ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

Bala,
Pia mimi nilikuwa napenda sana vibao vya Salna Brothers hasa Ufitini, pia wale New Urafiki Jazz walikuwa na wimbo unaimbwa hivi.......

.......kuna maneno nimeyasikia kwa majirani, ya kwamba
una mpango wa kuoa mke mwingine...........

Usiniache mpenzi eeeh ooh mary eeh, elewa wafitini mama si watu wazuri mamaaa.

Pia vibao maridadi kama Kiu ya Jibu, Sintaisononesho roho yangu toka DDC. Pili toka Tancult, Mwalalamika Pembeni- Vijana Jazz etc


Balatanda, tutafutie pia tune signatures? nyimbo za kutambulisha vipindi vya .......Mchana Mwema, Jioni Njema, Jibu lako, Nipe Habari, Ombi lako, Karibu RTD....
 
mkuu Balantanda na wadau wengine wa muziki,

hivi mmepita hapa?

https://www.jamiiforums.com/entertainment/157696-maji-pipa-tano-kwa-mikono-toka-mtoni.html


kuna hii kitu wakuu:

.........nichote maji pipa tano kwa mikonoo,
kutoka mtoni,
fikiri,
nitaweza vipi!!

kiitikio:
Amina kipenzi changu
mimi sitaweza,
agizo la wazazi wako linaniwia vigumu...............

(kasauti ka loviii kaningilia)
pendekezo langu mama
kukupata wewe amina,
masharti niliyopewa na wazi wako
sitaweza.............

Amina kipenzi changu
mimi sitaweza,
agizo la wazazi wako linaniwia vigumu...............


jamani mniwie radhi, ...................huu wimbo siukumbuki vizuri, ..................nakumbuka ulipigwa na super lovii kama sikosei................ (wakongwe mtanisahihisha)............. nimeusaka youtube, hakuna kitu............... naomba jamani kama kuna mtu ana clip yake hata audio tu, atuwekee jamani, tuburudike................ hata lyrics zitafaa kama clip itakuwa issue................. dah, OLD IS GOLD!!!!!!!...........
 
MWIMBAJI na mtunzi mahiri nchini, Shukuru Majaliwa, ameanza kazi rasmi katika bendi ya Mlimani Park "Sikinde Ngoma ya Ukae", kwa kuipua kibao chake cha kwanza kinachokwenda kwa jina la "Fadhila ya Punda ni Mateke".
Shukuru alijiunga Sikinde baada ya kuipiga teke bendi hasimu ya Msondo Ngoma "Mambo Hadharani" ambayo alikuwa akiifanyia kazi tangu kufariki dunia kwa Ali Mhoja Kishiwa "TX Moshi William" mwaka 2006.
Majaliwa ambaye ni muajiriwa wa bendi ya Mwenge Jazz, inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), atakuwa akiitumikia Sikinde wakati wa muda wake wa mapumziko.
Mbali ya wimbo huo, Majaliwa ametunga wimbo mwingine ambao bado hajaupa jina na unaendelea kufanyiwa mazoezi na bendi hiyo, ambayo kwa sasa imesimamisha maonyesho kupisha mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Sikinde kwa sasa imejichimbia kwenye ukumbi wake wa DDC uliopo Mwenge, jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kuandaa albamu mpya wanayotarajiwa kuiingiza sokoni baadaye mwaka huu.

NB....Hii nimeipata kwenye gazeti la Tanzania Daima la leo..

Shukuru Majaliwa ni mmojawapo wa wanamuziki mahiri kabisa wa Tanzania,ana kipaji
sauti yake inashabihiana kabisa na ile ya hayati TX Moshi William na alikuwa anaziba
hasa pengo la TX pale msondo....Hakika hili ni pigo kwa Msondo na ni neema kwa
Nginde.


Bala.

[TD="bgcolor: #ffffff"]
Majaliwa aipa Sikinde Fadhili ya Punda


na Ruhazi Ruhazi

[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #FFFFFF"]
[/TD]
 
...Kwa kuongezea kulikuwa na mtu anaitwa Ally Makunguru alikuwa akipiga 2nd Solo na some times rythm gitaa na mpiga drums anaitwa Chipembele Saidi. Kwa ambao kazi yake hawaifahamu vizuri kuna wimbo unaitwa Kata ya maji ukweni..jamaa amekaanga vyepe humo sio pole pole.
 
Tukunyema!
Mmenikumbusha mbali. Walikuja JKT Makutupora mwaka 90 au 91 (sikumbuki vizuri, Operesheni Kambarage ilikua). Walahi machungu yote ya jeshi tuliyasahau siku hiyo
 
Hivi ule wimbo wa Asossa Bomoa tutajenga kesho (ulipigwa marufuku RTD) unapatikana kwa sasa?
 
Me niko tayari kutoa kiasi chochote reasonably kupata hizo nyimbo,anyone???yeah,and I may also take for free!!
 
Mi bana ni Le champioo Sikinde ile ya Bitchuka,Gurumo,Maalimu Hamisi Kinyasi,Chidumule,Bushoke,Gama,Mwanyiro computer,Mulenga,King Michael Enock n.k nakumbuka nyimbo kama Clara,neema ,Christina Bundala,then numberi 2 ni Tancut ya akina Kyanga Songa na Kasaloo Kyanga ,Salvador,Kawalee sauti tamuuu we acha tu
 
Me niko tayari kutoa kiasi chochote reasonably kupata hizo nyimbo,anyone???yeah,and I may also take for free!!
Mtafute John Kitime wa wana Njenje yeye ni kama iliyokuwa RTD,wanapiga Salender bridge au mcheki kwenye FB
 
Nipo wimbo wao moja tu maana ndo ilikuwa yangu hiyo
 
Balantanda, hujawatendea haki Vijana Jazz Band kama hutataja wimbo wa mesenja kazua balaa
 
Mkuu Bala vipi Kyauri voice ya Mzee Iteitei ,mwendo wa jongoo na vumbi nyuma naomba simulizi kidogo,nakumbuka sax la mzee Iteitei
 
Balantanda, hujawatendea haki Vijana Jazz Band kama hutataja wimbo wa mesenja kazua balaa
Mkuu wangu sana Ngambo Ngali.....

Wimbo wa Visa vya mesenja(Mesenja kaleta balaa) haukuimbwa na Vijana Jazz Band......Uliimbwa na Maxmillan Bushoke akiwa na Bima Lee Orchestra wana Magnet Tingisha...
 
Kitu Ni wewe kipenzi utunzi wake Juma Ubao akiwa na The Six Manyara Band.

Ni wewe kipenzi nikupendae,kwa jina unaitwa Tabu,
Ni wewe kipenzi nikupendae,kwa jina unaitwa Tabu,
Mwenye sura nzuri ya kupendeza,tabia na heshima yako ni ya kusifika,
Japo kuwa maana ya jina lako ni matatizo,kwangu lina maana ya furaha na faraja.
Mwenye sura nzuri ya kupendeza,tabia na heshima yako ni ya kusifika,
Japo kuwa maana ya jina lako ni matatizo,kwangu lina maana ya furaha na faraja.

Ninalokuomba jihadhari na walimwengu,usione wakikuchekea,ukaona ni marafiki,na siri ya penzi letu ukawaeleza.
Ninalokuomba jihadhari na walimwengu,usione wakikuchekea,ukaona ni marafiki,na siri ya penzi letu ukawaeleza.
Watafanya kila njia waone tumetengana,kumbe penzi letu linawasibu moyoni, tafadhali chunga penzi letu kama benki inavyochunga fedha...

Ni wewe kipenzi nikupendae,kwa jina unaitwa Tabu,
Ni wewe kipenzi nikupendae,kwa jina unaitwa Tabu,
Mwenye sura nzuri ya kupendeza,tabia na heshima yako ni ya kusifika,
Japo kuwa maana ya jina lako ni matatizo,kwangu lina maana ya furaha na faraja.
Mwenye sura nzuri ya kupendeza,tabia na heshima yako ni ya kusifika,
Japo kuwa maana ya jina lako ni matatizo,kwangu lina maana ya furaha na faraja.

Ninalokuomba jihadhari na walimwengu,usione wakikuchekea,ukaona ni marafiki,na siri ya penzi letu ukawaeleza.
Kumbe penzi letu linawasibu moyoni, tafadhali chunga penzi letu kama benki inavyochunga fedha...

Kiitikio: Nakuapia wallah ooo wallah uliyoyasema mimi nimeyasikia...
Nakuapia wallah ooo wallah(sitothubutu kutoa siri ya penzi letu mamaa)..
Nakuapia wallah ooo wallah(napenda kiapo chetu kiwe cha kweli mpenzi)..
Nakuapia wallah ooo wallah(muhimu uliyoyasema mimi nimeyasikia)...
Nakuapia wallah ooo wallah(sitothubutu kutoa siri ya penzi letu mamaa)..
Nakuapia wallah ooo wallah(napenda kiapo chetu kiwe cha kweli mpenzi)..
Nakuapia wallah ooo wallah(nakuapia wallah oo wallah)....
Nakuapia wallah ooo wallah(nakuapia wallah oo wallah)....
Nakuapia wallah ooo wallah(nakuapia wallah oo wallah)....
 
Mambo yote tancut almasi orchestra, wana mangala dance-kinye kinye kisonzo. Kalala mbwembwe, john kitime, mapacha kasalo na kyanga songa, kibambe ramadhani, kawelee, father kidevu-abdul salvador. We bwana wacha!
 
Mambo yote tancut almasi orchestra, wana mangala dance-kinye kinye kisonzo. Kalala mbwembwe, john kitime, mapacha kasalo na kyanga songa, kibambe ramadhani, kawelee, father kidevu-abdul salvador. We bwana wacha!
Pia ilikuwepo bendi ya Tancut Almasi,bendi hii ilikuwa inamilikiwa na kiwanda cha kukata almasi kilichokuwa mkoani Iringa na ilikuwa ni mojawapo ya bendi za mikoani zilizokuwa na makali kweli(kama jirani zao wa JKT Mafinga wana Kimulimuli chini ya Zahir Ally Zorro na Kurugenzi ya Arusha).....Tancut Almasi walikuwa wakitumia mtindo wa Fimbo Lugoda na Kinye kinye Kisonzo,tisa kumi Mangala.......

Bendi hii ilitamba na nyimbo kama Samahani ya uongo,Pili wangu,Butinini,Ngoma za Afrika,Helena mtoto wa Arusha,Masikitiko,Lutandila,Safari siyo kifo na nyingine nyingi tu tamu...

Bendi hii iliundwa na wanamuziki kama Kalala Mbwembwe,Nanah Njige,Nuru Mhina,Kawalee Mutimwana,Kyanga Songa,Kasaloo Kyanga,Mafumu Bilali 'Bombenga',Shaban Yohana 'Wanted',John Kitime,Akuliake Saleh 'King Maluu',Ray Mlangwa,Mohammed Shaweji,Kibambe Ramadhan,Bakari Buhero,Abdul Mngatwa,Hashim Kassanga na wengine wengi......Bendi hii ilikuwa na hazina ya vipaji kwa kweli.......

Bendi hii ilitamba sana kabla ya kuanza kusambaratika baada ya wanamuziki wake tegemeo akiwemo Kalala Mbwembwe,Kyanga Songa na Kasaloo Kyanga kuanzisha bendi nyingine hapohapo Iringa ya Ruaha International ambayo ilitamba sana na wimbo wa Lutandila namba 2 Safari (Safari safari safari kweli tabu,naomba kwa Mungu baba nifike salama,safari yangu mieee,safari ya Zimbabweee............ulikuwa wimbo mtamu kweli jamani).....​
 
Bil kuvisahau vibao kama Mama,Tutasele, Mbuguswa na Masafa mrefu...

Hivi mnkumbuka kile kibwagizo cha 'akina mama mwipulikeee,ieeee mwipulikeee........Mbuguswaaaa'

Tunakikumbuka sana kama hivi: Va baaba eeeeeeeeeh, Va maama eeeeeeeeh, ndindindindi (vyombo), mwiplikaaaaaaaaaaaaaaaa.
 
Kitu majirani(huzima redio) toka kwao DDC Mlimani Park Orch. wana Sikinde Ngoma ya Ukae....



Ninapata tabu moyoni mwangu mimi kwa kweli nimekupenda wewe lakini hunijali mamaa..
Tumekuwa sisi wawili kama sinema,hapa nyumbani kwetu kila siku kelele..
Lakini kwa vile ee ee,tunaishi hapa kwa wazazi wako,mwenye sauti ni wewe ee...
Naogopa fedheha mama ooh mie,naona aibu kweli mpenzi,hapa ni kwa wakwe zangu sisemi lolote,fanya upendalo.....

Lakini kwa vile ee ee,tunaishi hapa kwa wazazi wako,mwenye sauti ni wewe ee...
Naogopa fedheha mama ooh mie,naona aibu kweli mpenzi,hapa ni kwa wakwe zangu sisemi lolote,fanya upendalo.....



Chorus: Hata mwezi bado oo ooh,tangu tuoane ee ee,kelele kila siku ndani ya nyumba yetu mamaa....
Hata mwezi bado oo ooh(ooh mama eeh),tangu tuoane ee ee(mama mama mama eeh),kelele kila siku ndani ya nyumba
yetu mamaa.....


Ninaporudi kazini majirani huzima redio ili wasikilize tunachogombana(aibu) wametupachika majina wewe Pwagu na mimi Upwaguzi kwa vile imekuwa ni mazoea ingawa nimekuoa kwa pesa na pendo langu ee,tabia zako zimenishinda,aah nasikitika....

Chorus: Hata mwezi bado oo ooh(ooh mama eeh),tangu tuoane ee ee(tangu tuoane),kelele kila siku ndani ya nyumba yetu
mamaa....ooh mama nasononeka ooh...
Hata mwezi bado oo ooh(ooh mama eeh),tangu tuoane ee ee(mama mama mama eeh),kelele kila siku ndani ya nyumba
yetu mamaa.....


Ninaporudi kazini majirani huzima redio ili wasikilize tunachogombana wametupachika majina wewe Pwagu na mimi Upwaguzi kwa vile imekuwa ni mazoea hajulikani nani mke ndani ya nyumba yetu,hajulikani nani mume aah nasikitika...

Chorus: Hata mwezi bado oo ooh(ooh mama eeh),tangu tuoane ee ee(tangu tuoane),kelele kila siku ndani ya nyumba yetu
mamaa....ooh mama nasononeka ooh... ooh oooh ooooh
Hata mwezi bado oo ooh(ooh mama eeh),tangu tuoane ee ee(tangu tuoane),kelele kila siku ndani ya nyumba yetu
mamaa.... ..

Enjoy...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…