Mezaliwa kijijini, kukulia huko pia,
Mazao yetu shambani, mengi tulijivunia,
Tukayajaza ghalani, akiba kijiwekea,
Tukawa wenye furaha, usiku tumevimbiwa.
Nilimaliza la saba, nikarudi kijijini,
Nikafaulu si haba, wa taifa mtihani,
Nikamuambia baba, nae akafurahini,
Usiku sikuulala, naiona...