Zitto Kabwe: Kwaheri John Magufuli, Buriani Tingatinga

Zitto alikuwa na matumaini makubwa ya kuteuliwa katika zile nafasi 10 za rais.

Huu msiba umemstua sana alijaribu kutaka maridhiano kama yaliyofanyika Zanzibar baina ya ACT na CCM
 
MAGUFULI AMEACHA ALAMA KWA WATANZANIA.

Nyie mnalilia njaa tu, vigeugeu sana. Mmewachanganya watanzania kwa kukosa ushirikiano baina yenu wapinzani, mnajenga nyumba moja ila mnagombania fito!
Alama gani?
 
Zitto badala ya kuhoji kwanini upinzani hamjapewa nafasi kwenye mazishi ya JPM hata ya kuweka shada kama wapinzani sembuse kuongea, wewe unabaki kuabudu na kusifu kama team LUMUMBA. Hii ina saidia nini wakati bado hatuoni demkrasia ikitamalak?

Haya maombolezo na mazishi hayakuwa ya CCM pekee bali ni kwa Watanzania wote..

Zitto amka!!!!
 
Akina Absalom Kibanda kupigwa, akina Dr. Ulimboka kung'olewa meno, yule mwandishi wa habari wa Iringa aliyepigwa bomu na polisi, akina kubenea waliomwagiwa Tindikali, n.k, n.k, mabomu ya Olasiti, yoye hayo yalitokea zama kabla ya utawala wa Magufuli.

Chuki yote dhidi ya Magufuli ni kwa vile aliziba mirija yote ya wanasiasa wajanja wajanja, wanaotumia kuongea kama mtaji. Kwao kuongea ndio demokrasia, na ulipokuja utawala unaotaka kazi na matokeo, badala ya kelele na uanaharakati, eti hiyo sio demokrasia.

Sometimes (oftentimes) demokrasia ni kichaka cha uvivu na utapeli, na sidhani kama nchi kama zetu zinahitaji demokrasia ya aina hiyo.
 
Ile katiba mpya ilishatekwa, ni bora ilivyovurugika.
 
Zitto umeongea yaliyo katika muktadha wako kuyaongea, lkn uhalisia si huo.

Nikutahadhalishe tu km ambavyo JPM aliwahi kumjibu mwandishi wa reuters pale Kampala alivyozuru Uganda 2016 shortly...

'' its either you choose human rights (democracy) or corruption"
 
Dunia iko kwa ajili ya wale wanaotaka kuishi ndani yake
Ahsante kwa tanzia nzuri uwe na maisha mema
 
Zito ulishafilisika kisiasa siku nyingi. Kwa hili uliloandika umejizika kabisa. Umetulazimisha tukuchukie. Huwezi kuamua kumchafua marehemu Dr Magufuli halafu ukabaki salama. Wote tulikuwa hapa hapa Tanzania huwezi kutudanganya! Kawadanganye mabeberu wafadhili wako!! Umeandika uchafu na wewe ni mchafu Sana!!
 
Umeandika vizuri sana ingawa ngumu kwa MATAGA kumeza ....tujenge taasisi sio personality MTU mmoja ....tupambane katiba ibadilisgwe yeye alitaka legacy tu hakuna lingine alijua muda nfupi SAA yake itazima alitaka atomize ndoto yake kysaidia jamii haraka haraka bila kuulizwa wala kucheleweshwa na demokrasia ....akaamua kusigina katiba alivyotaka akijua kwa nini .....issue ni muda ! Hakuwa na huo muda wa kusubiri mchakato betri yake ilikuwa inaisha kila sekunde ipitayo .....@ ZZK Tanzia yako ataandika Sheikh Said kama akiwa hai Ana LA basi swahiba JM atasaidia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…