kuingia ndani ya safina. Walihitaji kufuata wakati, kama Mungu waliyemwabudu alivyofuata wakati.
2. Miaka 450 hivi baada ya gharika, Yehova alimwambia mzee wa ukoo, Abrahamu, kwamba angepata mwana ambaye kupitia kwake uzao ulioahidiwa ungetokea. Katika Mwanzo 17:15-17, Mungu alisema kwamba Isaka angezaliwa “wakati huu uliowekwa mwaka ujao.” Je, ndivyo ilivyotokea? Maandiko yanatuambia hivi: “Sara akapata mimba, kisha akamzalia Abrahamu mwana katika umri wake wa uzee, kwa wakati uliowekwa, ambao Mungu alikuwa amemwambia” (Mwanzo 17:21; 21:2).
3. Biblia ina mifano mingi inayoonesha kwamba Mungu anafuata wakati (Yer 25:11-13; Dan 4:23-25; 9:25). Biblia inatuambia tuendelee kungojea siku ya Yehova inayokuja ya hukumu. Hata ingawa wanadamu wanaona kwamba ‘inakawia,’ tunahakikishiwa kwamba ‘haitachelewa’ (Hab 2:3).
4. Wanaume wote Waisraeli walipaswa kufika kwa wakati mahali palipochaguliwa kwa ajili ya “sherehe za majira za Yehova” (Law 23:2-7). Pia, Mungu aliweka nyakati ambazo dhabihu fulani zilipaswa kutolewa (Kut 29:38-39; Law 23:37). Je, hilo halionyeshi kwamba Mungu anataka watumishi wake wafuate wakati katika ibada yao?
5. Katika karne ya kwanza, mtume Paulo aliwapa Wakorintho maagizo kuhusu jinsi mikutano ya Kikristo inavyopaswa kuongozwa. Aliwahimiza hivi: “Mambo yote na yatendeke kwa adabu na kwa mpango” (1Kor 14:40). Kwa hiyo, mikutano ya wakristo ya ibada ilipaswa kuanza kwa wakati uliowekwa.
6. Maoni ya Yehova kuhusu kufuata wakati, hayajabadilika (Mal 3:6).
Tufanye nini ili tufike kwa wakati kwenye ibada
Tuangalie mifano michache.
Watu wengine wanaona kwamba kufanya matayarisho mapema kunasaidia sana (Meth 21:5). Kwa mfano, ikiwa tunahitaji kusafiri umbali fulani ili tufike kwa wakati fulani uliowekwa, je, si ni jambo la hekima kutenga wakati wa kutosha, kusafiri na kufika huko kwa wakati kamili?
Ni jambo la busara kuhakikisha kwamba tuna dakika za ziada ili tusichelewe, hata tukipatwa na “tukio lisilotazamiwa” njiani” (Mhu 9:11). Jambo ambalo linaweza kumsaidia mtu yeyote afike kwa wakati ni kujua vizuri muda wa kusafiri, ambao anahitaji,
Watu wengine wanahitaji kufanya mipango inayofaa ili kuondoka kazini mapema vya kutosha, na hivyo kufika kwenye mikutano ya Kikristo kwa wakati mzuri.
Ikiwa tuna watoto wachanga, ni vigumu zaidi kufika kwa wakati kwenye mikutano. Kwa kawaida, mama ndiye anayeachiwa jukumu la kuwatayarisha watoto, lakini washiriki wengine wa familia wanapaswa kumsaidia, ili wote waondoke kwa wakati kwenda kenye ibada.
Familia iweke muda wa kuondoka nyumbani, ili waondoke kwa wakati na kufika kwa wakati.
Zijue faida za kufika kwa wakati kwenye Ibada
1. Kutafakari kuhusu baraka ambazo tunapata tunapofika kwenye ibada ya Kikristo kwa wakati kunaweza kuimarisha tamaa na azimio letu la kufanya yote tunayoweza ili tusichelewe.
2. Kubadilishana uzoefu na waumini wengine
Mtu mmoja mwenye mazoea ya kufika kwenye ibada na mikutano kwa wakati, anasema hivi: “Ninachofurahia kuhusu kufika mapema ni kwamba ninapata nafasi ya kuwasalimu ndugu na dada, kuongea nao, na kuwafahamu vizuri zaidi”. Tunapofika mapema kwenye Jumba la Ufalme, tunaweza kufaidika kwa kusikia kuhusu uvumilivu na utumishi wa uaminifu wa wengine ambao wamehudhuria. Tunapohudhuria mikutano kwa wakati na kuzungumza nao mambo yenye kujenga, tunaweza kuwatia moyo ndugu na dada zetu na ‘kuwachochea katika upendo na matendo mazuri’ (Ebr. 10:24-25).
3. Kushiriki kwenye nyimbo na sala za kufungua ibada
Wimbo na sala ya kufungua ibada ni sehemu ya maana sana ya ibada (Zab 149:1). Nyimbo zinamsifu Yehova, na kutukumbusha sifa ambazo tunapaswa kusitawisha, na nyimbo zinatutia moyo kushiriki kwa shangwe katika huduma.
Namna gani sala ya kufungua? Katika nyakati za kale, Yehova aliliita hekalu ‘nyumba yake ya sala’ (Isa 56:7). Leo, tunakusanyika ili kusali kwa Mungu katika ibada zetu. Sala ya kufungua inamwomba Yehova, atuongoze na kutupatia roho takatifu. Tunapaswa kuazimia kufika kwenye ibada zetu kwa wakati, ili tushiriki wimbo na sala ya kufungua ibada.
4. Hakuna anayeimba na kumsifu Mungu, na kuomba kwa niaba ya muumini mwingine. Hivyo, hakuna anayepokea thawabu kutoka kwa Mungu, kwa kuimba na kuomba, kwa niaba ya muumini mwingine. Thawabu kutoka kwa Mungu ni ya muumini binafsi; hivyo, ni muhimu kuwahi kwenye ibada ili kupokea thawabu hizo.
5. Kujiandaa kiakili, mawazo na kiroho, tayari kwa kushiriki kwenye ibada
Inatayarisha akili na mioyo yetu kupokea habari ambazo zitazungumziwa.
6. Kuwahi kwenye sehemu ya ibada kabla ya wakati, NI USHINDI WA KWANZA, na kuchelewa kufika ni dalili ya kupoteza ushindi wako mapema kwenye ibada. Kuchelewa ni fedheha ambayo inakumaliza nguvu ya kiroho ya kwenda kufanya mambo makubwa.
Tumeona faida zinazopatikana kwa kuwahi kufika kwenye ibada. Hivyo, usikose kupata faida hizo, kutokana tu na kuchelewa kufika kwenye ibada.
Tumeona pia kuwa Mungu mwenyewe anafanya mambo kwa kufuata muda alioweka. Je iweje sisi, tunakwenda kwenye ibada ya Mungu tukiwa tumechelewa. Tujitahidi kusitawisha mazoea ya kufuata muda, katika kwenda kwenye ibada ya Mungu, ili tufike kwa wakati.