Kaka bado unakosea sana, Alshabaab hawachanganyiki kabisa na raia, jaribu kuuliza. Alshabaab kuna maeneo na miji ndani ya Somalia ambayo yapo chini ya Jeshi la Alshabaab na yanajulikana kabisa, kama ambavyo walikuwa wameshikilia bandari ya Kismayu wakati Uganda wameshikilia Mogadishu. Tafdhali ondoa mawazo kwamba Alshabaab wamechanganyika na watu, wangewezaje kuwa na silaha kubwakubwa kama magari ya kivita na vifaru walivyovikamata toka majeshi ya Kenya na Burundi walipovamia kambi zao?, wangewezaji kukusanya kodi toka kwa raia ili waweze kupata pesa za kuendesha vita?, wangewezaje kuendesha biashara ya mkaa kwa kiwango kikubwa kiasi hiki kama wamejificha ndani ya raia?.Kumbuka sasa hivi Somalia imegawanyika kama Syria, kuna maeneo yapo mikononi mwa Kenya(kusini), Uganda(katikati,), Burundi(kusini magharibi), Alshabaab( katikati na kaskazini magharibi). Djibout and Ethiopia(kaskazini na kaskazini mashariki). Ninajua utashangaa kwanini wasivamie hayo maeneo yao wakawatoa haraka, hilo ndilo swali ambalo kila mtu anajiuliza.