Uchaguzi 2020 Zitto Zuberi Kabwe: Watanzania hawatatusamehe tusipokuwa na mgombea mmoja wa Urais, mgombea mmoja kila Jimbo na kila Kata

Watanzania hawatatusamehe tusipokuwa na mgombea mmoja wa Urais, mgombea mmoja kila Jimbo,na kila Kata,
Zitto kalijua leo suala hili? Mbona 2015 yy alikataa? Aanhe ushakunaku. Chadema lindeni maslahi mapana ya nchi.
 

Hiyo ya kupanda jukwaa moja Act na CDM italeta hamasa kwa raia...
 
Hiyo ya kupanda jukwaa moja Act na CDM italeta hamasa kwa raia...

Hilo halikubaliki kisheria kama hamjaungana. Kwa sasa hilo haliwezekani. Kinachowezekana kwa sasa ni kuachiana majimbo bila vyama kushare jukwaa moja.
 
Tangu lini jamaa analipenda Taifa hili.

Alisema tuna Korona.

Akawa anapiga kampeni tunyimwe fedha za World Bank.

Huu upendo wa dhati kwetu umekuja kipindi anataka kura sio??
World bank sio mabeberu?
 
Basi aonesha mfano kwa kutokusimamisha wagombea katika nafasi ya urais na Wabunge na madiwani au kwa sababu anaona inafaa ndo maana anataka?Mbona 2015 alisimama peke yake?
 
Hapo namtetea Zitto, yeye ndiye aliyekataliwa na Chadema kwa sababu ya usaliti siyo kwamba yeye ndiye aliyewakataa.
Sikumbuki vzr Ila nakumbuka Kuna Maneno flani aliyatoa kipindi like akiwananga walioungana. Kama una ushahidi nikumbushe juu ya Hilo
 
Zitto alishalijibu hili kwamba Chadema na ukawa ndiyo waliomtenga hawakutaka kabisa washirikiane naye.
Ok.unadhani au Unajua kwanini wamkatae? Siri yao Mimi sijui,Kuna dhambi ukizifanya hii Dunia hata ndugu zako ukiwakaribia hawakuamini.
 
Huyo siyo opportunist ila ni ‘KIPYOTO’ (mchavuzi, mkorogagi) of which atarudi kundini kama kawaida!
CHADEMA kwasasa ni kama kibinti cha miaka 18-21 kiko kwenye peak hata kikiitwa nyodo kibao.

Ila siku ikibuma, mtatafuta ushirikiano hata na SAU nao watawakataa.
 
Zitto ana unafiki ndani yake. Ilitakiwa kabla ya wagombea wa vyama hawajapendekezwa ndio atoe hilo pendekezo lake lakini walikaa kimya. Muda wa kampeni umefika ndio anasema wapinzani waungane. Ni uhuni na ubinafsi ndani yake. Kuna game linataka kuchezwa hapa.
 
Huyo siyo opportunist ila ni ‘KIPYOTO’ (mchavuzi, mkorogagi) of which atarudi kundini kama kawaida!
Na cdm tupo nae vizuri kwenda kumuona lissu belgium mara 2 sio kigezo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…