Nakuunga mkonoKigogo ni mku.ndu tu yule, serikali na vyombo vyake vyote wameshindwa hata kumbaini kweli? Wambaini anaishi wapi watoe mpunga wa maana hata kama anaishi nje ya nchi sie wengine hata kujitoa mhanga siyo tatizo.Unamfumua mtu hata nikifia jela nchi nyingine poa tu
Mnataka muendelee kuachwa muongee nyie peke yenu? Kina Katambi, Kafulila, Waitala, Lijualikali ..... Siku hizi sio wanasiasa uchwara? Unataka tuendelee kugokewa na kina Polepole?Jana nilimuona Abdul Nondo akiongea kwenye media kwa mtindo wa "kufoka foka" huku dada aliyekuwa pembeni akimuangalia kwa mshangao....
Drama za wanasiasa njaa wa enzi za JK zimeanza kurudi kwa mbali!
Kigoma kuna Makabila mengi, Kuna Waha ambao ndiyo kabila kubwa lakini pia kuna Wabembe, Wabwali, Wagoma, Walagarasi na wasukuma (pembezoni)ZIto na kigogo yao mamoja. Asijibalaguze bila sababu kwanza uraia wake ni wa mashaka kuliko Mpango. Hakuna Muha anayeitwa Kabwe!
Hoja ya uraia ni mbaya sana. CCM wanaitumia sana kuumiza watu.Zito anaweza akawa na hoja kwenye kumlinda Mpango, lakini asitumie ukigoma kumlinda Mpango,
Wanahoji uraia wa Dk Mpango hawahoji kwa ajili ya kigoma. Wanahoji kwa ajili ya Taifa. Yaani Zito anaanza kukopi kwa JPM alivyoliharibu Taifa kwa kutengeneza ukanda...
Andika wewe vitu vya maana..kwa Nini nyie mnaojiita wakongwe mna mbwembwe Sana..mnafikiri msipochangia kwenye mijadala ya JF hakuna la maana litakalojadiliwa.JF, siku hizi ndiyo maana wakongwe wanachugulia na kuondoka bila kuchangia chochote, uzi kama huu kweli utapata wapi watu makini wa kuchangia labda wazee wa mipasho.
Ni kweli, But, Zito angeweza kumtetea Dk Mpango bila kuhusishwa na Kigoma. Nyerere alitengeneza Tanzania kua kitu kimoja. Ndio maana hata wanaohoji hawasemi kwa nini anapewa umakamu wa Raisi anayetokea Kigoma.Hoja ya uraia ni mbaya sana. CCM wanaitumia sana kuumiza watu.
Sasa cha kushangaza hata wanaojifanya watetezi nao wanapita njia ile ile. Na waathirika wakubwa ni watu wa mipakani haswa wanaojihusisha na siasa.
Kwa nini wachaga,wapare,wamasai hawanyanyapaliwi kama waha? Licha ya kuwa karibu na Kenya. Waha ili wasafiri kwenda sehemu yoyote TZ wanatakiwa wawe na barua ya mwenyekiti au kitambukisho.Watu wa mikoa ya pembezoni huwa wananyanyapaliwa sana kwa kubambikiwa uraia wa nchi jirani.
Zitto yuko sahihi kukasirika
VP hana maamuzi yoyote katika maamuzi ya rais anachoweza kufanya ni kushauri tu hivyo mtulize vihere here huko mipakani.VP haweza kujieleza kwa upumbavu wenu. Tatizo huyo Kigogo hata hajui lolote kuhusu Waha na lugha yao! Kile ni kiha nanile ni ngoma ya kiha, yes huu ni muda wa Waha kaeni lwa kutulia.
Acheni kupanic kama nguruwe pori...VP haitaji kutetewa kiivyo mi suala la yeye kutoka hadharani na kuulezea umma asili yake hasa ni ipi, Anaongoza taifa lenye makabila 120 tanznia nzima, haongozi tu watu wa kigoma.Acha umbayuwayu VP ajieleze kwa huo uzumbukuku wenu.?? Mtakuwa mmekosa agenda!
Tatizo kubwa ni kwamba Kigoma ni wahanga wakubwa mnoo wa hilo suala kutoka a na misimamo ya siasa zao ikifuatia Kagera. Nambie ninmkoa gani wanaopitia hali kubwa kama hiiNi kweli, But, Zito angeweza kumtetea Dk Mpango bila kuhusishwa na Kigoma. Nyerere alitengeneza Tanzania kua kitu kimoja. Ndio maana hata wanaohoji hawasemi kwa nini anapewa umakamu wa Raisi anayetokea Kigoma.
Zito ni public figure asingekua anasema hadharani kua sisi wa Kigoma tutamlinda Dk Mpango. Dk Mpango atalindwa na Tanzania na sio Kigoma.
Kwa nini wseme sasa, kisa tu kawa makamu.Namuunga mkono Zitto Kabwe.
Haya mambo yakienda hivi hata Mbowe mtasema siyo mtanzania ni mmalawi!
Kwani Sheria mama inasemaje??Namuunga mkono Zitto Kabwe.
Haya mambo yakienda hivi hata Mbowe mtasema siyo mtanzania ni mmalawi!
Ila ukumbuke na historia ya Kigoma ni mkoa uliolea wakimbizi kwa muda mrefu, ko kua na wakazi ambao sio raia wa Tanzania ni jambo la kawaida.Tatizo kubwa ni kwamba Kigoma ni wahanga wakubwa mnoo wa hilo suala kutoka a na misimamo ya siasa zao ikifuatia Kagera. Nambie ninmkoa gani wanaopitia hali kubwa kama hii
Unajua kuwa mkuu wa idara wa halmashauri tu.. unapitia vetting kiasi gani!?Acheni kupanic kama nguruwe pori...VP haitaji kutetewa kiivyo mi suala la yeye kutoka hadharani na kuulezea umma asili yake hasa ni ipi, Anaongoza taifa lenye makabila 120 tanznia nzima, haongozi tu watu wa kigoma.
Tanzania hatujawahi kufanya serious operation ya kufukuza watu. Kwanza Tanzania ya Nyerere ilikuwa inaamini kwenye Pan Africanism, imelea na kutoa passport kibao tu kea watu wasio raia.Ila ukumbuke na historia ya Kigoma ni mkoa uliolea wakimbizi kwa muda mrefu, ko kua na wakazi ambao sio raia wa Tanzania ni jambo la kawaida.
Kule Kigoma abiria wanakaguliwa uraia kwenye mabasi jambo ambalo ni nadra kukuta kwenye mikoa mingine. Kuhoji uraia ni jambo la kawaida. Lisifanye kuugawa utanzania, Tuipiganie Tanzania sio makabili.
Target yake Jiwe hayupo tenaSure,these few days amekuwa kama mtoto wa chekechea.
Tena manyovu!! mpaka unao tenganisha Manyovu na Burundi ni kijito kinacho tiririka maji safi kidogo kuliko mto ng'ombe pale kjtnyma DSM kipindi cha kiangazi! Wakazi wa hapo wanalima Burundi na hujipatia mahitaji yao huko.Wewe ni Muha? Kufanya kazi kambini pekee hakukupi fursa ya kuwajua waha/warundi. Mimi ni Muha na nafanya kazi kambini (RSC) nawajua Waha, Warundi, Wasubi, Wanyarwanda ma Wahangaza na tamaduni zao. Pale alipokuwa VP ni Manyovu katika kipindi cha kampeni, ni mpakani na Burundi na kuna wenyeji (ambao ndo unawaona wanaimba) hakuna kiashiria chochote cha urundi kwa watu wale maana zile nyimbo ni za Kiha na wamevaa nguo za CCM (sidhani kama CCM wana tawi Burundi)
Hana USAHIHI wowote ni MNAFIKI TU kama anapigania hill Mbona Kabendera na Yule ASKOFU walipoambiwa Sio RAIA hakuibuka Kuwatetea?Watu wa mikoa ya pembezoni huwa wananyanyapaliwa sana kwa kubambikiwa uraia wa nchi jirani.
Zitto yuko sahihi kukasirika