Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Kiongozi wa cha chama cha ACT-Wazalendo taifa Zitto Kabwe amesema endapo wananchi wa mkoa wa Katavi watawachagua viongozi wa upinzani watahakikisha wanaletea mabadiliko katiko sekta ya afya, maji na elimu.
Ameyasema hayo alipokua akizungumza na wananchi wa manispaa ya Mpanda katika uwanja wa Sikonge na kusema kuwa a endapo watapata ridhaa upinzani watahakikisha wanatatua kero za wakulima sambamba na kuboresha maisha ya watanzania.
Aidha, amewaomba wananchi wa jimbo la Mpanda mjini kumchagua mgombea ubunge kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Rhoda Kunchela na kusema kuwa wao kama vyama upinzani wameona ni vyema kusimamisha wagombea wanaoweza kumshinda mgombea wa CCM.
Akizungumzia nafasi ya urais kiongozi huyo amesema viongozi wa upinzani wamekaa kwa pamoja na kuona ni vyema kumsimamisha mgombea urais kupitia chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Tundu Lissu.
Chanzo: Mpanda Radio
Ameyasema hayo alipokua akizungumza na wananchi wa manispaa ya Mpanda katika uwanja wa Sikonge na kusema kuwa a endapo watapata ridhaa upinzani watahakikisha wanatatua kero za wakulima sambamba na kuboresha maisha ya watanzania.
Aidha, amewaomba wananchi wa jimbo la Mpanda mjini kumchagua mgombea ubunge kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Rhoda Kunchela na kusema kuwa wao kama vyama upinzani wameona ni vyema kusimamisha wagombea wanaoweza kumshinda mgombea wa CCM.
Akizungumzia nafasi ya urais kiongozi huyo amesema viongozi wa upinzani wamekaa kwa pamoja na kuona ni vyema kumsimamisha mgombea urais kupitia chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Tundu Lissu.
Chanzo: Mpanda Radio