Dr. Balantanda amenikumbusha mbali. Miongoni mwa nyimbo nazopenda sana ni "Ni wewe pekee" wa Nguza Viking/Marquis na Jack wa Nico Zengekala. Nikisikiliza nyimbo hizi nahisi mapigo ya moyo yanabadilika.
Single ya Alikiba, "Usinisemee kama napenda kula" tutaisikiliza kweli?
Nico Zengekala(R.I.P) pamoja na kilema chake cha upofu alikuwa habari nyingine mkuu,angalia mashairi ya nyimbo hizi utaona maana ya ninachokisema ama ulichokisema wewe hapo juu...
Jackie...
Mtoto Jackiee,mtoto wa Nirobi
Ingawa ni mara ya kwanza mimi nawe Jackiee
Tulipokutana palee Kampala kwenda Nairobi
Tulifurahiana sana kama tuliishi mwaka
Tabia yako njema kweli sitoisahau.
Mtotoo Jackie,mtoto wa mama Jackie wa mapendo
Japokuwa tuliachana stendi ukielekea Nairobi nyumbani eeh
Lakini tutakutana,nitakuja kutembelea,nawe karibu nyumbani eeh
Ooh Jackie yeyeeeh
Mtoto wa mama Jackie wa mapendo
Japokuwa tuliachana stendi,ukielekea Nairobi nyumbani eeh
LAkini tutakutana,nitakuja kutembelea,nawe karibu nyumbani eeh
Ooh Jackie yeyeeeh
Kiitikio:
Mtoto Jackie eeh,mpenzi wangu najaribu kukusahau lakini nashindwa
Hasa ni ile ndoto inayonisumbua naota unaniletea kifuko cha DHAMBARAU
Nimejaribu kukusahau lakini nashindwa,hasa ni kwa ile ndoto inayonisumbua eeh
Mtoto Jackie eeh,mpenzi wangu najaribu kukusahau lakini nashindwa
Hasa ni ile ndoto inayonisumbua naota unaniletea kifuko cha DHAMBARAU
Nimejaribu kukusahau lakini nashindwa,hasa ni kwa ile ndoto inayonisumbua eeh
Mtoto Jackie eeh,mpenzi wangu najaribu kukusahau,lakini nashindwa,hasa ni kwa ile ndoto inayonisumbua naota unaniletea kifuko cha DHAMBARAU
Sauti yako nyororo inaniua sana na mwendo wako wa maringo unanikondesha mamaaah,ayoleli mwanamama nakuwinda sana Jackie yeyeyeeeh mwanamamaah aeaeeh
Mtoto Jackie eeh,mpenzi wangu najaribu kukusahau,lakini nashindwa,hasa ni kwa ile ndoto inayonisumbua naota unaniletea kifuko cha DHAMBARAU
Mvumilivu hula mbivu,Jacki yeyeeeh,mvumilivu hula mbivu Jackie yeyeeeh
Jaribu kuvumilia yeeh tutaonana mamaah kama sio Kampala ni Tanzania mamaa
Jackie yeyeyeeh mwanamama aeaeeh
Mtoto Jackie eeh,mpenzi wangu najaribu kukusahau,lakini nashindwa,hasa ni kwa ile ndoto inayonisumbua naota unaniletea kifuko cha DHAMBARAU
Jackie yeyeyeeh nitakuja Nairobi
Nitakuja Nairobi eeh nikuone mamaah
Jackie yeyeyeeh nitakuja Nairobi
Tutafurahi pamoja mi na wewe mama yeeh
Jackie yeyeyeeh nitakuja Nairobi
Jackie yeyeyeeh Maneno sema na yeye
Jackie yeyeyeeh nitakuja Nairobi
ama kitu
Solemba
Solemba solemba solemba aaaaaaaaaah
Sitakuwa nikifika nyumbani kwako,aibu nilopata ni kubwa sana,
Ahadi nilopewa ilivunjwa oooh ooooh hata bila kosa,
Ulinipa ahadi tukutane kwenu,nikitumaini nimewahi,
Nilichopata kwako ni matusi oooh ooh na dharau tele,
Ungenieleza ukweli Solemba,kuliko kunidanganya ooh,
Najuta kuitimiza ahadi oooh ambayo si ya kweli,
Ungenieleza ukweli Solemba,kuliko kunidanganya ooh,
Najuta kuitimiza ahadi oooh ambayo si ya kweli,
Bridge
Ulinipa ahadi tukutane kwenu,nikitumaini nimewahi,
Nilichopata kwako ni matusi oooh ooh na dharau tele,
Ungenieleza ukweli Solemba,kuliko kunidanganya ooh,
Najuta kuitimiza ahadi oooh ambayo si ya kweli,
(Wote): Nilikupenda kimapenzi Solemba ee,Ila dharau uliweka mbele Solemba
Zengekala: Ulinikana mbele za watu ati hunifahamu,
Ndugu zako na marafiki walianza kutoka nje,
Waliponiona ni mimi,walishangaa sana mama,
Mbona hivyo solemba mama eee
(Wote): Nilikupenda kimapenzi Solemba ee,Ila dharau uliweka mbele Solemba
Zengekala: Nilikuuliza mbona ulinitendea hivyo Solemba,
Ulisema mimi hujipendekeza kwako tena sana,
Na kuwa hunipendi,nakusumbua bure mamaa,
Mola yupo Solemba,Eloi yupo mamaa.
(Wote): Nilikupenda kimapenzi Solemba ee,Ila dharau uliweka mbele Solemba
Zengekala: Nilichomwa na jua toka asubuhi,
mpaka saa nane Solemba,Sababu ya kukungoja wewe
Kumbe ulikuwa ndani,unachungulia dirishani,
Huna huruma Solemba,I shall never forget you mamaa,
(Wote): Nilikupenda kimapenzi Solemba ee,Ila dharau uliweka mbele Solemba
Zengekala: Sikutaki tena,sina haja nawe,
Nimeshapata mwingine anayenipenda kwa roho moja,
Tafuta bwana mwingine utakayembabaisha kama mimi,
Nimeshituka Solemba,nimeshituka solemba.
(Wote): Nilikupenda kimapenzi Solemba ee,Ila dharau uliweka mbele Solemba
Zengekala: Lalala lalala lalala lalalalala
Nimeshapata mwingine anayenipenda kwa roho moja,
Tafuta bwana mwingine utakayembabaisha kama mimi,
Nimeshituka Solemba,lololo lolololo mama lo
(Wote): Nilikupenda kimapenzi Solemba ee,Ila dharau uliweka mbele Solemba