2021 AFCON Special Thread

Naam alikuwa akifanya biashara zake katika visiwa vya re union ndo rais biya aliwaalika ikulu katika kuuliza uliza kila wanae mtajia ana waambia sio huyo mara mtu akatamka Roger akawaambia naam wakamjibu huyo kaisha staafu soka akawaambia huyo huyo atafutwe aje alisaidie taifa millah akarudi mechi ya ufunguzi dhidi ya Argentina bao alifunga François omam biyik kwa kichwa dakika ya 67 mila akiingia dakika ya 81 kuchukua nafasi ya Cyril makanaky watu wawili wa kati Benjamin massing na mdogo wake mfungaji wa bao Andrew kana biyik akipewa kadi nyekundu. Mechi Roger alifunga na kukata mauno ilikuwa dhidi ya Colombia akimpokonya mpira nyanda mtata ila mtamu sana rene heiguita.
 
Asante mkuu kwa kuweka rekodi sawa!! 🙏🏻
 
kudos mkuu nilijiuliza sana ni nani huyu anayepewa jukumu la kupeleka kombe uwanjani bila majibu . this is super good kuwaheshimu malegend wetu, bila shaka kwasasa atakuwa na nafasi fulani katika moja wapo ya shirikisho la mpira wa miguu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshambuliaji wa zamani wa timu ya taifa ya Cameroon, Roger Milla...

Kama ni mfuatiliaji wa WC, kuna mchezaji mmoja mwafrika huwa anaoneshwa oneshwa baada ya kufunga goli anakimbilia kilipo kipendera cha kona na kuanza kukata mauno...
sawasawa mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waarabu ndicho nachowapendea hawana time na mzungu....angalia hata akina aboutrika n.k ni mafundi haswaa lakini hawakuwa na tamaa ya kwenda nje, nationality yao ndio kitu cha kwanza, na wala hawaringi
Mahrez, mido, Salah Kwan sio waarabu?
 
Mkuu, unaweza tupa kwa uchache kuhusu Rashid Yekini pia
 
Mkuu, unaweza tupa kwa uchache kuhusu Rashid Yekini pia
Mmoja kati ya miamba ya soka sio tu naigeria bali hata club yake ya kwanza nje ya bara la Africa Victoria setubal ya ureno aliichezea kwa mafanikio kwa michezo 108 na kufunga magoli 90 toka 1990 mpaka 1994. Alikuwepo katika fainali ya mataifa huru (afcon )mwaka 1994 na kuweza kushinda dhidi ya timu pendwa na pengine iliyoonewa huruma na mashabiki wengi duniani kwa waqt huo ya Zambia ambayo walijikusanya upya baada ya ajali mbaya kutokea katika soka la Africa kupoteza wachezaji zaidi ya 20 na viongozi wao katika pwani ya Gabon. Nigeria wakatwaa kombe huku wakiwa na nafasi ya kwenda USA katika kombe la dunia na miamba ya Nigeria yekin samson siasia chidi nwanu stephen keshi wakitutoa kimasomaso kwa kushinda mechi dhidi ya Bulgaria Rashid akifunga bao na kwenda kuzishika nyavu kwa nguvu na hisia kali style hiyo ilitamba sana zama hizo. Baadae aliondoka setubal na kwenda nadhani Spain hakuwahi kupata waqt mzuri tena katika soka kama alivyokuwa setubal ndio mwanasoka bora 1993 wa afrika ndio all time top scorer wa Nigeria 37. Alifariki 2010 kama sijasahau akiwa na miaka 48.
 
Na alifariki akiwa na maradhi ya akili. Miongoni mwa Striker halisi unapotaja neno hilo pamoja na kina Patrick Mboma na Samuel Eto'o na George Weah.
 
Na alifariki akiwa na maradhi ya akili. Miongoni mwa Striker halisi unapotaja neno hilo pamoja na kina Patrick Mboma na Samuel Eto'o na George Weah.
Yaah pana sintofahamu kubwa kuhusu umauti wake pana jirani alisema aliwaona nduguze wakimchukua mkuku mkuku na baada ya siku chache ikatangazwa amefariki. Unapo zungumza natural striker kwa afrika huwezi muondoa ingawa alikuwa na uchoyo flan tizana game ya fainali 1994 dhidi ya Zambia bado tutamkumbuka yekini
 
Asante Mkuu, clip zake huwa napenda sana kuziangalia YouTube, style yake ya kushangilia huwa inanivutia sana

Alale mahali pema peponi mkongwe huyu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…