JamiiForums
JF Official Account
- Nov 9, 2006
- 6,229
- 5,285
Zimesalia siku 10 pekee kabla ya kukabidhi zawadi kwa Washindi wa Shindano la Stories of Change 2024. Mwaka huu Washiriki walionesha 'Nguvu ya Kalamu' zao kwa mawazo, maoni na michango ya kipekee kuhusu 'Tanzania Tuitakayo' wakilenga kuiboresha sekta mbalimbali Tanzania kwa Miaka 5-25 ijayo Kiuchumi, Elimu, Afya, Teknolojia, Kilimo n.k.
Siku hiyo pia itakuwa ni ya kuwatambua Waandaji Bora wa Maudhui kutoka hapa jukwaani JamiiForums.com na kuwatuza kwa mchango wao Mkubwa katika Majukwaa.
Shindano lilianza rasmi Mei 1, 2024 na kufikia ukomo Juni 30, 2024, ambapo baada ya kupitia maandiko yote, Majaji wamehitimisha kazi yao na kuwachagua Washindi ambao watakabidhiwa rasmi zawadi zao Septemba 21, 2024.