ziko wapi shule za vipaji maalum?

mr. over view

Member
Joined
Jan 3, 2014
Posts
14
Reaction score
0
hivi punde tumeshuhudia matokeo ya mitihani ya kidato cha sita lakin cha kushangaza ndani ya shule kumi bora, shule za vipaji maalum hazionekani na zaidi ya hayo tumeshuhudia uwepo wa shule ya kata ndani ya kumi bora [kisimiri]. Je hi ni kuonyesha kwamb vipaji kwa sasa vipo kata?
 

kibaha ni shule ya nini???…. Acha ushabiki wewe
 

kwanza kabisa, naomba nikusahihishe, Kisimiri ni moja yashule za vipaji kwa hivi sasa. Na pili, uwepo wa hizo shule ambazo wewe unaziita za kata imetokana hizi shule kuwa na watahiniwa waliosoma masomo ya arts pekee na it seems mitihani ya haya,masomo haikuwa migumu sana. Hapo kwenye kumi bora, shule zenye masomo ya sayansi (au pamoja na arts) ni chache ....Ndio maana unakutashule kama Mzumbe, Ilboru, Tabora Boys zimetupwa mbali!
 


Ha ha ha ha..eti Kisimiri ni shule ya kata!!

Vipi na orodha ya wanafunzi bora wa kwanza pia hazipo?
 
Shule za vipaji maalumu zitabaki kuwa hivyo lazima tuukubali ukweli huu hata kama wengine tunamachungu ya kutopata nafasi katika shule hizo.kuweka kumbukumbu vizuri kwa wavulana shule hizi ni Kibaha,Iliboru.Mzumbe na Tabora wavulana.

Kulinganisha shule hizi na feza boys,kisimiri,igawele na shule hizi ni kulinganuisha jua na nyota.
1.Toka mkoloni shule hizi zimedhihirisha ubora wake mpaka leo.
2.Idadi ya wanafunzi wanaotahiniwa katika shule hizi ni kubwa sana ukilinginisha na shule nilizozitaja hapo juu zenye watahiniwa wachache mfano Feza ilikuwa na watahiniwa 60 pekee.daraja la 1-36,daraja la pili 18,daraja la tatu 6,hakuna four wala ziro.igowole ambayo ni ya kwanza ina watahiniwa 30tu,Kisimiri watahiniwa 52 tu.daraja la 1 -34,la pili 10,la tatu 8.

3.Shule nyingi hizi ndogondogo hutegemea sana udanganyifu kwenye mitihani ndiyo maana inaweza chomoza mwaka huu ikapotea kabisa isionekane tena wakati hizi za vipaji watu hutunisha misuli hasa kombi zenyewe nyingi ni za sayansi mfano pcb Hebu tuzipe

kwa mamtiki hiyo shule za vipaji maalumu zimezihirisha uwezo wao angalia matokeo yake na idadi ya watahiniwa.

1.Kibaha watahaniwa 161,daraja la kwanza 82,la pili 59,la tatu 18,la nne 2 hakuna 0.
2.Mzumbe watahiniwa 125,daraja la kwanza 56,la pili 38,la tatu 29,la nne 2 hakuna 0.
3.Iliboru watahiniwa 150,daraja la kwanza 53,la pili 50,la tatu 44,la nne 3 hakuna 0.
4.Tabora wavulana watahiniwa 158,daraja la kwanza 49,la pili 62,la tatu 45,la nne 2 hakuna 0.

Huwezi kuzinganisha na shule za watahiniwa wachache,hebu linganisha na shule zingine za wanafunzi wengi kama Tambaza,Pugu,Milambo ndo utajua kweli hizi shule ni majembe.

hazina daraja 0,daraja la nne ni 7 tu

hongereni madogo kwa kudhihirisha uwezo wenu njia nyeupe vyuo vikuu.

UKIONA NYANI MZEE JUA KAKWEPA MISHALE MINGI.
 
Igowole ni shule mpya bado na bado haijapewa hadhi ya vipaji maalum,shule ipo kwenye mazingira magumu ila waalimu na wanafunzi wamejitolea kufanya vizuri,
na ukumbuke wanaochaguliwa wote wamefaulu form four,
tofauti na hizo zinazoitwa za vipaji ni passmarks za kidato cha nne,
Ile ya kwanza ina jina la kihehe nayo ni ya vipaji?..just being curious
 
Big Result now...!

Nashindwa kuelewa sisi watanzania ni watu wa aina gani. Kimsingi hii ni kama vile kutanua Goli ili kuweza kufunga kiurahisi na kujisifu eti sisi najua.....

Hebu tazama
Kutoka 0 zaidi ya 2000 last year mpaka 0 around 600 this year.
Kutoka Div I 300 last year mpaka Div I 4000 this year, Huu ni utani, atakayefurahia haya lazima atakuwa na matatito ya akili. (All are numbers are rounded to the nearest whole number)

Kabla ya kuanza kuzibeza hizo shule maalumu nafikiri tungeangalia kwanza uhalisia wa kufaulu na matokeo kwa ujumla wake ndio tungeweza kutoa mchago ulio bora zaidi. Binafsi hainiingi akilini wala sioni haki ya kuzibeza special schools maana kiuhalisia wao ndio waliofana vizuri hasa katika nyanja za sayasi Biology, Physics, Mathematics, Chemistry na Geography.

Kujisifu tumefaulisha bila kuchnaganua uwezo wa mwanafunzi aliye faulu ni sawa na kuuza ng'ombe ili kulipia deni la kuku.
 

Ivi Tanzania kuna shule za vipaji maalumu? na kama zipo wana vipaji gani hasa? kuimba, mpira, riadha, kucheza au vipaji gani hasa?
 
Ivi Tanzania kuna shule za vipaji maalumu? na kama zipo wana vipaji gani hasa? kuimba, mpira, riadha, kucheza au vipaji gani hasa?

Kimsingi Shule hizi serekeli ilishazifuta, hasa pale waziri mwenye dhamana aliposema kuendelea kuwepo kwa shule za wanafunzi wenye vipaji maalumu ni ukiukwaji wa haki za binadamu na uwekaji wa matabaka katika elimu, tena ni kukiuka misingi ya usawa katika jamii. Kilichopo sas ni ile asili ya kujituma, heshima ya shule iliyokwisha jiwekea toka zamani (yaani Historical background) na mazingira ya kimasomo ikiwemo asili ya kiushindani ndiyo vitu vinavyofanya kazi mpaka sasa. Ila wizara na serekali kimsingi ilishaachana na hizi shule ikiwemo Msalato, Kilakala na nyinginezo nyingi.

Nahisi vijana hawa wanastahili sana kupongezwa badala ya kubezwa hasa unapoanza kuyachambua matokeo haya kwa kina na kwa ki-mchepuo. hasa ukiangalia comment za ndugu yangu ng'wana onang'wa kulwa kama ifuatavyo:-

1.Kibaha watahaniwa 161,daraja la kwanza 82,la pili 59,la tatu 18,la nne 2 hakuna 0.
2.Mzumbe watahiniwa 125,daraja la kwanza 56,la pili 38,la tatu 29,la nne 2 hakuna 0.
3.Iliboru watahiniwa 150,daraja la kwanza 53,la pili 50,la tatu 44,la nne 3 hakuna 0.
4.Tabora wavulana watahiniwa 158,daraja la kwanza 49,la pili 62,la tatu 45,la nne 2 hakuna 0.
 

umesema kweli mkuu hata kama shule hizi za vipaji zimefutwa imebakia ile asili ya kujituma na wanafunzi wanaofanya vizuri kidato cha nne wanachaguliwa katika shule hizi,nafikiri bado zinapewa first priority ya kuchagua wanafunzi wazuri wanaoingia kidato cha tano.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…