#COVID19 Zimbabwe yarejesha masharti ya kupambana na Corona

#COVID19 Zimbabwe yarejesha masharti ya kupambana na Corona

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Zimbabwe imerejesha marufuku ya kutotoka nje na karantini za lazima kwa wasafiri wote huku kukiwa na ongezeko la visa vya Covid ili kuzuia kuenea kwa aina mpya ya kirusi cha Omicron.

Nchi hiyo imerekodi zaidi ya visa 130,000 vya Covid na takriban vifo 4,700 tangu janga hilo lianze mapema mwaka jana.

Mamlaka ya Zimbabwe iliimarisha masharti ya Covid-19 ikitaja ukosefu wa uwajibikaji upande wa umma na wanaamini kuwa hali itazidi kuwa mbaya zaidi msimu wa sikukuu unapokaribia.

Pia kuna hofu ya wimbi la nne.

Rais Emmerson Mnangagwa alipitisha tena amri ya kutotoka nje kutoka saa tatu usiku hadi saa kumi na mbili asubuhi saa za huko.

Wasafiri wote wa kimataifa watahitajika kupimwa wanapowasili na kuwekwa karantini katika kituo kilichoteuliwa na serikali kwa gharama zao wenyewe.

Biashara zote zitahitajika kufungwa saa moja usiku.

Masharti hayo ni pigo kwa sekta ya utalii, ambayo ilitarajia msimu wa kawaida wa sikukuu.

Hatua hizo zitatathminiwa baada ya wiki mbili.

BBC Swahili
 
Kuna kitu wanasayansi kinawatatiza, hizi lockdowns zinadidimiza sana uchumi na kuleta athari za vijana kukosa ajira. Wananchi wanapaswa kupaza sauti zao kupinga hatua hizi badala yake viongozi wawahamasishe wananchi kuchanjwa ikiwa ni pamoja na kuchukua tahadhari binafsi.
 
kule US wanasema serikali ikiiweka nchi kwenye lockdown kama mwaka jana kuna hatari ya FED kuishiwa mbinu za kupambana na inflation
 
wa ngapi wamekufa leo na kirusi hicho Uingereza?
Waulize kwa nini wanazuia watu kutoka affrica kuingia huko kama wanajiamini?

Au umekurupuka kama wa kukurupuka?
 
Waulize kwa nini wanazuia watu kutoka affrica kuingia huko kama wanajiamini?

Au umekurupuka kama wa kukurupuka?
Uruhusiwe kuingia hata kama hujachanja? wenzetu wanalinda watu wao sababu mtu mmoja kwao ana thamani kubwa sn siyo kama huku tunauliwa kama mbu
 
Back
Top Bottom