A day in the Buddhist college

Kwa kiasi fulani nimeongelea ishu za ajabu ajabu lakini ndani ya Buddhism kuna mengi mazuri na yenye faida nyingi, namaanisha Buddhism kama philosophy na sio kama dini

1: CHAKULA
hiki ni kitu kinachoheshimiwa mno ndani ya Buddhism, sio kila mtu ana Neema ya kuenjoy utamu wa chakula, ale ashibe
Ndani ya Buddhism chakula ni ibada, na mikalangizo yote ya chakula ni kwasababu ya kiungo kidogo sana ULIMI, lakini ndani ya Buddhism chakula ni dawa chakula ni ibada kwahiyo hatupaswi kuchagua chakula
Huwa kuna kitu cha ajabu sana na cha kijinga nakiona sehemu nyingi...!!!! Watu kubakisha chakula.. Ndani ya buddhist college ilikuwa ni mwiko mkubwa kubakisha chakula... Pakua unachomaliza, usile ukabakisha hakuna aliye tayari kula makombo, lakini vilevile ni kwamba wakati wewe unabakisha kuna mtu anahitaji japo robo ya hicho ulichobakisha...TAFAKARI

2:MAJI
Hapa Africa tuna matumizi mabaya sana ya maji, hatujali serikali haijali viongozi hawajali...tunapoteza maji mengi mno kwa upuuzi tu...Maji ni uhai Maji ni kila kitu, kila tone la maji lina thamani na maana kubwa mno....yaheshimu Maji yatunze
 
Unamaanisha meditation? Maisha yetu chuoni yalijaa meditation lakini ile ya kukaa kimya kwenye lotus posture (yenye maumivu mengi sana) ilikuwa ni dk 50 kila siku lakini pia tulikuwa na meditation retreats za siku 3,5 na 7

Levitating??
 
nilipata kuwa huko mwaka 2001, jina langu la dhama ni ben yue
 

3: KANUNI YA IMPERMANENCE
Kwamba hakuna kidumucho milele, lakini kwenye hili tuna shida moja kubwa sana, tunavyovipenda tunatamani viwepo milele, tusivyovipenda tunatamani vituondoke mara...! Hii kanuni inayomtesa sana mwanadamu.. Laiti tungekuwa na ufahamu wa kutomiliki milele matatizo mengi sana Africa yasingekuwepo hasa kwenye siasa

4:COMPASSION AND LOVING KINDNESS(HURUMA NA UPENDO)
hili wengi tunalikosea tangu ngazi ya familia mpaka kwenye Jamii, unaonyesha UPENDO kwa mtoto kwa kumpa pesa nyingi za matumizi bila kutafakari atazitumiaje
Unampa teja pesa bila kujua kuwa unaelea tatizo
Unashindwa kukemea uovu kisa tu unaogopa kuonekana mbaya kwenye familia au Jamii au kwakuwa una maslahi na huo uovu
Buddhism inafafanua vifungu vingi kwenye misahafu yetu ambavyo havikufafanuliwa
 
Ok tajaribu kufanya hivyo japo nyingine zipo jukwaa la dini ambapo ni wachache wana access ya kufika huko

hivi mkuu ili kufika jukwaa la dini kuna kujiregister tena kwa Ajili ya jukwaa hilo au inakuaje coz mi kila nkifungua huwa hapafunguki
 
Levitating??

Ulieza ku-levitate mkuu???

Hii ishu ya levitation kuna mdau humu aliniita muongo na kwamba chuo chetu ni feki...lakini bado naomba niseme tena sisi hatukujifunza levitation... Buddhism ina sects nyingi kama Mahayana, Vajrayana na Theravada lakini vilevile hata Taoism na Conficious zote zinahusishwa na Buddhism bila kusahau Krishna/kshna consciousness
 

Ila mwenzangu we una moyo. Mi kuelezea mambo ya kule kwa watanzania nahisi ni mpaka ipite miaka kama 150 hivi ndiyo watanzania wa kizazi hicho wataweza kunielewa kidooogo!. Ila hongera sana.
 
Ila mwenzangu we una moyo. Mi kuelezea mambo ya kule kwa watanzania nahisi ni mpaka ipite miaka kama 150 hivi ndiyo watanzania wa kizazi hicho wataweza kunielewa kidooogo!. Ila hongera sana.
Infopaedia nipende tu kusema kuwa nashukuru mno uwepo wa JF , sehemu ambapo tunaweza kuongea kwa uhuru na uwazi... Imenichukua zaidi ya miaka mitatu na kujishauri kwingi sana mpaka kuleta hii habari lakini vilevile nikiwa makini kusimulia bila kuharibu
Kinachonipa faraja zaidi ni kwamba kumbe kuna members humu tuliokuwa pamoja kule...ningeongeza chumvi hakika ningekosolewa maramoja
 
Last edited by a moderator:

Sasa kwa sisi wenye akili finyu na zilizoko kwenye majitaka, hii sutra ina uhusiano gani na KARMA-SUTRA. Nyie mmesema kuwa huko hakukuwa na MAMBOZ, sasa hizi SUTRA zinaingiaje wakuu Infopaedia na Mshana Jr.

LOL.
 
Last edited by a moderator:
Pouwa witnessj nimekupenda bure mdada

Hapa naona CHAKRA au SUTRA imeingia, witnessj. LOL

I am sorry, I am just messing around.

Lakini kwa kweli mkuu mshana jr nimelipenda hili bandiko lako. Mimi nimejifunza the philosophical approaches za dini zote hapa duniani kutoka Atheism mpaka Zoroastrianism. Lakini sijaingia kwenye mambo ya jikoni ya hizi dini isipokuwa UKRISTU, UISLAMU, na UYAHUDI. Kwa hiyo nimefurahi sana ulipofungua ka-mwanya kadogo sana katika hii imani ya BUDDHISM.

Asante.
 

Nimekusoma mkuu
 
Naona hapo ume-confuse them (changanya) kila kitu kupata dini yako mwenyewe. Hii dini yako yakuamini kila kitu inaitwaje?

Sasa, kama usipoongeza ufahamu wako katika maisha (life experience and knowledge) pamoja na dini yako uliozaliwa nayo (ya wazazi au walezi wako) basi wewe hutakuwa na muamko wa kiroho (a spiritual awakening) bali utakuwa unafuata imani (dogma) tu. Pengine mkuu mshana jr amekwisha kujibu.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…