ZINDUKA: Hatua za kuchukua Wakala na mteja ili kukabiliana na Utapeli mpya

ZINDUKA: Hatua za kuchukua Wakala na mteja ili kukabiliana na Utapeli mpya

Tomaa Mireni

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2015
Posts
2,395
Reaction score
2,391
Ni siku nyingine tena nakuja kivingine, Natumai mko powa wasomaji.

Leo nataka kuwapa mbinu za kukabiliana na matapeli sababu hawaishi na kila siku wana mbinu mpya.

Kwa sasa mawakala ndio wanaongoza kwa kutapeliwa kupitia wateja wao kivipi? Twende pamoja kwenye makala hii.

Kwanza kabisa kuna utapeli wa aina mbalimbali,wa kwanza tapeli anaweza kujua taarifa au tabia zako kiasi kupitia rafiki yako au ndugu yako na akazitumia kutumiza lengo lake.

Pili matapeli wengi kwa sasa wanajua wengi wa raia hawana pesa nyingi kwenye simu zao kwa hiyo wanawatumia kutapeli mawakala. Huu ndio utapeli 🔥 kwa sasa.



Iko hivi, anaweza kuja mteja wako,jirani yako,mpangaji mwenzako ambaye unamjua vizuri kabisa na huna shaka nae, akiongea na simu akiwa na namba na jina kwenye karatasi akitaka umtumie kiasi fulani cha pesa. Kwa haraka hutakuwa na mashaka nae sababu ni mteja wako(jirani, rafiki) kulingana record zenu za nyuma. Akiwa bado simu iko hewani tapeli akihakikisha hampi nafasi ya kushauriana na wakala kabisa ili asije akashtukiwa.

Miongozo na semina toka kwenye makampuni ya simu ni kwamba
1. Muwekee pesa mteja ambaye yuko na simu yake hapo hapo.
2. POKEA PESA HESABU PESA TUMA PESA. n.k


Sasa hapo utachukua simu na kutuma pesa kwenye namba uliyopesa na mteja wako. Baada kutuma atakwambia kuna hela imetumwa huku kwangu na hapo mtaanza kutoa kwenye simu ya mteja wako sasa. Mtatoa na pesa haitatoka sababu hakuna salio(kumbe ni meseji ya kufoward au ya kawaida) sio ya pesa.

Tapeli anazima simu anawaacha mkigombana wewe na mteja wako sababu.

WAKALA USITUME PESA KABLA HUJAPOKEA PESA(ACHANA NA MAZOEA)

Nina visa zaidi ya vinne nimeshuhudia mwenyewe wateja wawili niliwasaidia mimi na wengine mawakala wapigwa pesa ndefu sana. Nitatoa kimoja kiwe funzo na ushuhuda.

KISA CHA KWELI KWANGU
Alikuja mpangaji mwenzangu akiongea na simu,huyu namjua sana tunakaa nyumba 1 na pesa zake anatumaga kwangu na kutoa kwangu hata kama sina float atanisubiri au atatoa kisha baadae atafata pesa yake, kwa hiyo swala la kuaminiana ni 💯 mimi na yeye. Mazungumzo yalikuwa hivi:

Jirani: braza una salio kwenye voda?
Mimi: kiasi gani?
Jirani: kama 340,000.
Mimi: ndio ipo
Jirani: naomba unitumie kwenye namba hii(ananipa karatasi huku simu yake ikiwa kwenye sikio)
Mimi: naomba hela nihesabu kabisa.
Jirani: nakupa ipo kwenye simu hii naongea nayo.
Mimi: kata simu kwanza(nahitaji ufafanuzi zaidi)
Jirani: hapana huyu jamaa naongea naye kasema nisikate simu mpaka hela itumwe.
Mimi: nikashtuka kidogo!! Nikauliza ni nani?
Jirani: labda uongee nae(akanipa simu)
Mimi: mambo vip?
Simu: safi nsugu yangu,anatoa maelezo marefu ya kukosea muamala ukaja kwa jirani yangu kiasi cha 390,000 lakini akitaka kurudiahiwa 340,000 tu hiyo 50k ni ya usumbufu.
Mimi: kwanini asikurudishie kupitia simu hii hii bila kutumia wakala?
Simu: hapana kaka,ukitumiwa pesa na kurudisha kwa namba iliyotuma huwa inachelewa kufika ndio maana nataka itumwe kwa wakala moja kwa moja kisa yeye atoe hapo kwako, nisadie ndugu yangu.
Nikampa jirani simu nikamwambia kata hiyo simu. Akadai ameambiwa asikate mpaka hela itumwe (kwa kitisho cha kublokiwa namba na kutafutwa popote alipo).

Mimi: KATA SIMU HIYO. Kweli akakata simu na nikwambia huyo tapeli kama ni kweli basi tutoe hiyo hela ikitoka tumtumie. Ukweli hakua na hela ila msg ya kutimwa lakini sender ni namba ya kawaida imeseviwa M-PESA.

Jirani yangu hakuamini,kesho alikuja kunishukuru sana na kusema kama ningetuma angelipaje? Hakulala usingizi akijiuliza maswali tu.

MWISHO.
Kama ningechukulia poa kwamba "huyu namjua ngoja nitume tu" nani angepata hasara? Ni jirani yangu lakini sikutumia mazoea,nilitimia kanuni za kazi.

Ndugu wasomaji kuweni makini mnapoona fursa ya haraka isiyotumia nguvu kubwa,wala muda kuipata. Huenda ikawa wewe ndio fursa yenyewe.

ASANTENI. Kama umepata elimu kidogo kupita makala hii sio mbaya ukanipa kura yako.
 
Ni siku nyingine tena nakuja kivingine, Natumai mko powa wasomaji.

Leo nataka kuwapa mbinu za kukabiliana na matapeli sababu hawaishi na kila siku wana mbinu mpya.

Kwa sasa mawakala ndio wanaongoza kwa kutapeliwa kupitia wateja wao kivipi? Twende pamoja kwenye makala hii.

Kwanza kabisa kuna utapeli wa aina mbalimbali,wa kwanza tapeli anaweza kujua taarifa au tabia zako kiasi kupitia rafiki yako au ndugu yako na akazitumia kutumiza lengo lake.

Pili matapeli wengi kwa sasa wanajua wengi wa raia hawana pesa nyingi kwenye simu zao kwa hiyo wanawatumia kutapeli mawakala. Huu ndio utapeli [emoji91] kwa sasa.



Iko hivi, anaweza kuja mteja wako,jirani yako,mpangaji mwenzako ambaye unamjua vizuri kabisa na huna shaka nae, akiongea na simu akiwa na namba na jina kwenye karatasi akitaka umtumie kiasi fulani cha pesa. Kwa haraka hutakuwa na mashaka nae sababu ni mteja wako(jirani, rafiki) kulingana record zenu za nyuma. Akiwa bado simu iko hewani tapeli akihakikisha hampi nafasi ya kushauriana na wakala kabisa ili asije akashtukiwa.

Miongozo na semina toka kwenye makampuni ya simu ni kwamba
1. Muwekee pesa mteja ambaye yuko na simu yake hapo hapo.
2. POKEA PESA HESABU PESA TUMA PESA. n.k


Sasa hapo utachukua simu na kutuma pesa kwenye namba uliyopesa na mteja wako. Baada kutuma atakwambia kuna hela imetumwa huku kwangu na hapo mtaanza kutoa kwenye simu ya mteja wako sasa. Mtatoa na pesa haitatoka sababu hakuna salio(kumbe ni meseji ya kufoward au ya kawaida) sio ya pesa.

Tapeli anazima simu anawaacha mkigombana wewe na mteja wako sababu.

WAKALA USITUME PESA KABLA HUJAPOKEA PESA(ACHANA NA MAZOEA)

Nina visa zaidi ya vinne nimeshuhudia mwenyewe wateja wawili niliwasaidia mimi na wengine mawakala wapigwa pesa ndefu sana. Nitatoa kimoja kiwe funzo na ushuhuda.

KISA CHA KWELI KWANGU
Alikuja mpangaji mwenzangu akiongea na simu,huyu namjua sana tunakaa nyumba 1 na pesa zake anatumaga kwangu na kutoa kwangu hata kama sina float atanisubiri au atatoa kisha baadae atafata pesa yake, kwa hiyo swala la kuaminiana ni [emoji817] mimi na yeye. Mazungumzo yalikuwa hivi:

Jirani: braza una salio kwenye voda?
Mimi: kiasi gani?
Jirani: kama 340,000.
Mimi: ndio ipo
Jirani: naomba unitumie kwenye namba hii(ananipa karatasi huku simu yake ikiwa kwenye sikio)
Mimi: naomba hela nihesabu kabisa.
Jirani: nakupa ipo kwenye simu hii naongea nayo.
Mimi: kata simu kwanza(nahitaji ufafanuzi zaidi)
Jirani: hapana huyu jamaa naongea naye kasema nisikate simu mpaka hela itumwe.
Mimi: nikashtuka kidogo!! Nikauliza ni nani?
Jirani: labda uongee nae(akanipa simu)
Mimi: mambo vip?
Simu: safi nsugu yangu,anatoa maelezo marefu ya kukosea muamala ukaja kwa jirani yangu kiasi cha 390,000 lakini akitaka kurudiahiwa 340,000 tu hiyo 50k ni ya usumbufu.
Mimi: kwanini asikurudishie kupitia simu hii hii bila kutumia wakala?
Simu: hapana kaka,ukitumiwa pesa na kurudisha kwa namba iliyotuma huwa inachelewa kufika ndio maana nataka itumwe kwa wakala moja kwa moja kisa yeye atoe hapo kwako, nisadie ndugu yangu.
Nikampa jirani simu nikamwambia kata hiyo simu. Akadai ameambiwa asikate mpaka hela itumwe (kwa kitisho cha kublokiwa namba na kutafutwa popote alipo).

Mimi: KATA SIMU HIYO. Kweli akakata simu na nikwambia huyo tapeli kama ni kweli basi tutoe hiyo hela ikitoka tumtumie. Ukweli hakua na hela ila msg ya kutimwa lakini sender ni namba ya kawaida imeseviwa M-PESA.

Jirani yangu hakuamini,kesho alikuja kunishukuru sana na kusema kama ningetuma angelipaje? Hakulala usingizi akijiuliza maswali tu.

MWISHO.
Kama ningechukulia poa kwamba "huyu namjua ngoja nitume tu" nani angepata hasara? Ni jirani yangu lakini sikutumia mazoea,nilitimia kanuni za kazi.

Ndugu wasomaji kuweni makini mnapoona fursa ya haraka isiyotumia nguvu kubwa,wala muda kuipata. Huenda ikawa wewe ndio fursa yenyewe.

ASANTENI. Kama umepata elimu kidogo kupita makala hii sio mbaya ukanipa kura yako.
Au ulikuepo eneo la tukio mzee mana nimemfungulia mama koku kiofisi cha uwaka kifremu cha home sasa wife katoka nikamshikia akaja mteja kama hivyo jirani anaongea na simu na karatasi yake ya namba na jina nimuwekee 358000 si mteja nikamuwekea bila kujiuliza, mmmmh kumbe anaongea na tapeli nasubiri pesa naona kaganda tu nikashtuka palepale kupiga customer care ila ishatoka, mmmmh nikasema hapa tukienda police tutalipana mwaka mzima nikavaa sura ya kazi nikamfungia ndani hapa hutoki hadi pesa akapigia ndugu jamaa na marafiki usiku ikapatikana laki tatu,nikasema angalau iliyobaki nikaweka upole kidogo ikalipwa baada ya siku mbili tatu,kweli mkuu TUONDOE MAZOEA sehemu zetu zote tuwapo.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] Kuna Jamaa mmoja alitepiliwa mwaka Jana laki Moja Kwa mbinu hii, teh teh hapa Mbeya
 
mi kalinipigia kadada sauti nzuuuri kwel kweli kakawa kanijiliza et kakosea kutuma pesa naomba nimrudishie kidogo nimtumie,niimuuliza maswali manne akashindwa kuyajibu
 
Au ulikuepo eneo la tukio mzee mana nimemfungulia mama koku kiofisi cha uwaka kifremu cha home sasa wife katoka nikamshikia akaja mteja kama hivyo jirani anaongea na simu na karatasi yake ya namba na jina nimuwekee 358000 si mteja nikamuwekea bila kujiuliza, mmmmh kumbe anaongea na tapeli nasubiri pesa naona kaganda tu nikashtuka palepale kupiga customer care ila ishatoka, mmmmh nikasema hapa tukienda police tutalipana mwaka mzima nikavaa sura ya kazi nikamfungia ndani hapa hutoki hadi pesa akapigia ndugu jamaa na marafiki usiku ikapatikana laki tatu,nikasema angalau iliyobaki nikaweka upole kidogo ikalipwa baada ya siku mbili tatu,kweli mkuu TUONDOE MAZOEA sehemu zetu zote tuwapo.
Katika matukio manne niliotaka moja alikuja mdada kwa style hiyo wa jiran tu,akataka nitume 360,000 nikamwambia sina float (wakati huo tapeli anasikia ninavyomjibu) akaniambia una kiasi gani nianze na hicho nikamwambia nina 20,000 tu. Akaambiwa tuma hiyo hiyo.

Nikamwambia si ukate simu,akasingizia anaongea na kakake,nikamuuliza unaweka kwako au unamtumia mtu? Akajibu anaweka kwake,mm nikatoa hofu sababu kasema ni kakake afu pia 20k sio nyingi.

Nikatuma 20k nikamwambia tayari,simu ikakatwa chap. Nikamwambia naomba hela akasema hajaona msg,nikamwonyesha yangu,akapiga tena simu haipatikani,akapagawa!! Nikamuuliza umeweka kwako au ulikuwa unamtumia mtu?(maelezo marefu) kakake alitaka amtumie hela ikifika yeye atamtumia muda huo huo(kiasi kingi kuzidi ambacho angemtumia).

Nikashtuka tayari katapeliwa,nikamwambia kwa hiyo tunafanyaje? Hana cha kusema kapagawa,nikamwambia kama ningetuma ile 360k ingekuwaje? Hana jibu,nikaingiza ndani nikakaa mlangoni nikamwambia apige ndugu zake warudishe hiyo hela bila hivyo hatotoka hapo.

Akawatafuta ndugu zake lakini akaambilia 10k tu. Nikamwambia acha mkoba na simu ukatafute hiyo 10k ingine,akaja rafiki yake na 10k kukomboa vitu vyake.

Kwa huruma nilimwonesha hakuamini mpaka leo huwa ananiheshimu sana na akasema nilimsitiri sababu angekuwa hajulikani angeitiwa mwizi na kudhalishwa.

Matukio ni mengi mno,afu maumivu wanapata mawakala zaidi.
 
nangwanda mimi ni wakala boss kwa hiyo hayo matukio nayajua vizuri kabisa
Yule dogo anapita ananiamkia tu shikamoo brother,bila kumvalia sura ya kazi ilikua inapotea 358000 au nilipwe ten ten,siku brother wake kaja kumaliza 38000 anatia huruma kidogo nimsamehe lkn nikasema nimetumwa pesa watoto waende chooni
 
Yule dogo anapita ananiamkia tu shikamoo brother,bila kumvalia sura ya kazi ilikua inapotea 358000 au nilipwe ten ten,siku brother wake kaja kumaliza 38000 anatia huruma kidogo nimsamehe lkn nikasema nimetumwa pesa watoto waende chooni
Duuu hapo kwenye waende chooni sasa. Ila kwa kwel umakini unahitajika wa hali ya juu
 
Watu wanapigwa sana asee. Sijui hii kitu itaisha lini tu.
 
Yule dogo anapita ananiamkia tu shikamoo brother,bila kumvalia sura ya kazi ilikua inapotea 358000 au nilipwe ten ten,siku brother wake kaja kumaliza 38000 anatia huruma kidogo nimsamehe lkn nikasema nimetumwa pesa watoto waende chooni
Kabisa mkuu,usiangalie sura kabisa hata kama mnalala wote
 
Hivi kile kitengo cha cyber crime kule police huwa wanaweza kuwa trace na kuwakamata hawa matapeli ?
Wale ni ngumu sana kuwa trace sababu wanatumia simu nyingi na hawakai nazo muda mrefu hewani. Ndiomana wakikamatwa wanakuwa na laini hata 60 na simu kibao sasa utawa trace vipi?
 
Back
Top Bottom