Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 15,819
- 33,255
1. Katiba hii imewapa nguvu Wanasiasa na Wateuliwa wao kuamua chochote bila kuhojiwa na kuwajibika kwa yeyote. Hili linawawezesha CCM kutumia fedha za Umma kwa shughuli zao bila kuhojiwa na kuambiwa lolote na yeyote. Leo hii kwenye Halmashauri zetu Mkurugenzi wa Halmashauri anaweza pewa amri na Mwenyekiti wa CCM au Katibu wa CCM (Mkoa/Wilaya) kutoa fedha za Umma ambazo ni kodi za Wananchi kwa Shughuli za Kichama kama kuwapa posho wajumbe wa CCM, Kununua t-shirt na mabango kwa ajili ya CCM.
Endapo sasa tukisema tuwe na Katiba Mpya inayosema hakuna Rais kuteua Wakurugenzi wa Halmashauri na Wakurugenzi pia wakurugenzi hawa watawajibika kwa wananchi moja kwa moja au Kamati za Bunge, basi mjue mrija mkuu wa CCM kuenjoy pesa za Umma utakuwa umekatwa na Chama kitajifia.
2. Katiba ya sasa imempa mamlaka Rais kutowajibika kufuata ushauri wa mifumo rasmi ya nchi hivyo kumweka Rais kuwa Alpha na Omega. Kwenye hili Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM halazimiki kufuata ushauri wa mtu yeyote, iwe kwenye teuzi, iwe kwenye masuala ya fedha za nchi ambazo ni kodi za Wananchi au jambo lolote lile. Kwenye hili Rais anaweza leo amuru fedha za walipakodi kwenda kutumika kwa shughuli ambazo hazipo kwenye bajeti au hazikuidhinishwa na Bunge.l kwa faida yake binafsi au ya CCM.
Hivyo fedha za walipakodi zinatumiwa na watu hawa kwa namna wanavyoona wao inafaa na hakuna wa kuwaambia au kuwafanya chochote. Fedha za umma zinatumiwa kwa utashi wa Rais hivyo anaweza toa amri wa Katibu Mkuu hazina na kumwambia toa Bil 8 mpe mwanangu na hakuna anayeweza kuhoji au kufanya chochote.
3. Katiba imeweka mamlaka yote ya uteuzi na utenguzi wa Rais hivyo kulazimisha Mifumo kufanya kazi kwa matakwa ya Rais na sio Sheria za nchi. Hili linawanufaisha CCM kwa kuwa Rais ambaye ni Mwenyekiti wao ndiyo mwenye final say.
Kwenye hili CCM wakimwambia msimamizi wa Uchaguzi tunataka jimbo fulani. Msimamizi wa Uchaguzi hawezi simamia haki kwa sababu anajua kuwa akisimamia haki tu Rais ambaye ni mwenyekiti wa Chama anaweza kumfanya kuwa jobless kwa kumtengua.
Leo hii CCM wakimwambia Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Mtangaze mgombea wa CCM kashinda kura za urais kwa asilimia 80 hawezi kuwabishia kwa sababu anayeamua maisha yake na kura yake na uwepo wake ni huyo Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM.
Pia Watendaji wa Serikali wanashindwa kuwa huru kusimamia Sheria maana wanajua endapo wakisimamia Sheria kinyume na matakwa ya Chama cha Mapinduzi, kesho Waziri ambaye ni mwana CCM anaweza kuja kumsimamisha kazi au hata kumfukuza Kazi.
4. Kupitia Katiba hii iliyo palarlyize mifumo ya nchi. CCM hasa Viongozi wake na Familia zao wananufaika sana na Rushwa kubwa ambazo zinawafanya waishi bila hofu ya kukamatwa na kuchukuliwa hatua.
Kwenye hili ni CCM ndio wanaoamua nani ashtakiwe Mahakamani na kwa kosa gani. Hii ni kwa sababu leo hii mifumo haiwezi fanyia kazi Rushwa kubwa za CCM kwa sababu Katiba imeiweka mifumo kufanya kazi kwa maelekezo ya Wanasiasa na sio kwa uhuru.
Sote tunaona ni Wanasiasa wanaoamrisha TAKUKURU kufanya uchunguzi wa Mambo. Huwezi kuta TAKUKURU anachunguza wanasiasa kwa sababu ana taarifa za Rushwa za Wanasiasa. Hili linafanya mifumo kuwaona Wanasiasa kama Mungu na sio wanasiasa kuiheshimu mifumo.
Narudia tena.
Nchi yetu itapata maendeleo pale tu tutakapopata KATIBA MPYA.
Na kamwe, Watanzania tusitegemee CCM watakubali suala la KATIBA MPYA. Maana wao ndo wanufaika wakuu wa udhalimu unaofanyika kutokana na ubovu wa KATIBA tuliyonayo sasa.
Endapo sasa tukisema tuwe na Katiba Mpya inayosema hakuna Rais kuteua Wakurugenzi wa Halmashauri na Wakurugenzi pia wakurugenzi hawa watawajibika kwa wananchi moja kwa moja au Kamati za Bunge, basi mjue mrija mkuu wa CCM kuenjoy pesa za Umma utakuwa umekatwa na Chama kitajifia.
2. Katiba ya sasa imempa mamlaka Rais kutowajibika kufuata ushauri wa mifumo rasmi ya nchi hivyo kumweka Rais kuwa Alpha na Omega. Kwenye hili Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM halazimiki kufuata ushauri wa mtu yeyote, iwe kwenye teuzi, iwe kwenye masuala ya fedha za nchi ambazo ni kodi za Wananchi au jambo lolote lile. Kwenye hili Rais anaweza leo amuru fedha za walipakodi kwenda kutumika kwa shughuli ambazo hazipo kwenye bajeti au hazikuidhinishwa na Bunge.l kwa faida yake binafsi au ya CCM.
Hivyo fedha za walipakodi zinatumiwa na watu hawa kwa namna wanavyoona wao inafaa na hakuna wa kuwaambia au kuwafanya chochote. Fedha za umma zinatumiwa kwa utashi wa Rais hivyo anaweza toa amri wa Katibu Mkuu hazina na kumwambia toa Bil 8 mpe mwanangu na hakuna anayeweza kuhoji au kufanya chochote.
3. Katiba imeweka mamlaka yote ya uteuzi na utenguzi wa Rais hivyo kulazimisha Mifumo kufanya kazi kwa matakwa ya Rais na sio Sheria za nchi. Hili linawanufaisha CCM kwa kuwa Rais ambaye ni Mwenyekiti wao ndiyo mwenye final say.
Kwenye hili CCM wakimwambia msimamizi wa Uchaguzi tunataka jimbo fulani. Msimamizi wa Uchaguzi hawezi simamia haki kwa sababu anajua kuwa akisimamia haki tu Rais ambaye ni mwenyekiti wa Chama anaweza kumfanya kuwa jobless kwa kumtengua.
Leo hii CCM wakimwambia Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Mtangaze mgombea wa CCM kashinda kura za urais kwa asilimia 80 hawezi kuwabishia kwa sababu anayeamua maisha yake na kura yake na uwepo wake ni huyo Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM.
Pia Watendaji wa Serikali wanashindwa kuwa huru kusimamia Sheria maana wanajua endapo wakisimamia Sheria kinyume na matakwa ya Chama cha Mapinduzi, kesho Waziri ambaye ni mwana CCM anaweza kuja kumsimamisha kazi au hata kumfukuza Kazi.
4. Kupitia Katiba hii iliyo palarlyize mifumo ya nchi. CCM hasa Viongozi wake na Familia zao wananufaika sana na Rushwa kubwa ambazo zinawafanya waishi bila hofu ya kukamatwa na kuchukuliwa hatua.
Kwenye hili ni CCM ndio wanaoamua nani ashtakiwe Mahakamani na kwa kosa gani. Hii ni kwa sababu leo hii mifumo haiwezi fanyia kazi Rushwa kubwa za CCM kwa sababu Katiba imeiweka mifumo kufanya kazi kwa maelekezo ya Wanasiasa na sio kwa uhuru.
Sote tunaona ni Wanasiasa wanaoamrisha TAKUKURU kufanya uchunguzi wa Mambo. Huwezi kuta TAKUKURU anachunguza wanasiasa kwa sababu ana taarifa za Rushwa za Wanasiasa. Hili linafanya mifumo kuwaona Wanasiasa kama Mungu na sio wanasiasa kuiheshimu mifumo.
Narudia tena.
Nchi yetu itapata maendeleo pale tu tutakapopata KATIBA MPYA.
Na kamwe, Watanzania tusitegemee CCM watakubali suala la KATIBA MPYA. Maana wao ndo wanufaika wakuu wa udhalimu unaofanyika kutokana na ubovu wa KATIBA tuliyonayo sasa.