Ukosoma kitabu cha Principles na falsafa za Marcus utagundua na kufahamu kuwa Marcus ana link kubwa kwa Haile Selassie. Marcus ndiye aliyetabiri ujio wa Greatest Black King katika Ushairi wake wa mwaka 1923 na mwaka 1930 yalitimia maneno yake. Marcus alikuwa motivated sana na Kusimikwa Ufalme wa Ethiopia Haile Selassie. Aliwahi kusema ndiye mwafrika wa kwanza kusujudiwa na wazungu. Na ni kweli. Ndiye mtu wa kwanza mweusi Malkia Elizabeth II aliyemuinamia na kumpa heshima alipomwona. Ilimpa motivation sana Garvey. Alipokuwa mdogo aliwahi kuota ndoto ya Mfalme mweusi anainamiwa na mzungu na alihisi ametimiza kuona ndoto ile.
Wafuasi wa Back to Africa movement wengi walikimbilia Liberia na Wengine Haile Selassie aliwapa Sehemu yake ya eneo lake Binafsi wakae na kuwatunza na mpaka leo wapo Shashamane Ethiopia.
Kwame alisaidiwa sana na Haile Selassie kushinda ukoloni nchini kwake na walikuwa marafiki sana. Ila wote walishirikiana sana katika kumtetea mtu mweusi.
Haile ndie nayetambulika kama Mfalme aliyeweka historia kubwa Kiimani na kihistoria ya mwafrika. Aliwasaidia viongozi wa Afrika kijeshi na ndiye mweusi wa Kwanza kusimama League Of Nation (Umoja wa Mataifa) kumtetea mtu mweusi. Ndiye mwanzilishi umoja wa Afrika na kiongozi wa Kwanza wa AU. Na kupewa heshima yake kwa kuweka makao makuu kuwa Mjini mwake.
Ila yote hayo...tuwaenzi leaders wetu waliotupigania mpaka hapa. Wanahistoria kubwa sana.