Zipi Gharama za kujifungua mama mjamzito hospitali za serikali?

Zipi Gharama za kujifungua mama mjamzito hospitali za serikali?

Bigsteve

Member
Joined
Nov 23, 2017
Posts
37
Reaction score
59
Wakuu habari za mchana?
Natumaini mko sawa na mishe kama kawa zinasogea.
Nimebahatika kupata mwanamke mzuri ambae mpaka ninapoandika uzi huu ni mjamzito na mungu akijaalia mwezi ujao tunatarajia kupata mtoto.
Kulingana na hali ya uchumi nimeona ni vyema kujiandaa financially mapema atleast nijue ni kiasi gani kinaweza kutosha kulipa gharama katika hospitali za Serikali?
Wenye uzoefu naomba msaada na mawazo katika jambo hili.Asanteni
 
Kujifungua kama ni government bure labda vifaa tu uwenavyo, ila kama ni private andaa pesa na ujauzito ni kipindi ambacho unatakiwa kujiandaa kiuchumi kidogo ndomana tunashauriwa hata sie mahospital tuwe tuweka vijiakiba maana chochote kinaeza kutokea kimatumizi,
 
Ni kuwa na vifaa vyake vya kujifungulia tu! Gharama yake haizidi 50,000
Hivi vifaa unavosema so ndio vile kwenye tangazo lao LA TV, wanasema vinatolewa bure kwa kila mama mjamzito wakati Wa kujifungua!? Na nimarufuku kuuziwa! Kiufupi Huduma za kujifungua ni bure, utacholipia ni malazi na complication zozote zitazotokea za kimatibabu.

Lakini kama wanavosemaga damu haiuzwi, ila unapokuwa na Shida ndo utajua inauzwa? au inabidi uwe na hela ndo uipate!
 
Hivi vifaa unavosema so ndio vile kwenye tangazo lao LA TV, wanasema vinatolewa bure kwa kila mama mjamzito wakati Wa kujifungua!? Na nimarufuku kuuziwa! Kiufupi Huduma za kujifungua ni bure, utacholipia ni malazi na complication zozote zitazotokea za kimatibabu.

Lakini kama wanavosemaga damu haiuzwi, ila unapokuwa na Shida ndo utajua inauzwa? au inabidi uwe na hela ndo uipate!
Sasa we siku nenda na mkeo uwaambie vifaa bure uone kama hujatukanwa wewe mkeo na hicho kilicho tumboni (kiukweli manesi wanatukana sana)
 
Hivi vifaa unavosema so ndio vile kwenye tangazo lao LA TV, wanasema vinatolewa bure kwa kila mama mjamzito wakati Wa kujifungua!? Na nimarufuku kuuziwa! Kiufupi Huduma za kujifungua ni bure, utacholipia ni malazi na complication zozote zitazotokea za kimatibabu.

Lakini kama wanavosemaga damu haiuzwi, ila unapokuwa na Shida ndo utajua inauzwa? au inabidi uwe na hela ndo uipate!
Hivyo vifaa ni kwa ajili ya kurahisisha huduma ukisubiri vya bure utaambulia matusi. Vifaa vyenyewe ni pamba, mpira, chupa ya spirit, pair of gloves pamoja na ile dawa. Ukingoja vya bure mara utaambiwa vimekwisha au mwenye funguo ya stoo hayupo tena wakati huo mkeo ndio muda umefika wa kujifungua, jenga picha je ukiwa na vifaa vyako?
 
Hivi vifaa unavosema so ndio vile kwenye tangazo lao LA TV, wanasema vinatolewa bure kwa kila mama mjamzito wakati Wa kujifungua!? Na nimarufuku kuuziwa! Kiufupi Huduma za kujifungua ni bure, utacholipia ni malazi na complication zozote zitazotokea za kimatibabu.

Lakini kama wanavosemaga damu haiuzwi, ila unapokuwa na Shida ndo utajua inauzwa? au inabidi uwe na hela ndo uipate!
Achana na hospital za serikali, mi kuna siku muhimbili nliambiwa hamna tissue ya kunifutia jelly kwenye kipimo cha ultrasound, niende nikatafute ndio nirudi kupima, tissue inafanya mtu ukose kipimo!!
Heri aende tu na vifaa vyake kwa usalama zaidi
 
Then watu wanaona hospitali zilizopo mjini ndio mpango mzima, lakini kwangu ni tofauti.
Nawasifu sana wauguzi wote na madaktari wa Hospitali ya Pugu kama wamo humu naomba wapokee pongezi zangu. Hawana maringo, hawakashifu wagonjwa, hawasimbulii, wala hawanyanyasi wagonjwa na wanajali utu.
 
Hivi wanakuwaga na maana gani, wanaposema Huduma Fulani ni bure!? Wakati kiuhalisia hawana uwezo Wa kutoa bure na kwa ufanisi!!? Siku moja nilienda agha khan Dodoma na kadi ya bima, nikawa na malaria, kufika kwenye dawa eti "dawa official ya malaria inayotolewa na bima ya afya ni dawa mseto" ambayo wenyewe wameishiwa, walionayo haihusian na bima ya afya! Hivo niinunue cash! Wakanipa panadol za kopo, nikawauliza "hizi expayer date yake ni lini?? Ikabidi wanibadilishie wanipe za blister.
 
Huduma ya kujifungua kwenye hospitali ya serikali ni bure, jiandae tu kwa yale mahitaji basic!
 
Huna bima mkuu!? Ungetaja na mkoa uliopo ili kama kuna wajuzi wakupe coordinates za kituo kizuri na gharama zake. Vituo vya afya vingi vipo poa tu, sema kwa emergency cases za uzazi ni bora uwe katika vituo vikubwa maana hawachelewi kukuambia ambulance mbovu na wakati kishanuka.
 
Back
Top Bottom