Zitto Kabwe: Sherehe za Mapinduzi za leo ndiyo za mwisho kwa Rais Magufuli ambaye anamaliza muda wake wa Urais Oktoba mwaka huu

Zitto Kabwe: Sherehe za Mapinduzi za leo ndiyo za mwisho kwa Rais Magufuli ambaye anamaliza muda wake wa Urais Oktoba mwaka huu

M-mbabe

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2009
Posts
13,203
Reaction score
23,027
Kichwa cha uzi kinajieleza chenyewe.

Si kauli yangu bali ni ya mwanasiasa machachari kabisa mh Zitto ambayo kaitoa leo kupitia ujumbe wake wa twitter akimjibu JPM kuhusu kuhusika kwa TISS katika utekaji.

Ni kauli nzito ambayo inahitaji mikakati mizito sana kivitendo (NEC huru, nk) ili azma yake ifikiwe. Vyama vya siasa na taasisi huru zianze mikakati mapema maana 2020 yenyewe ndiyo hii.

CC Zitto, John Mnyika, nk, nk


 
ZZK almaarufu Ayatollah ana wenge sana baada ya tathmini ya chama kuonesha chama kina bendera nyingi kuliko wanachama.
Kwani Zitto kakosea wapi kwenye hili?

Uchaguzi upo Oktoba 2020 na lolote linaweza kutokea ukizingatia huku ndani ya CCM yetu kuna mpasuko wa kufa mtu.... ninyi mlioko huko nje hamjui tu!
 
Acha kujifanya mtu wa system wakati mkata nyasi tu wa ngombe wa mh Paul makonda
kwani Zitto kakosea wapi kwenye hili?

uchaguzi upo October 2020 na lolote linaweza kutokea ukizingatia huku ndani ya CCM yetu kuna mpasuko wa kufa mtu.... ninyi mlioko huko nje hamjui tu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mh. Zito ni mwanasiasa, na ametoa kauli ya kisiasa kuonyesha matamanio yake katka ulingo wa kisiasa katika uchaguzi utakaofanyika mwaka huu. Kauli yake imejaa ukweli kabisa kwa kuwa Rais aliyepo madarakani anamalizia kipindi chake kutokana na matakwa ya kikatiba.

Na ili apate kuwa tena Rais mteule wa baada ya uchaguzi kwa kipindi kijacho na kisha kuapishwa tena kuwa Rais wa JMT hana budi kufikia vigezo vifuatavyo;
1. Apitishwe tena na chama chake kugombea nafasi hiyo
2. Ashinde kupitia mchakato wa upigaji kura kwa kushindanishwa na wagombea kutoka vyama vingine vya ushindani
3. Ithibitike kuwa ana akili timamu na mwenye afya isiyotia shaka
4. Mpaka siku ya uchaguzi ajaliwe kuwa hai kwa kadiri Mwenyezi Mungu atakavyo na kwa mapenzi yake Yeye mwenyewe tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ZZK almaarufu Ayatollah ana wenge sana baada ya tathmini ya chama kuonesha chama kina bendera nyingi kuliko wanachama.
Hiyo haiondoi ukweli wa kauli yake. Its true JPM hizi ni sherehe zake za mwisho kama presidaa.
Msimdanganye, maana yeye mwenyewe na mwawaziri wake, Wakuu wastaafu na viongozi waandamizi wa chama chake wanalijua hilo. Kuwa hii vita ta kupata Tume huru ikikamilika tuu basi mzee ajaze masanduku na mabegi yake kwenye ATCL Airbus kutanguliza nyumbani tuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom