Nikweli zoom mnakuwa na hilo tatizo sana hata mie hapa nimejaribu ku apply lakini ikifika hataua ya kuingiza zile alama nikimaliza tu ili nitume najibiwa kwamba nimekosea,,,ktk hili inawabidi mkubali na mfanye marekebisho coz leo unawezaona kwamba upo sahihi lakin kumbe kuna kitu kimebadilika kwenye system bila kujua....hata mie hili hali inanikera sana hata km hamlipwi na sisi tunaotafta hizo kazi lakini kumbuka umejitangaza mwenyewe kufanya hii kazi haina budi basi kuwa makini na kurekebisha haya makosa..:lol::lol:
binafsi nawaunga mkono na kuwapongeza sana zoom tanzania. kwani kupitia wao nimepata kazi niliyo nayo, pia nimefanya interview 2 ambazo nimeshindwana malipo na waajiri husika, na ingine ya tatu ni juzi tu, nimehudhuria na ninasubiria majibu pia.
sijawai kukutana na tatizo lolote na ninawapa big up sana kutusaidia sisi job seeker kutafuta kazi. m sure ukifuata utaratibu uliopo kila kitu kitakuwa pouwah!
Mara kwa mara huwa tunafanya test ya system yetu kuhakikisha kuwa inafanya kazi vizuri. Watu wengi wanashindwa katika hatua ya kuingiza zile alama kwa sababu zifuatazo:
Watu waliofuata ushauri hapo juu, walifanikiwa kirahisi. Jaribu halafu unitaarifu kama utashindwa
- Kwanza kabisa USIACHE space kati ya zile herufi. Zi-type zote bila kuacha space, kama neno moja.
- Pili, kama herufi zipo kwa herufi kubwa, andika kwa herufi kubwa, kama zipo kwa herufi ndogo, andika kwa herufi ndogo.
- Pia, una uwezo wa ku-REFRESH zile alama na kujaribu tena.
Tatizo linabaki kuwa mnatoa space ndogo sana ya attachments. 2MB ni kiduchu ku-upload CV, cover letter na certificates ambazo ujue lzm zinakuwa ni scanned docs.
Bumpkin Billionaire, unapotuma documents na picha kwa kutumia email, ni bora uzi-reduce size. Uchunguzi wetu umeonesha kuwa attachments zenye ukubwa wa zaidi ya 2MB zinaweza kupata shida kufunguka au kupokelewa. Hebu soma hapa ili ujue jinsi ya kupunguza size ya mafile > ZoomTanzania | Image Optimization