2021 AFCON Special Thread

2021 AFCON Special Thread

Okay Senegal bingwa na Ana deserve was a better team today. Lakini golikipa wa tournament Ni gamal wa Egypt sio Mendy wa Senegal na player wa tournament ni Vincent Aboubakary sio Sadio Mane. Sijui wanatumia vigezo vipi kuchagua hawa wachezaji[emoji2371]
Aboubakary n mfungaji bora .... hawez kuwa mchezaj bora ..coz mchezaji bora wanaangalia vitu vingi zaid ya kufunga tuu ...Ukimuangalia Mane kwanza amekua akianzisha mashambulizi ....ametoa assist kadhaa na pia ameweza kuiongoza team yake mpaka kufika fainal ...
 
Beki Za Egypt watatu wanacheza zamalek na mmoja wa kushoto ahly ahly. Nadhani sababu wachezaji wao wengi hawataki kwenda ulaya kucheza pia gabaski nae ilikuwaje akawa kipa namba 2?

Kuna kale ka jamaa cha Senegal kanapiga beki ya kulia kalikosa penalty ni moto aseeh yupo vizuri Sana kiufupi team zote mbili mbavu zao kulia na kushoto zilikuwa fiti Sana..

Lakini tukubali elneny alipotezwa na gueye vibaya Sana.. Mpaka trezeguet alipoingia akawa anashuka chini kusaidia..
Anaitwa bouna sarr yupo bayern Munich
 
Wakuu nina maswali


Kwanini Algeria kwenye mashindano haya alivaa shati katika Ina badge ya fifa timu nyengine hazikufanya hivyo ?



Je kuchukua afcon unaweza fuzu mojakwamoja world cup ?
 
Asanten sana wanangu wa Senegal Hakika mmeifanya siku ya Leo kuwa mzuri sana, nimpongeze mtoa mada kwakwel umejitajidi sana kuweka update za kinachoendelea Ubarikiwe sana hata sisi tusioenda vibanda umiza tumeumizana humu humu hahaha, niwape pole mlioumia ndio mpira hata sisi tuliumia hivyo hivyo timu zetu pendwa zilipotolewa usifikir tulipenda kuhama hama hapana, Ila yote Kwa yote tumepata burudani, Nipende kukushukuru wewe uliyetumia bando kuuchangamsha Uzi huuu wengine milikuwa mkipita Kimya Kimya mbarikiwe sana. Basi Kwa niaba ya fundi mitambo na clue nzima ya matangazo iliyoongozwa na kiongozi wetu muanzisha mada, tufunge ukurasa huu wa kwanza na tufungue wa pili kuzichambua timu zetu kama zitatoboa world cup
 
Wakuu nina maswali


Kwanini Algeria kwenye mashindano haya alivaa shati katika Ina badge ya fifa timu nyengine hazikufanya hivyo ?



Je kuchukua afcon unaweza fuzu mojakwamoja world cup ?

Amechukuwa ubingwa wa Fifa arab cup, may be ndiyo nembo yenyewe iyo, lakinii cna uhskika
 
Baada ya mashindano ya AFCON22 timu za Afrika zinajiandaa kwa WC Qatar.
Katika timu 10 za Afrika zilizofuzu mchujo wa mwisho wa kupata timu 5, ni nchi moja tu DRC ambayo haikushirikia AFCON Cameroon iliyoisha leo.

Kwa maana nyingine tumeziona timu 9 (ukiondoa DRC) zikionyesha nguvu zao ikiwa zitafuzu WC.

Kwa mtazamo binafsi katika timu zote zilizoshiriki AFCON, Ivory Coast ndiyo iliyoonyesha soka kubwa ambalo kama ingefuzu WC nina uhakika ingesumbua, bahati mbaya haimo katika 10

Tuziangalie timu 10 zitakazotoa 5 kuelekea Uarubuni kwa WC

DRC- Ukiacha mechi za kufuzu ambazo imetumia wachezaji wa kulipwa hatuwezi kupima uwezo wake, haikushiriki AFCON. Tunabaki kuamini tu kama itafuzu ina wachezaji wa kulipwa

Nigeria- Ni dhaifu sana ukilinganisha na zilizowahi kushiriki WC. Haina mpangilio wa soka, wachezaji wanatumia vipaji na uzoefu wao bila team work

Tunisia- Mchezo wao ni ule ule wa kila mara, haina timu ya kutisha lakini ina timu ya matumaini

Ghana- Ina timu mbovu sana kama itafuzu WC inahitaji kubadili mchezo na hata wachezaji.
Kama itafuzu WC haivuki hatua ya kwanza. Ghana imepoteza ile ''total football'

Cameroon- Ina timu nzuri sana hasa viungo na beki, haina forward ikimtegemea Aboubakary.
Abou akiwa chini ya ulinzi Camroon imezima. Ikifuzu WC inaweza kuingia 16 lakini si zaidi ya hapo

Egypt- Ina timu nzuri hasa ulinzi. Wanacheza 5-4-1 wakimtegemea Salah.
Kama Cameroon, ukimweka Slaa chini ya Ulinzi Egypt haina kazi.

Mali- Wanatumia nguvu sana kuliko maarifa, hawana mashambulizi ya kupanga.
Si timu ya kutumainia WC kama itafuzu.

Morroco- Wana timu nzuri pia lakini ushambuliaji wao si mzuri.
Wana viungo wazuri na hutegemea sana ''winger' . Kwa mipira ya kudondosha, ni ngumu sana kuzifunga timu za Europe. Ikifuzu WC inaweza kuingia 16 si zaidi ya hapo

Senegal- Ina timu nzuri lakini beki yake inakatika sana. Inahitaji kuimarisha eneo la kiungo na kuacha kumtegemea mshambuliaji mmoja tu. Ikifuzu inaweza kuingia 16 si zaidi ya hapo

Algeria vipi mkuu?
 
ni nani huyu mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Star wa Cameroon kwenye World Cup ya 1990 pale Italy.

Alikuwa kashastaafu kabla ya Rais Paul Biya kumuomba aiongezee nguvu timu ya taifa ya Cameroon iliyokuwa inaenda kwenye michuano hiyo.

Basi kama ilivyo ada, kauli ya Rais ni sheria, Roger Milla akarudi timu ya taifa na mechi ya ufunguzi, Argentina bingwa mtetezi dhidi ya Cameroon, Roger Milla akafunga goli huku Cameroon ikiishangaza Dunia kwa ushindi wa 1-0.

Shangilia yake kuelekea kwenye kibendera ikampatia umaarufu mkubwa na ni icon ya mojawapo ya World Cup ya 1990

Kutokana na ushujaa huo, mwanamuziki nguli kutoka DRC, Pepe Kalle katika albamu yake ya Gerant akamtungia Roger Milla kibao ambacho mpaka leo kimebaki na umaarufu wake!!

Nafikiri umemsoma sasa Roger Milla kwa ufupi
 
Mwez ujao hawa Mashujaa wanakutana tena kutafuta Qualification ya wc
Screenshot_2022-02-07-13-47-51-09_92b64b2a7aa6eb3771ed6e18d0029815.jpg
 
Sijui kwann hachezi ulaya
Waarabu ndicho nachowapendea hawana time na mzungu....angalia hata akina aboutrika n.k ni mafundi haswaa lakini hawakuwa na tamaa ya kwenda nje, nationality yao ndio kitu cha kwanza, na wala hawaringi
 
Mwez ujao hawa Mashujaa wanakutana tena kutafuta Qualification ya wcView attachment 2111237

Kwanini walioongoza kundi kwa maana nafasi ya kwanza na yapili wasipite moja kwa moja w/c


Just think timu zinazokutana ni bora, Algeria, Morocco, Senegal, Egypt, Nigeria, Cameroon n.k.....moja ikishinda inapita na nyingine inabaki, kwa maana timu chache sana zitakazoshiriki....ebu niambie timu kama Algeria na morocco wakimiss, timu ipi tutegemee itatuwakilisha na kufanya vyema!! Sijajuwa FIFA wana malengo gani kwa timu za Afrika
 
Waarabu ndicho nachowapendea hawana time na mzungu....angalia hata akina aboutrika n.k ni mafundi haswaa lakini hawakuwa na tamaa ya kwenda nje, nationality yao ndio kitu cha kwanza, na wala hawaringi
Alafu Ulaya wanatoa matimu mengi mengine hata hayaeleweki.

Afrika tupewr timu kumi, nchi zipo 54 na timu zilizo competitive ni zaidi ya 15,
 
Back
Top Bottom