2010 elections: JF tunasupport WAZEE au VIJANA?

2010 elections: JF tunasupport WAZEE au VIJANA?

back to the same


Tyson [Wassira] kasema hawaachii vijana jimbo la Bunda kwavile wanapuliza ganja!! Mbona na yeye alikuanalipuliza alipokuwa kijana na haikumzuia kupata uongozi; na wenzie anaofanya nao kazi mbona tunawajua kuwa wanalipuliza ganja na wanafanya kazi vizuri tu; itabidi Tyson atafute sababu nyingine ya kukataa kung'atuka!!!! Tuchague viongozi kufuatana na jinsi watavyochangia kututoa katika lindi hili la umaskini ni sio kwa kigezo cha umri!!
 
To me i think we need to have both generations to support the head of state to implement 2010/15 manifesto.
 
Hapa tutapotezana. Tanzania au watanzania wengi wamezoea mambo ya chama kimoja ndio maana unakuja na hoja kama hii.

Kwa hali ilivyo sasa watu wanaangalia mtu binafsi badala ya sera za chama. Chama kama kinataka kuongoza nchi ni lazima kiwe na sera zinazofaa kijimbo hadi kinchi. Hivyo basi kusema utamchagua mzee au kijana kwa sera zake binafsi bila kuangalia sera za chama chake ni sawa na kuchagua sura kama wengi mlivyofanya kwenye uchaguzi uliopita.

Hapa swala la msingi ni kujadili sera za kila chama, kuzipima kama zinafaa, halafu unafanya uamuzi.

Hawa viongozi tuliochagua kwa kusikiliza sera zao binafsi ndio hivyo tena tumekuja kugundua wengi wao ni mafisadi. Sasa utaendelea kumchagua fisadi kwa kuwa ni kijana au mzee. Wakati huo huo chama chake hakina hata mpango wa kumshitaki kwa kuwa wote ni mafisadi?

Jamani watanzania wenzangu, tubadilike na tuache unafiki. Mabadiliko ya kweli yanaanza na wewe na mimi binafsi. Tuchague kiongozi kulingana na sera na sio sura.

Aagh! Vidole vinauma, tujaribu kubadilika!
 
Kuna mahusiano makubwa sana kati ya umri wa mtu na uwezo wa kufanya maamuzi ya haraka kutokana na mazingira husika,mie siamini mzee aliyekaa bungeni miaka arobaini akaleta mabadiliko kwa maana ya maendeleo kwenye jimbo husika ama wizara husika,mifano ipo mingi ya hawa wazee kushindwa kutofautisha mfumo wa vyama vingi na chama kimoja,wengi wa wazee hawa bado wanamawazo ya kale ya chama kushika hatamu,na kwamba hawaamini **** kuna chama kinaweza kuongoza nchi hii nje ya CCM.Kwa hiyo tunahitaji vijana wanaoweza kuleta maendeleo ya kweli lakini pia kama wapo wazee wenye uwezo unaofanana na Dr.Slaa,S.Sita,shelukindo na wengine wapewe nafasi ili wawape vijana uzoefu.
 
- Tu-support uwezo wa uongozi ushahidi upo wazi wa wanaoweza na wasioweza, kuna vijana hawafai na kuna wazee wasiofaa, JF tujiepushe na ideology za ujana na uzee maana ushahidi tunao tena mkubwa sana kwamba sio tija, kuna vijana wametuangusha na kuna wazee wametuangusha,

- Binafsi siwezi kushauri kuudwa sheria moja ya kuwazuia wazee wa CCM, na nyingine ya kuwaruhusu wazee wa Chadema, ninasema itakwua ni a National nightmare kuwakosa wazee kama Dr. Slaa na Ndesamburo bungeni kwa sababu ya hizi ideology za ujana na uzee, cha muhimu JF tukachukue fomu za kugombea, tuelimishe wananchi kuhusu viongozi wanaofaa na wasiofaa na sababu, sio maneno ya ujana na uzee!

- Hii kioo cha jamii kinapaswa kuwa bigger than hizi ideology za uzee na ujana, maana hazina nafasi katika jamii yoyote duniani inayotaka kuendelea mbele, na pia it is about time sasa taifa letu likaanza kufikiria mikakati ya kuwapatia wazee wenye elimu za juu nafasi za kuendelea kutumia elimu zao na experience zao za kazi kwa taifa, kama majuzi tumeona jinsi Mzee Kaunda alivyopewa kazi kule Boston ya kufundisha University miaka miwili na malipo mazito sana,

- Halafu pia tatizo lingine kubwa ni namna ya kuwajengea hoja nzito za kuwafanya wakubali, badala ya kutumia matusi na kejeli, na huwezi kusema mzee Slaaa, abaki lakini wazee wengine waondoke haya hayawezi kuwa mawazo ya Great Thinkers!

JF tuende kuchukua fomu za kugombea uongozi ndio dawa peke yake ya kuwajibu wazee tusiowataka!


Respect.

FMEs!
 
I think its about time tukaamua kama chombo kwenye uchaguzi wa 2010 tunasupport Vijana au wazeee

by Vijana simaanishi akina calibr ya akina Lawrence Masha (alishapata nafasi na alishindwa na si Kijana anymore) balli ninamaanisha Vijana ambao wako UNDER 36 yrs regardless of chama kipi wanakiwakilisha

In otherwords tunaendelea na BACK TO THE SAME au NEW BLOOD

lakini its about time tukaamua tuko upande upi.

This quest is useless.
 
Possibly it is very exhilarating subject!!!!
First let us look the advantage and disadvantages of the subject on the table.To me it preposterous to bring this topic on the table because if we will entertain this kind of topics, absolutely it will exterminate the democracy which we're enjoying in Tanzania.
I could much appreciate if we could start discussing how we can educate our people for not selecting their leaders on the basis of corruption, that could worth something rather than discussing vijana and wazee. What we need is a proficiently leader regardless of the sex or age.
Naipenda Sana Tanzania
 
Back
Top Bottom