Kidudu Mtu
Member
- Nov 7, 2009
- 64
- 0
IJUMAA iliyopita, Rais Jakaya Kikwete aliandaa hafla maalumu ya kukaribisha Mwaka Mpya kwa mabalozi wanaowakilisha nchi zao Tanzania, iliyofanyika Ikulu ya Dar es Salaam na ambayo huifanya kila mwaka kama ada.
Akizungumza na mabalozi hao katika salamu zake za Mwaka Mpya kwao, pamoja na mambo mengine, Rais alisisitiza wawakilishi hao wa nchi hizo kuzingatia kuwa mwaka huu ni wa uchaguzi nchini, na asingetarajia kuwaona wakijiegemeza katika vyama vya siasa au wagombea.
Bila kutafuna maneno, Rais aliwaambia mabalozi hao kuwa watanzania hawataki kuchaguliwa viongozi, ila wana uamuzi wao wenyewe na ridhaa ya kuona ni chama gani au kiongozi yupi anastahili kuwaongoza katika kipindi kingine cha miaka mitano.
Aliwaonya kuwa atakayekiuka dhima yake ya uwakilishi wa nchi yake, atakuwa anajihalalishia kufukuzwa nchini na atakuwa pia amemdhalilisha aliyemtuma kumwakilisha, kwani kufanya hivyo ni kukiuka kazi yake ya uanadiplomasia.
Tunampongeza Rais na kuungana naye katika kuwafahamisha mabalozi hao kuwa Tanzania ina wenyewe na kuwakaribisha kuziwakilisha nchi zao si hati ya kuwaruhusu kuingilia mambo ya ndani ya nchi kama vile wanataka kuitawala.
Diplomasia si ukoloni, hivyo balozi anapokuwa ameteuliwa na nchi yake kuiwakilisha katika nchi nyingine, atambue kuwa anakwenda huko si kuiamrisha, kuiagiza au kuielekeza kufanya hiki au kile, la hasha, jukumu lake ni kujenga na kuimarisha uhusiano uliopo.
Kazi na wajibu wa balozi ni kupatanisha au kusuluhisha kama kuna mgogoro na kusababisha mambo yafanikiwe katika nchi yake au nchi aliyomo; hivyo hana haki ya kuikemea, kuigombanisha au kuikosanisha nchi anayoiwakilisha na nchi mwenyeji au kuwafarakanisha wananchi wa nchi hiyo.
Kwa kuwa huo ndiyo wajibu wake, kama alivyowaambia Rais Kikwete, basi waendelee kusaidia ili hatimaye uchaguzi nchini uwe huru na wa haki na kila upande utakaoshiriki uridhike na matokeo na kuendelea kuijenga nchi kwa pamoja.
Ilishakuwa kama kawaida kwa baadhi ya mabalozi kujisahau na kujikuta wakifanya siasa badala ya uwakilishi, na matokeo yake huegemea katika baadhi ya vyama vya siasa na hatimaye kuchangia kujenga chuki miongoni mwa wananchi.
Yawezekana misaada yao ndiyo inayowapa kichwa cha kudhani kuwa wanaweza kuifanyia lolote nchi na kutishia kuinyima misaada kama haitatii amri, kama hiyo ndiyo imani na welewa wa baadhi ya mabalozi, basi wajue Tanzania ni 'masikini jeuri' asiyetaka kuyumbishwa.
Watanzania na hasa viongozi wa vyama vya siasa wanaodhani kuwa mambo hayaendi bila ufadhili, walisahau hilo na badala yake walinde uhuru wao wa kujiamulia mambo yao wenyewe kwa maslahi yao na kuhakikisha wanaondokana na fikra za utumwa.
Tunasema balozi ye yote atakayekiuka mwito wa Rais Kikwete, aoneshwe njia na awaache watanzania wajiamulie mambo yao ya kidemokrasia kwa kupingana bila kupigana na kuchaguana kwa uhuru na haki kama wanavyoona na kujipangia wao.
SOURCE: http://www.habarileo.co.tz/tahariri/?n=5189&cat=tahariri
SWALI: HIVI TANZANIA KUNA UCHAGUZI AU UTEUZI?
Mhariri anazungumzia demokrasia ipi? Ya kura kwa kubadilishana na khanga, wali, pombe na fulana?
Akizungumza na mabalozi hao katika salamu zake za Mwaka Mpya kwao, pamoja na mambo mengine, Rais alisisitiza wawakilishi hao wa nchi hizo kuzingatia kuwa mwaka huu ni wa uchaguzi nchini, na asingetarajia kuwaona wakijiegemeza katika vyama vya siasa au wagombea.
Bila kutafuna maneno, Rais aliwaambia mabalozi hao kuwa watanzania hawataki kuchaguliwa viongozi, ila wana uamuzi wao wenyewe na ridhaa ya kuona ni chama gani au kiongozi yupi anastahili kuwaongoza katika kipindi kingine cha miaka mitano.
Aliwaonya kuwa atakayekiuka dhima yake ya uwakilishi wa nchi yake, atakuwa anajihalalishia kufukuzwa nchini na atakuwa pia amemdhalilisha aliyemtuma kumwakilisha, kwani kufanya hivyo ni kukiuka kazi yake ya uanadiplomasia.
Tunampongeza Rais na kuungana naye katika kuwafahamisha mabalozi hao kuwa Tanzania ina wenyewe na kuwakaribisha kuziwakilisha nchi zao si hati ya kuwaruhusu kuingilia mambo ya ndani ya nchi kama vile wanataka kuitawala.
Diplomasia si ukoloni, hivyo balozi anapokuwa ameteuliwa na nchi yake kuiwakilisha katika nchi nyingine, atambue kuwa anakwenda huko si kuiamrisha, kuiagiza au kuielekeza kufanya hiki au kile, la hasha, jukumu lake ni kujenga na kuimarisha uhusiano uliopo.
Kazi na wajibu wa balozi ni kupatanisha au kusuluhisha kama kuna mgogoro na kusababisha mambo yafanikiwe katika nchi yake au nchi aliyomo; hivyo hana haki ya kuikemea, kuigombanisha au kuikosanisha nchi anayoiwakilisha na nchi mwenyeji au kuwafarakanisha wananchi wa nchi hiyo.
Kwa kuwa huo ndiyo wajibu wake, kama alivyowaambia Rais Kikwete, basi waendelee kusaidia ili hatimaye uchaguzi nchini uwe huru na wa haki na kila upande utakaoshiriki uridhike na matokeo na kuendelea kuijenga nchi kwa pamoja.
Ilishakuwa kama kawaida kwa baadhi ya mabalozi kujisahau na kujikuta wakifanya siasa badala ya uwakilishi, na matokeo yake huegemea katika baadhi ya vyama vya siasa na hatimaye kuchangia kujenga chuki miongoni mwa wananchi.
Yawezekana misaada yao ndiyo inayowapa kichwa cha kudhani kuwa wanaweza kuifanyia lolote nchi na kutishia kuinyima misaada kama haitatii amri, kama hiyo ndiyo imani na welewa wa baadhi ya mabalozi, basi wajue Tanzania ni 'masikini jeuri' asiyetaka kuyumbishwa.
Watanzania na hasa viongozi wa vyama vya siasa wanaodhani kuwa mambo hayaendi bila ufadhili, walisahau hilo na badala yake walinde uhuru wao wa kujiamulia mambo yao wenyewe kwa maslahi yao na kuhakikisha wanaondokana na fikra za utumwa.
Tunasema balozi ye yote atakayekiuka mwito wa Rais Kikwete, aoneshwe njia na awaache watanzania wajiamulie mambo yao ya kidemokrasia kwa kupingana bila kupigana na kuchaguana kwa uhuru na haki kama wanavyoona na kujipangia wao.
SOURCE: http://www.habarileo.co.tz/tahariri/?n=5189&cat=tahariri
SWALI: HIVI TANZANIA KUNA UCHAGUZI AU UTEUZI?
Mhariri anazungumzia demokrasia ipi? Ya kura kwa kubadilishana na khanga, wali, pombe na fulana?