Yamebaki masaa machache kabla hatujaenda kujipanga katika foleni kuelekea katika masunduku ya kupigia kura. Hili kila mtu mwenye akili timamu analipatia uzito wa kipekee kwani ndio muamuzi wa kumuweka madarakani kiongozi mkuu wa nchi, na kwa mujibu wa katiba ya nchi yetu, ni kiongozi atakayehudumu kwa takribani miaka mitano ijayo. Hicho sio kipindi kifupi, ni kipindi kirefu sana.
Kwa kuzingatia hilo, nadhani kila mmoja wetu anaweza kuona ni namna gani atajutia kwa kitendo kitakachopelekea kushuhudia mambo yanaenda kinyume au tofauti na alivyotegemea wakati anapiga kura. Hapa ndipo unakuja ule msemo kuwa majuto ni mjukuu, kama mababu zetu walivyotuasa. Sasa kwa hapa, mtoto ni nani na mjukuu ni nani?
Mtoto ni kura yako utakayopiga kesho; ndio mustakari utakaoamua ni na nani awe madarakani. Kufanya maamuzi yasiyo sahihi katika kupiga kura ndio yatazaa usiyoyategemea na kukuacha umeduwaa; na huyu ndio majuto mwenyewe. Hivyo basi, tutafakari kwa hekima kabla ya kupiga kura zetu, kwani ukifanya makosa huwezi kufanya masahihisho, kwa hiyo kama ni mzigo umebeba mgongoni, basi huutui mpaka miaka mitano ipite.
Tumewasikia wakinadi sera zao kila mahali walipokwenda kwa ajili ya kuomba kura. Kila mmoja wao alieleza vipaumbele vyake pindi atakapochaguliwa kuwa kiongozi. Kwa mtu makini, mpaka kufikia sasa hivi ameshampata mtu sahihi,ambaye hapo kesho atampa kura yake.
Ni jambo lisilotia shaka kuwa katika hao waliopitishwa na vyama vyao kugombea kinyang'anyiro hicho, yupo mmoja ambaye sera zake zimelenga kuwajali zaidi wananchi na mustakabali mzima wa taifa letu, huyu si mwingine bali ni Dr. John Pombe Joseph Magufuli.
Sisemi haya kwa sababu ya itikadi au ushabiki, la hasha. Nasema haya kutokana na ukweli kuwa kila alipopita alisema kile ambacho kiko ndani ya uwezo wake kiutekelezaji. Ameongelea mambo kadha wa kadha, kama vile afya, elimu, maji, barabara, nishati, na miundombinu mingine huku akielekeza huduma hizo kuwa na masilahi kwa matabaka yote ya watu hapa nchini; mtu wa kipato cha chini, cha kati, na cha juu, wote kwa namna moja au nyingine watanufaika kwa sera hizi zinazoonekana kutekelezeka.
Na hili halina shaka kwa kuwa tayari tumeona kwa kipindi cha miaka mitano anayomaliza. Hii inatupatia dira nzuri ya kuamini na kuona kuwa huyu kumbe tukimpa tena, atatusogeza mbali zaidi. Hapa gari limeshashika spidi tunachotakiwa kulichochea mafuta ili liende spidi kubwa zaidi (it is in dynamic state), kuliko kuanza kuliwasha gari ambalo limesimama tu (in static), nguvu ya kulianzisha itakuwa kubwa zaidi.
Mara nyingi tunaamini kwa kile tunachokiona, mheshimiwa huyu tumeyaona aliyofanya kwa kipindi alichokaa madarakani, sasa kwa nini tuwe ba shaka naye ilihali tunashuhudia mambo makubwa aliyoyafanya? Tusije kujilaumu baadae kwa kuchagua kwa kubahatisha na hivyo kuubeba huo mgogoro kwa kipindi cha miaka mitano.
Hivyo, tuone ni bahati kuwa na mgombea ambaye historia yake tunaijua vyema, na hivyo kutokuwa na mashaka ya kumchagua mtu sahihi. Mwanazuoni mmoja aliwahi kusema, "one bird in the hand worths two birds in the bush", tafsiri yake ni kuwa ndege mmoja uliyemshika mkononi ana thamani ya ndege wawili walioko porini. Maana yake hapa ni kuwa tushikilie kwanza kile tulicho nacho, kuliko kukipoteza, tukitegemea tutatafuta kingine.
Tuna ndege wetu tayari mkononi, tumtunze huyu, tusiwe na tamaa ya wale wawili wa porini. Kwanza hatujuwi kama tunaweza kuwakamata na isitoshe tutakapoenda huko porini kuwatafuta tutakutana na changamoto nyingi sana. Huko porini tunaweza kuchomwa na miti/miiba, kukumbana na wanyama wakali kama nyoka na wengineo, na zaidi ya hapo, hao ndege tunaowakimbiza hata tukiwapata wanaweza wakawa na matatizo yao, maana na wenyewe pia ni viumbe. Wanaweza wakawa na magonjwa kama vile typhoid, mafua ya ndege, na magonjwa mengine wahusianayo nayo.
Hivyo ni bora tukaridhika na huyu mmoja tuliyekuwa naye kuliko kusumbuka kuwafuata wale wawili wa porini huku tukiwa hatuna uhakika wa kuwapata lakini pia na afya zao. Kiongozi mmoja mwandamizi mstaafu kutoka Kanda ya Kaskazini, aliwahi kuwauliza wananchi wa moja ya mikoa ya huko kuwa, hivi inaingia akilini, nyumbani wameandaa wali na nyama, halafu eti hawa tulioandaliwa wali ma nyama tunauacha wali halafu tunakwenda porini kutafuta matunda pori. Hiyo inaingia akilini kweli? Labda mwenda wazimu ndio anaweza akafanya hivyo.
Hata mimi nakumbuka kipindi tulipokuwa watoto, kilikuwa kipindi cha mvua, watoto wa jirani yetu walienda porini kutafuta uyoga, walipata na wakarudi nyumbani wakapika na kula. Wakati huo mama na baba yao walikuwa shambani. Baada tu ya kumaliza kula, wakaanza kuumwa matumbo, wakahara na kutapika, muda mfupi baadae hali zao zilikuwa mbaya sana. Majirani wakawabeba na kuwapeleka hospitali, na wazazi wao kupelekewa taarifa huko shambani. Nilikuja kugundua kuwa kumbe sio kila uyoga huliwa, uyoga mwingine una sumu!
Ndugu zangu, kesho twende tukapige kura, asibaki hata mmoja. Tukampe Dr. John Pombe Joseph Magufuli kura za ndio. Lakini pia tumpe na wabunge na madiwani ili kukamilisha mafiga matatu, kwani figa moja au mawili hayainjiki chungu. Tusisahau miradi aliyoianzisha, aje akamilishe na kuanzisha na kuendeleza mingine. Huyu ni mtu wa watu, haangalii matabaka, rangi, kabila wala dini.
HUYU NI MWENZETU
Kwa kuzingatia hilo, nadhani kila mmoja wetu anaweza kuona ni namna gani atajutia kwa kitendo kitakachopelekea kushuhudia mambo yanaenda kinyume au tofauti na alivyotegemea wakati anapiga kura. Hapa ndipo unakuja ule msemo kuwa majuto ni mjukuu, kama mababu zetu walivyotuasa. Sasa kwa hapa, mtoto ni nani na mjukuu ni nani?
Mtoto ni kura yako utakayopiga kesho; ndio mustakari utakaoamua ni na nani awe madarakani. Kufanya maamuzi yasiyo sahihi katika kupiga kura ndio yatazaa usiyoyategemea na kukuacha umeduwaa; na huyu ndio majuto mwenyewe. Hivyo basi, tutafakari kwa hekima kabla ya kupiga kura zetu, kwani ukifanya makosa huwezi kufanya masahihisho, kwa hiyo kama ni mzigo umebeba mgongoni, basi huutui mpaka miaka mitano ipite.
Tumewasikia wakinadi sera zao kila mahali walipokwenda kwa ajili ya kuomba kura. Kila mmoja wao alieleza vipaumbele vyake pindi atakapochaguliwa kuwa kiongozi. Kwa mtu makini, mpaka kufikia sasa hivi ameshampata mtu sahihi,ambaye hapo kesho atampa kura yake.
Ni jambo lisilotia shaka kuwa katika hao waliopitishwa na vyama vyao kugombea kinyang'anyiro hicho, yupo mmoja ambaye sera zake zimelenga kuwajali zaidi wananchi na mustakabali mzima wa taifa letu, huyu si mwingine bali ni Dr. John Pombe Joseph Magufuli.
Sisemi haya kwa sababu ya itikadi au ushabiki, la hasha. Nasema haya kutokana na ukweli kuwa kila alipopita alisema kile ambacho kiko ndani ya uwezo wake kiutekelezaji. Ameongelea mambo kadha wa kadha, kama vile afya, elimu, maji, barabara, nishati, na miundombinu mingine huku akielekeza huduma hizo kuwa na masilahi kwa matabaka yote ya watu hapa nchini; mtu wa kipato cha chini, cha kati, na cha juu, wote kwa namna moja au nyingine watanufaika kwa sera hizi zinazoonekana kutekelezeka.
Na hili halina shaka kwa kuwa tayari tumeona kwa kipindi cha miaka mitano anayomaliza. Hii inatupatia dira nzuri ya kuamini na kuona kuwa huyu kumbe tukimpa tena, atatusogeza mbali zaidi. Hapa gari limeshashika spidi tunachotakiwa kulichochea mafuta ili liende spidi kubwa zaidi (it is in dynamic state), kuliko kuanza kuliwasha gari ambalo limesimama tu (in static), nguvu ya kulianzisha itakuwa kubwa zaidi.
Mara nyingi tunaamini kwa kile tunachokiona, mheshimiwa huyu tumeyaona aliyofanya kwa kipindi alichokaa madarakani, sasa kwa nini tuwe ba shaka naye ilihali tunashuhudia mambo makubwa aliyoyafanya? Tusije kujilaumu baadae kwa kuchagua kwa kubahatisha na hivyo kuubeba huo mgogoro kwa kipindi cha miaka mitano.
Hivyo, tuone ni bahati kuwa na mgombea ambaye historia yake tunaijua vyema, na hivyo kutokuwa na mashaka ya kumchagua mtu sahihi. Mwanazuoni mmoja aliwahi kusema, "one bird in the hand worths two birds in the bush", tafsiri yake ni kuwa ndege mmoja uliyemshika mkononi ana thamani ya ndege wawili walioko porini. Maana yake hapa ni kuwa tushikilie kwanza kile tulicho nacho, kuliko kukipoteza, tukitegemea tutatafuta kingine.
Tuna ndege wetu tayari mkononi, tumtunze huyu, tusiwe na tamaa ya wale wawili wa porini. Kwanza hatujuwi kama tunaweza kuwakamata na isitoshe tutakapoenda huko porini kuwatafuta tutakutana na changamoto nyingi sana. Huko porini tunaweza kuchomwa na miti/miiba, kukumbana na wanyama wakali kama nyoka na wengineo, na zaidi ya hapo, hao ndege tunaowakimbiza hata tukiwapata wanaweza wakawa na matatizo yao, maana na wenyewe pia ni viumbe. Wanaweza wakawa na magonjwa kama vile typhoid, mafua ya ndege, na magonjwa mengine wahusianayo nayo.
Hivyo ni bora tukaridhika na huyu mmoja tuliyekuwa naye kuliko kusumbuka kuwafuata wale wawili wa porini huku tukiwa hatuna uhakika wa kuwapata lakini pia na afya zao. Kiongozi mmoja mwandamizi mstaafu kutoka Kanda ya Kaskazini, aliwahi kuwauliza wananchi wa moja ya mikoa ya huko kuwa, hivi inaingia akilini, nyumbani wameandaa wali na nyama, halafu eti hawa tulioandaliwa wali ma nyama tunauacha wali halafu tunakwenda porini kutafuta matunda pori. Hiyo inaingia akilini kweli? Labda mwenda wazimu ndio anaweza akafanya hivyo.
Hata mimi nakumbuka kipindi tulipokuwa watoto, kilikuwa kipindi cha mvua, watoto wa jirani yetu walienda porini kutafuta uyoga, walipata na wakarudi nyumbani wakapika na kula. Wakati huo mama na baba yao walikuwa shambani. Baada tu ya kumaliza kula, wakaanza kuumwa matumbo, wakahara na kutapika, muda mfupi baadae hali zao zilikuwa mbaya sana. Majirani wakawabeba na kuwapeleka hospitali, na wazazi wao kupelekewa taarifa huko shambani. Nilikuja kugundua kuwa kumbe sio kila uyoga huliwa, uyoga mwingine una sumu!
Ndugu zangu, kesho twende tukapige kura, asibaki hata mmoja. Tukampe Dr. John Pombe Joseph Magufuli kura za ndio. Lakini pia tumpe na wabunge na madiwani ili kukamilisha mafiga matatu, kwani figa moja au mawili hayainjiki chungu. Tusisahau miradi aliyoianzisha, aje akamilishe na kuanzisha na kuendeleza mingine. Huyu ni mtu wa watu, haangalii matabaka, rangi, kabila wala dini.
HUYU NI MWENZETU