2016 to 2021, maono ya kuwa Hayati Magufuli atafariki dunia yalikuwa ni mengi sana humu ndani na nje ya hili jukwaa

2016 to 2021, maono ya kuwa Hayati Magufuli atafariki dunia yalikuwa ni mengi sana humu ndani na nje ya hili jukwaa

Kipindi hicho nilikuwa sio mtumiaji sana wa Jf, hizo nyuzi sikuziona.

Ila kosa kubwa ambalo PM Majaliwa alifanya ni kuudanganya umma kuwa Magufuli ni mzima kumbe alikuwa anaumwa kweli. Wakati ambao kulikuwa na minong'ono nchi nzima Magufuli anaumwa,viongozi wangejitokeza na kusema ukweli kama anaumwa kuna namna iliyo nje ya uwezo wa kibinadamu ingeweza kufanyika kuzuia kifo chake mpaka amalize muhula wake lakini viongozi waliudanganya umma , umma ukaja kushtukizwa na taarifa za kifo chake.

Niliyahisi maumivu ya watanzania mahali popote mwili wa Magufuli ulipokuwa unapita. Watanzania waliumizwa sana na kifo cha Magufuli.
Hata waliouwawa wakati wa Magufuli, watanzania wengi waliumizwa na vifo vile.
 
Kwa zile heka heka za jiwe ilikuwa ngumu kutoboa hai. Ndio maana watu wengi walimtabiria kifo

maana Maadui walikuwa smart kuliko wanaomlinda.

Hakuna mtu mweusi yeyote anaeweza kujilinda dhidi ya biological weapon ama technological weapon kama wababe wakitaka kukuondoa duniani.

Huwezi kujilinda na hayo mambo kwa kutegemea walinzi wenye degree za udsm na muhimbili
Maadui zake walikua smart kuliko yeye
 
Hakuna Mtanzania aliyeumizwa na kifo cha huyo mtu wako, iko hivi, Kijijini kwetu Kajunjumele aliwahi kuwapo Mamba kwenye mto Kiwira aliyekuwa anamaliza watu na mifugo, watu hawakumpenda Mamba yule, lakini siku alipokuja kuuawa na Maofisa wa wanyapori, Kyela nzima ilijaa kuja kujionea Mamba huyo mla watu, umati ulikuwa mkubwa sana!

Unadhani Mamba yule alipendwa?
Jubha jubha!
Hawakufuata kitoweo hao mkuu?
 
Yeyote anayejifanya Mungu atakufa kibwege sana! Wakati Jiwe, Polepole na Bashiru wakinunua Wapinzani, Jiwe alikuwa akisema hivi, Nanukuu "Waacheni waliolemewa na mizigo waje kwangu nami nitawapumzisha" Hii ilikuwa kauli ya kijinga kabisa ya Jiwe ya kujjfananisha na Mungu iliyommaliza kabisa.

Nabii Lema aliwahi kumuonya kwamba akiendelea kujiita Mungu atakufa lakini akapuuza na akamkamata na kumtupa selo kwa muda mrefu, ndio kama hivihivi wanavomfanyia Dr Slaa
Nimejiuliza, nikujibu au niache...nimesikitishwa na ulichoandika.

Itoshe kusema mkuu, unawaza/kufikiri ki-CCM CCM, ingawa sijajua wewe ni wa mlengo gani.
 
Back
Top Bottom