A/C katika gari imeundwa kwa Vifaa kadhaa vinasaidia kuleta ubaridi

A/C katika gari imeundwa kwa Vifaa kadhaa vinasaidia kuleta ubaridi

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
FB_IMG_1521838788834.jpg

A.C KATIKA GARI IMEUNDWA NA VIFAA KADHAA AMBAVYO VYOTE KWA PAMOJA UFANYA KAZI YA UZALISHAJI WA BARIDI KATIKA GARI

1.A.C COMPRESSOR
Kifaa hiki kinatumika katika ufuaji wa ubaridi katika A.C.

2.A.C CONDENSER
Kifaa hiki hutumika katika upoozaji wa gesi katika AC

3.A.C EVAPORATOR
Kifaa hiki hutumika katika kugandisha ubaridi kwenye mfumo wa upoozaji.

4.EXPANSION VALVE
Kifaa hiki hutumika katika kulinganisha gesi ya kiasi kikubwa na kiasi kidogo.

5.RECEIVER DRIER
Kifaa hiki hutumika katika uchujaji wa gesi katika A.C

6.HIGH PIPE
Kifaa hiki hutumika katika kupitgisha gesi kwenye mfumo wa A.C ikiwa ya moto.

7.LOW PIPE
Kifaa hiki hutumika katika kupitisha gesi kwenye mfumo wa A.C ikiwa ya baridi

8.THERMOSTART
kifaa hiki hutumika katika kupumzisha compressor pindi hewa inapokuwa kali(baridi sana au joto sana).

9.AC FILTER
Kifaa hiki hutumika katika kuchuja vumbi lisiingie ndani ya gari na kuchafua mfumo wa hewa.

10.BLOWER FAN
Kifaa hiki hutumika katika kutengeneza hewa na kupeleka katika overporator.

11.SPEED CONTROL
Kifaa hiki hutumika katika kuongeza na kupunguza kasi ya blower fan.

12.CONDENSOR FAN
Kifaa hiki hutumika katika kusaidia kupooza condensor ili ipishe gas kwa wepesi

14.COMPRESOR A.C OIL
Ni mafuta yanayosaidia katika ulainishaji wa ndani ya piston.

15.VACUUM SILENCE
Kifaa hiki hutumika katika kupandisha na kushusha ukimya (silence) na sauti ya injini pindi uwashapo A.C.

16.PRESSURE SWITCH
Kifaa hiki hutumika katika kuwasha compressor na feni ya condenser pindi uwashapo A.C.

"Elimu kuhusu usalama barabarani ni jukumu letu sote"
 
shuleni tungekuwa tunafundishwa hivi kwa lugha yetu.tusingefeli.
Ingekuwa hii nchi siyo tengemezi sawa kama ni tengemezi wacha tuendelee kutumia lugha ya wakoloni kufundishia...
 
Hapa naomba wataalamu wa magari wakupe maelezo ya kina.
cc
Rrondo
Mshana jr
 
Tofauti ya kiwango cha mafuta kinachotumika AC Ikiwashwa na isipowashwa ni kidogo sana.
Jibu ni ndiyo! Kwa sababu unapowasha Air conditioner kwenye gari unaiongezea engine mzigo wa kusukuma/kuzungusha compressor! Inakuwa kama gari inapanda mlima hivyo kuifanya engine ilazimike kutumia mafuta mengi zaidi ili kupata nguvu ya kusukuma!! Kiwango cha mafuta kinachoongezeka kinatofautiana kwa gari moja na jingine!
 
Back
Top Bottom