Sheria ya Ulinzi wa Taarifa ya Binafsi ya mwaka 2022 (Tanzania) inatumika kwa 'Ulinzi wa Taarifa Binafsi', ambazo ni taarifa zinazohusiana na mhusika wa taarifa (data subject). Sheria hii inawapa watu haki ya kulindwa faragha zao katika ukusanyaji, uchakataji na udhibiti wa taarifa.
Dkt. Noe Nnko
Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) imezitaka taasisi na mashirika kuwa makini katika matumizi ya taarifa za watu, kwani mtu yeyote ambaye taarifa zake zitatumika bila idhini anaweza kudai fidia ya hadi Sh. milioni 100, kwa mujibu wa sheria.
Akizungumza Machi 1, 2025...
TUME ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC), imesema wenye madaftari ya wageni kujiandikisha kwenye malango ya ofisi zao wanafanya makosa kwa mujibu wa Sheria ya Taarifa Binafsi kwa kuwa wanakusanya taarifa za watu bila ridhaa yao.
Mkuu wa Mahusiano na Mawasiliano wa Tume, Innocent Mungy ameyasema...
Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) imeongeza muda wa mwisho wa usajili kwa taasisi zote za umma na binafsi ambazo hazijajisajili kabisa na ambazo hazijakamilisha hadi kufikia tarehe 30 Aprili, 2025 baada ya muda wa usajili wa hiari kumalizika tarehe 31 Desemba, 2024 kama ilivyoelekezwa na...
Wakuu,
Wahenga wanasema mwenzako akinyolewa zako tia maji, Wenzetu Namibia yamewakuta, sisi tunajipanga vipi?
Taarifa kamili hizi hapa chini:
---
Kampuni ya simu ya Telecom inayomilikiwa na serikali ya Namibia imeshambuliwa na wadukuzi na kusababisha uvujaji wa taarifa nyeti za wateja...
https://www.youtube.com/live/JA35HedbKJA
JamiiForums na ADRH (Africa Digital Rights Hub) wanaendesha Kongamano la Afrika kuhusiana na Ulinzi wa Taarifa Binafsi jijini Kampala, Uganda ambapo Mwaka huu wa 2024 Kongamano hilo linaangazia Ulinzi wa Taarifa Binafsi kama nyenzo muhimu katika ukuaji...
Taasisi ya JamiiForums kwa kushirikiana na Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) iliendesha Mafunzo ya Uelewa wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi kwa Mhimili wa Mahakama ili kurahisisha mazingira ya Utekelezwaji wake katika Mashauri mbalimbali yanayofika Mahakamani.
Mafunzo hayo...
Kampuni ya TIGO imesema haihusiki na sakata la kuvuja Taarifa za Tundu Antipas Lisu
HONORA imesema kampuni mama ya Tigo haikuwa mmiliki Wakati Makamu mwenyekiti wa Chadema mh Tundu Antipas Lisu anashambuliwa
----
Dar es Salaam. Kampuni ya Honora Tanzania Public Limited Company ("TIGO")...
Hii ni sheria ya 2022 , lakini ni vyema kujifunza yafuatayo tunavyoelekea kwenye kesi ya Tundu Lissu vs Tigo kama mkusanyaji na mchakataji wa taarifa za Tundu lissu.
1. Kuna Tume ya ulinzi wa Taarifa binafsi
2. Mtu yeyote atakayebaini kuwa mkusanyaji au mchakataji amekiuka misingi ya ulinzi wa...
Mahakama yaiamuru Kampuni ya Safari Automotive Limited kulipa Fidia ya Milioni 10 kwa kusambaza video za mteja wao bila ridhaa yake.
Mahakama Kuu (Masijala ndogo ya Dar es Salaam) yaiamuru Kampuni ya Safari Automotive Limited kumlipa Godwin Danda fidia ya Shilingi Milioni Kumi (10,000,000/=) za...
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo amewapiga marufuku watendaji wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), wenye tabia ya kuuza siri za wateja na kuwasababishia matatizo.
Amesema kuwa haiwezekani mtumishi wa BRELA akachukua data na siri za kampuni akaenda kuuza kwa watu...
Hapa chini ni nyaraka zenye taarifa binafsi za mtu ambaye anaonekana aliomba nafasi ya kazi mahali fulani, lakini baada ya nyaraka zake kuisha kuisha umuhimu wakazitelekeza kiholela. Sijui waliuza hizo karatasi au walitupa watu wakaokota, haieleweki. Ila sasa zinapatikana kwa akina mama wauza...
Rais Samia, kwanza nashukuru umemuondoa Nape Nnauye kwasababu TCRA na Tume ya Ulinzi wa Taaifa Binfsi(PDPC), ni taasisi zilikuwa chini yake na mpaka anaondoka, hatuijaona hizi taasisi zikiwa serious katika kuchukua hatua(sijaona wala kusika waliokamatwa kwa kudhalilisha watanzania).
Naomba...
YAH: ONYO DHIDI YA KUFUNGA VIFAA VYA USALAMA (CCTV) KWENYE MAENEO YA FARAGHA
Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi - PDPC inatoa onyo kali kwa Taasisi na kampuni zote zinazotumia kamera za usalama ikiwa ni pamoja na maeneo ya kazi kuhakikisha wanazingatia Sheria na Kanuni za Ulinzi wa Taarifa...
Huu utaratibu wa wageni kutakiwa kujiandikishaa kwenye kitabu vya wageni vinavyofanana na vitabu vya mahudhurio ya wanafunzi kwenye hoteli, lodge na guest ni wa kijima au kishamba sana na umepitwa na wakati. Ni utaratibu mbovu kwa usalama na usiri wa mteja. Hii ndio sababu mojwapo inayopelekea...
Wapendwa wana JamiiForums,
Tunafurahia kuwa sehemu ya jamii yetu inayoheshimu faragha yenu kwa kuwaruhusu kutumia majina bandia ili kuwa huru kutoa maoni yenu na kushiriki mijadala kwa namna mbalimbali.
JF kama mitandao mingine ya kijamii inakutanisha watu wa aina mbalimbali, wenyewe nia...
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Emmanuel Mkilia amezionya Taasisi na Watu Binafsi wanaotoa Mikopo na kisha kuwadhalilisha Wakopaji ikiwa wameshindwa kurudisha Mikopo
Amesema, “Tutoe onyo kwa watu/Taasisi za Mikopo zinazowanyima haki ya faragha wateja kwa kuweka mikataba...
Juhudi za openAI za kupunguza matokeo yasiyo ya kweli kutoka kwenye chatbot yake ya ChatGPT yamegonga mwamba kwa sheria za data za Umoja wa Ulaya
Jopo la wachunguzi lililoundwa kwaajili kufuatilia usahihi wa taarifa za ChatGPT imesema "Ingawa hatua zilizochukuliwa ili kuzingatia kanuni ya uwazi...
Mara ya kwanza nilioona suala hili Royal Village, nimekuta wapiga picha kibao, ukikaa sura wazi wanakukochoa, na mtu umeshalipa hela nyingi kukaa kwa amani, ukitaka picha utawaita mwenyewe ila kule hali ni tofauti.
Niko hoteli nyingine leo, the same sh*t, jamaa kakomaa na kamera lake anataka...
Juzi (03.04.2024) tumeshuhudia Mh. Raisi akizindua Tume ya ulinzi wa taarifa binafsi na kusisitiza juu ya ulinzi wa taarifa binafsi kwakufata sheria. Sasa, je ni kwanini Sheria ya ulinzi wa taarifa binafsi ni muhimu kwetu watanzania? Leo nitawasanua wadau juu ya umuhimu wa sheria hii mpya nchini...
Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ya Mwaka 2022, ilianza kutumia rasmi Mei 01, 2023 na Tume inayosimamia Ulinzi wa Taaarifa Binafsi japo ilianza kufanya kazi tangu Mei 2023, imezinduliwa jana na Rais wa Samia Suluhu Hassan.
Najua Tume ina kazi nyingi za kufanya hasa kwa wakati huu ambapo ndio...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.