Ha ha haKwenye Katiba kumeainisha vitu ambavyo ni vya muungano na vingine sio vya muungano, mfano mafuta na gesi au madini, wazanzibari wanadeka sana na huyu mwenzao kaja naona ndio ameamua kuwabeba muda sio mrefu atatuletea habari za Chato nyingine.
Huu muungano sio koti alisema Karume, kuendelea nao ni kujiumiza vichwa bure, hao marais wenyewe wanatoka Zanzibar kuja kututawala bara, kwanini siku nyingine asitoke Rais bara akatawale Zanzibar?
Uko sawa 4% ni ndogo sana kwa Zanzibar.Usichokifahamu ni kwamba TRA wanakusanya kodi hadi Zanzibar. Ndio maana sheria inataka 4% ya mapato yote Tanzania iende Zanzibar. Tena hio 4% kwa maoni yangu ni ndongo ingepaswa walau 15%.
Hapo ndio huwa nauchukia huu muungano, angalia wabunge kutoka zanzibar hivi wako Dodoma kwa kazi gani ? kutunga sheria ambazo hazitumiki zanzibar? kujadiri budget ambayo haitumiki zanzibar !! yaan naona wamekuja bara kuchuna tuu.Kodi yote inayokusanywa na TRA Zanzibar hubaki Zanzibar, hakuna senti inayovuka maji
Wakati huo huo wafanyakazi wa TRA Zanzibar ambao wote ni wazanzibar wanalipwa na TRA Taifa (ambayo mapato yake yanatokana na jasho la watanganyika)
Umedadavua vizuri mkuu, je wabunge kutoka Zanzibar wanafanya nini Dodoma nisaidie tujue faida zao kwa bara.chapwa24 Sheria inaitaka serekali ya muungano iipatie Zanzibar 4.5% ya misaada yote pamoja na Bakia la Pato la Muungano.
Swali la kwanza ni kua Bakia la pato la Muungano ni lipi? Pato la muungano ni yale mapato yote yanayokusanywa na jamhuri katika mambo ambayo yamo ndani ya muungano kisheria.
Inavyotakiwa ni kuwa baada ya mapato yote kukusanywa, fedha inatakiwa itumike kwenye Budget ya mambo ya muungano, fedha yote itakayobakia inatakiwa igawanywe kwa washirika wa muungano. Kwahiyo Zanzibar wanatakiwa wapate 4.5% na Bara wapate 95.5%
Mfano: kama mapato ya mwaka ya source zote za Muungano ni milioni 120. Halafu Matumizi ya muasuala ya Muungano kuanzia mishahara pamoja na miradi mambo mengine ni milioni 20. Kwahiyo itabakia milion 100, Sasa hiyo mia itatakiwa igaiwe Zanzibar wachukue milioni 4.5 na Bara wachukue milion 95.5. Sasa tatizo lnakuja kuwa Bara hawajawahi kuwalipa Zanzibar stahiki yao ya mgao wa mapato kwa miaka yote hiyo. Pesa zote wanachukua wao, na ndio mana Zanzibar wanalalamika na ndio moja katika kero kubwa za muungano.
Swali jengine linalokujia wewe ni, Kwanini Zanzibar wapewe mgao wa fedha wakati wewe huuoni mchango wao kwenye hayo mapato?
Mtu yoyote anaetaka kuja Tanzania anlipia visa, Pesa ya visa direct inaingia kwenye mfuko wa Muungano. Zanzibar kwa mwaka kunakwenda watalii wasiopungua laki 3, hawa malipo ya visa zao zote zinachukuliwa na Bara, Zanzibar haifidika na hela visa ya watalii wanaokwenda kwao.
Ma company yote ta TZ, kuanzia ya mitandao ya simu, ving'amuzi, Mabenk na mengineyo, Yanasajiliwa Bara, lakini yanafika mpaka Zanzibar kutoa huduma bila kulipa kodi yoyote kule Zanzibar. Yani ni hivi Voda wanalipa Kodi Bara lakini wanatoa huduma mpaka Zanzibar. Fedha wanazolipia za kodi ni kwa ajili ya kutoa huduma mpaka Zanzibar, ila sasa TRA hawagawi mgao wa fedha zinazotokana na makampuni kwa Zanzibar.
Hiyo ni mifano miwili na ipo mengi tu kwenye kila sekta inayohusu Muungano.
Kwa kifupi wanachokifanya Serekali ya SMT, ni wizi wa mchana kabisa, Kila mwaka wanawaibia Zanzibar karibu 1 trillion. kwa kipindi cha miaka kumi kiharaka haraka Zanzibar wanaidai Tanzania fedha isiyopungua Trillion 10.
Huo ndio ukweli wenyewe fedha zote zinazokusanywa na TRA tawi la Zanzibar hubakizwa Zanzibar kama ulikua hujui anza kufuatilia sasa bunge la bajeti la mwaka wa fedha 2021/2022
Zanzibar ni kupe kwa Tanganyika
Umedadavua vizuri mkuu, je wabunge kutoka Zanzibar wanafanya nini Dodoma nisaidie tujue faida zao kwa bara.
Hawa watu hata umeme wa kutoka bara hawaulipii na hawana mchango wowote wa kustahili hiyo asilimia,si wanajifanya wana mafuta na mafuta sio suala la muungano sasa wameona mama ametoka kwahiyo wanamtega, hawa ni waroho na walafi wanapenda sana kujiangalia wao,sisi tukihamia kwao wanakuwa wa kwanza kulalamika ujinga mara oh wao wana ardhi kidogo wakati wao wamejazana huku bara,hawana tofauti na mtoto aliyedekezwa sasa akinyimwa hata peremende basi hulia na kugalalagala chini ili tu apate attention kutoka kwa wazazi wake. Na wamesema kwa miaka 30 hilo suala halijapatiwa ufunguzi ,kwa hiyo leo ndio wameona ni muda wa kupata ufumbuzi ,tatizo hao wanaobweka tayari wanajiona chama cha zambarau kina madaraka huko Zenj.Kuna hoja nimekuta watu wanaongea, ni kuhusu kile ambacho mama amesema waziri wa fedha akakae na mwenzake wajadili na kusuluhisha katika kero za muungano. Ninaupenda sana Muungano,ninauunga mkono. lakini, nilijiuliza kitu kimoja, mimi kama mtu wa bara sitaki tupigwe pia kama wazenji wasivyopenda kupigwa.
1. hivi Zanzibar inachangia kitu gani kwenye kwa Tz bara kinachowastahilisha tuwagawie hiyo asilimia? Bara inafaidika nini toka Zanzibar?
2. Mgao unaoongelewa ni wa misaada toka nje, au ni mapato ya nchi (pato la madini bara, TRA, navitu vyote vya bara)?
3. kama ni mapato ya nchi, kwani TRA haipo Zanzibar ya kikwaokwao?
4. proportion ya wingi wa watu + ukubwa wa eneo vinazingatiwaje wakati wa kugawa pato ya muungano?
5. kwanini marais waliopita walikuwa hawashughulikii hilo jambo, kulikuwa na kitu gani walichokiona? including one of them who was Zanzibari.
6. kwa anayeelewa, naomba anieleweshe hili jambo kwasababu kama vile tu zanji wasivyopenda kupigwa, mimi kama mtu wa bara pia sipendi na sikubali.
Naongea hivi kwasababu watu wanavyoongea mtaani wanaongea kama vile kwasababu mama ni mzanzibar basi wanaona wazanzibar wanaweza kupitisha vitu vingi sana ambavo vilikuwa havipiti kwa awamu za nyuma ambazo nyingi hazikushikwa na rais wa zanzibar.
MWISHO: siongei kwa ubaya, wala kwa unafiki, ila ninaongea kinachoongelewa mitaani. Ninamwamini mama atafanya makubwa. Ila naamini tunatakiwa kuwa na busara ya hali ya juu kwasababu kuna mambo tunaweza kufanya tukifikiri tunajenga muungano kumbe ndio tunauweka kwenye mazingira ya kubomoka kabisa.
Wewe ndio muongo nyie wazenj ni wabaguz sana na mnachukia sana watu wa bara wakati na nyie ni wahamiaji tu huko kisiwani.Sio vizuri kwa mtumzima kuwa muongo
Wewe ndio muongo nyie wazenj ni wabaguz sana na mnachukia sana watu wa bara wakati na nyie ni wahamiaji tu huko kisiwani.
Samahani mkuu,Ninaupenda sana Muungano
Na huu ndio ujinga tunaouzungumzia kila siku. Eti halafu na wewe ni msomi.Msaada sawa kama haujalenga eneo maalumu. Mkopo si unachukuliwa kufanya kitu husika. Mkopo wa kujenga stigilazi ZNZ wa gawiwe wa nini? Hili la mkopo wasaidiwe kwa kudhaminiwa kama watakuwa na mkakati wa kuulipa.
Haya mambo yapo kwenye makubaliano ya mambo ya Muungano.Wanaitwa wanga ukitaka kuwa mkweli. Lakini roho mbaya ni hao waliosema mafuta yetu haya wahusu Watanganyika hapa napo kama utataka kuwa mkweli wa nafsi yako na kuukataa unafiki kama dhambi.
Sasa mkuu hakuna huo msaa wa JM Tanzania kwa ajili ya hospital ya Mnazi mmoja.Msaada ambao ni general kwa Tanzania ni sawa. Kwa mfano msaada wa vyandarau kwa Tanzania wa chukue 4% yao. Lakini msaada kwa Serikali ya JM Tanzania kwa ajili ya Hospital ya Mnazi mmoja ZNZ utapiga 96% ya huo msaada ije Tanganyika?
Tugawane vitamu na vichungu.Binafsi sina shida kama hiyo 4% itahusisha mapato na madeni. Kama ni mapato tu, hapo kuna tatizo.