Uchaguzi 2020 Ziko wapi sera zinazohusu kero za wafanyakazi toka kwa wagombea wetu wakuu?

Dumbuya

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2014
Posts
596
Reaction score
878
Wanajamvi,

Katika sikia sikia zangu za sera na ahadi mbalimbali za wagombea katika uchaguzi wa mwaka huu ; kundi moja kubwa la "Wafanyakazi" (Umma na Binafsi) ambao ni walipa kodi wa uhakika hapa nchini ni kama limesahaulika au halijapewa kipaumbele kabisa.

Wapi sera zinazohusu kero za wafanyakazi toka kwa wagombea wetu wakuu?

- Pensheni na mafao mbalimbali
- Mifumo ya ajira
- Makato ya Kodi
- Kima cha chini cha mshahara
- Nyongeza ya mishahara

Wapi nguvu ya wafanyakazi katika taifa hili au ndo tumekubaliana kuwa ajira ni [emoji706]

Dumbuya.
 
Wafanyakazi tunaimani na Dr Magufuli, anatufanyia mambo mazuri
Vipi suala la mafao na Pensheni mbona haliongelewi ipasavyo?

Fao la kujitoa, naamini hiki ndo kilio cha wafanyakazi wengi kwenye hili. Kusubiri miaka 55/60 ni kejeli.
 
Wafanyakazi tunaimani na Dr Magufuli, anatufanyia mambo mazuri

Wafanyakazi! Wangapi? Jiseme wewe "mfanyakazi"

Mnadharau hili kundi lakini;
Mimi! Mke wangu! Wadogo zangu 4! Wazazi 2! Ndugu tunao tegemeana zaidi 30! Wenza wao! Watoto wao, daaaah! Kundi kubwa sana mmelikosa
 
CCM inewadharau wafanyakazi sana kwa kipindi chote cha miaka 5. Tusifanye makosa kiruhusu ccm ibaki mwaka huu.
 
Kwa hili la wafanyakazi, mkombozi Lissu alishaongelea. Ataleta ahueni kubwa sana.
 
Afadhari hata zanzibar Mwinyi amewaahidi kuongeza mishahara halafu magufuli bila aibu jana amempongeza Sheini kwa kuongea mshahara kwa wafanyakazi wa zanzibar kweli wewe mzee kosa tulilokukosea wafanyakazi ni kubwa kiasi gani,umefunga uhamisho,hutaki kuboresha mishahara na kuboresha maslahi ya watumishi ili hali unajua maisha yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiongozi ambaye hajali sheria na haki za watu hafai kuwa kiongozi.

Watumishi wengi wanaopuuza hili ni wale wanaoshiba vizuri, lakini hili lisiwafanye mshindwe kufanya maamuzi sahihi
 

Dawa ya watu aina ya magu ni kuwapuuza tu na hivyo kujali maisha yako. Kumlilia na kumsujudia ni kumpa tu sifa na utukufu asio stahili.
 
Mfanyakazi mwenye 1Mil gross anakatwa PAYE Tshs.105,000/- .

Ukipiga hesabu za mwaka ni kuwa mshahara mzima wa mwezi mmoja anakatwa kama kodi.
 
Wasubiri tulete ndege nyingine tano na tukamilishe daraja la busisi, bila kusahau stigliza na sgr..
 
Kama baba mwenye nyumba ananyanyasa wapangaji, unadhan jirani atafanyaje. Kiukweli hayo siyo kipaumbele cha hawa viongozi wetu hasa chama tawala.

Wao vipaumbele ni ujenzi wa barabara, madaraka, ununuzi wa ndege tena bado anafikiria kuongeza zingine akirejea madarakani.

Tunaambiwa tufunge mikanda as if nchi ipo kwenye mapambano ya kivita duuh
 
Ni wakati muafaka kwa watumishi kutumia haki yao ya msingi ipasavyo sababu serikali haiwahitaji tena watumishi kwani hawana mchango kwa nchi ndo maana hawapandi vyeo,hawana nyongeza za mishahara,hawana posho ya aina yoyote,kikokotoo Cha pensheni ni changamoto.wasifanye makosa tena inawagharimu milele.

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…