10% ya mikopo ya nchi yetu huwa anachukua nani?

10% ya mikopo ya nchi yetu huwa anachukua nani?

Mwande na Mndewa

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2021
Posts
1,117
Reaction score
3,153
Wakristo wa Ulaya walitusamehe nusu ya deni la taifa mwaka 2000, ila hivi sasa tunaelekea kuvunja rekodi ya kukopa kama vile nchi inaisha kesho.

Tukumbuke tuna watoto na wajukuu watakaohitaji kuishi katika nchi hii. Mikopo tunayokopa leo huku Waziri wa Fedha akitabasamu akiwa na afya tele, italeta balaa kwa nchi yetu hapo kesho. Mjomba mzungu aliyetusamehe mwaka 2000 hayupo tena.

Sasa hivi tunakopa kwa Mchina na Mwarabu. Hatari, Mwarabu asivyo na adabu ataomba taarabu. Swali ni hili: huyu dalali anayetudalalia usiku na mchana tuchukue mikopo ni nani?

Na ile ten percent ya hiyo mikopo anachukua nani hata kama rate ya mikopo si rafiki kwa ustawi wa nchi yetu?
 
Nchi yetu inaendelea kukopesheka kwa sababu Moja tu,tuna rasilimali nyingi sana,je ni sahihi kuendelea kukopa kila leo ilihali tuna rasilimali nyingi zinazotupa uwezo wa kukopa?
 
Mchina, Mwarabu, naona sasa umemsahau South Korea - Trillion 6. ( Pesa ndefu)- (( Koloni la USA))... sijui ni kwa nini sisi nchi kama nchi tunashabikia sana hayo mambo ya " tunakopesheka"... tufike mahali tuachane kabisa na mikopo. Ni utumwa, na tukiiendeleza, itakuwa ni mifano ya kausha damu na tutaitwa " highly indebted countries" kama tulivyokuwa tunaitwa kabla ya hao so called " wakristu na ndugu zao Paris club" hawajatusamehe. Tuamke, umatonya umezidi kwa kweli, bakuri kila sehemu. Ni aibu tupu kama nchi imeshindwa kujisimamia mambo yake yenyewe.
 
Back
Top Bottom