A man's life summarized in three pictures

Matokeo ntakupa asee, yaani bila ubishi. Aaah wapi kwani mi mchezaji wa simba au Yanga nishindie chipsi mayai?
Mi napiga vyakula vya uhakika sio vya ki-dada du na kisharobaro..🙂

haya bana nita kupm saa kumi na mbili na nusu kupata matokeo. mkuu.
 
i thought it was supposed to be virse versa
Yeah, you are right, mimi kabla sijaona nilikuwa nyonde nyonde, lakini baada ya kuoa, nimekuwa na siha nzuri mpaka vibinti vinanitizama kwa matamanio..................!
 
Yeah, you are right, mimi kabla sijaona nilikuwa nyonde nyonde, lakini baada ya kuoa, nimekuwa na siha nzuri mpaka vibinti vinanitizama kwa matamanio..................!

ha ha ha ha ha ha ! lol u have made my day Mtambuzi. hongera sana kwa hilo yelekea wewe uko kanaani na hao wengine bado wako misri.
 
Last edited by a moderator:

Hahahaaa.... Umeniacha hoi maana hata mimi sometimes huwa nawaza kama wewe..
 
Hahaa! Huyo wa katikati nimempenda sana. Inaonekana ni jogoo wa kazi mpaka kanyonyoka; yaonekana kazoea suluba. Huyo hawezi kupata mdonde huyo kwani yu imara sana kwa sababu ya mazoezi ya kila siku. Huyu wa kwanza japo ni mnene, kanawiri lakini ni legelege. Wa mwisho sina comment.
 
im still single boy nikirudi nyumbani inabidi nijiangalie kwanza kabla sijafanya maamuzi lol. kama ni mtindo huo ila mtoto nahitaji
 
Mama Mdogo umetisha watu huku, to you single guys out there dont worry kama alivyosema Mtambuzi its vice versa.
 
Last edited by a moderator:
Nimempenda huyo divorced amejazia.


But naked lol.
Nabakia single, maana ni kweli kwa sasa nipo kama picha namba moja.
Nafanya kile nataka kwa muda ninaopenda.
 
Mama Mdogo umetisha watu huku, to you single guys out there dont worry kama alivyosema Mtambuzi its vice versa.

Hili bandiko nimeliweka kwa nia njema siyo kumtisha mtu, nimelileta ili watu wasome hiyo hali halisi kifani (model), waji-fitishe, watafakari kulinganisha na hali halisi,na baada ya hapo wachukue hatua muafaka kufanya damage control. Ni hicho tu, maisha yenyewe yamejaa stress, unategemea stress zitapungua ukioa/olewa? Je hali itakuwaje ukiwa mtalaka/mjane baada ya kuzoea stress zako na za mwenzako, halafu anakuwa hayupo? Kwa hiyo hizo picha za jogoo anayeendelea kupigika ndiyo hali halisi. Ni mambo mdundo ki-stress kwa kwenda mbele!!!
 

Well said Mama Mdogo ukweli mtupu.
 
Last edited by a moderator:
Nimempenda huyo divorced amejazia.
.
MadameX Mimi alieniacha hoi ni huyo MARRIED! ... yaani anatembea kwa maringo! anadundadunda huku akijidai ... anajaribu kujitutumua lakini wapi! ... maisha yamejaa stress za kila aina ... za kazini, mke, watoto! ... LOL!
.
 
John Gottman, mtaalamu anayeheshimika katika masuala ya ndoa, anaripoti kwamba, ndoa yenye matatizo, inaweza kuongeza uwezekano wa kukuletea magonjwa kwa asilimia 35! Anaamini kwamba kuitumikia ndoa yako kila siku itakusaidia zaidi kwenye afya yako au kuishi maisha marefu kuliko kutoishughulikia na ukajikuta ni mtu wa kuumwa hovyo.

Ingawa wengi wetu tunaamini kwamba hasira ni chanzo kikuu cha uhusiano mbovu, Gottman amegundua kwamba siyo hasira pekee ambazo ni tatizo, bali ni vipi tunatatua migogoro yetu kwenye ndoa. Kutoa hasira kwa nia ya kujenga kunaweza kufanya maajabu kwa kusafisha hali ya hewa na kuurejesha uhusiano kwenye njia yake. Hata hivyo mitafaruku huwa ni tatizo kukiwepo mambo manne ambayo ni: Kumshambulia mwenzio, (kuponda), dharau, kujitetea badala ya kuomba radhi kwa nia, na kunyamaza unapoongeleshwa na mwenzio.

Kuponda ni nini? Kuponda kunahusu kumshambulia mwenzio bila kujali utu wake, mahali na muda.

Ni vema kila mmoja wenu akatoa dukuduku lake, lakini usimponde na kumshambulia mkeo au mumeo, wakati mwingine mbele ya watu wengine au hata watoto.

Dharau nayo? Dharau ni hatua moja ya kumponda mwenzi wako na inahusisha pia kumuumiza. Dharau ni alama ya wazi ya kutomuheshimu mtu.

Mfano wa dharau ni pamoja na kumshushia hadhi, kukunja uso, au kumchanachana mwenzio kwa vicheko vya kebehi. Tabia hii wanayo zaidi wanawake.

Kujitetea na kutafuta visisngizio je? Kujitetea wakati ugomvi umepamba moto linaonekana ni jambo jema, lakini hakusaidii kuurejesha uhusiano mahali muafaka. Mtu anapojitetea au anapotafuta visingizio, mara nyingi anakuwa kwenye mfadhaiko mkubwa na hivyo kushindwa kusikiliza vema mambo yanayoongelewa. Kukataa kuwajibika kwa makosa yako na kutafuta visingizio ni aina mojawapo ya kujitetea.

Kunyamaza nako? Mtu anakataa kuitikia. Kwa kawaida kunyamaza kunaweza kusiwe kubaya, lakini katika masuala ya uhusiano, kunyamaza wakati wa mtafaruku kunaweza kuhatarisha ndoa yenu. Kama ni mwenye kawaida ya kunyamaza, unajiondoa mwenyewe kwenye ndoa, badala ya kutatua matatizo yenu. Wanaume wana tabia ya kunyamaza zaidi ukilinganisha na wanawake.

Kwa kweli, kwa mujibu wa utafiti wa Gottman wa matatizo manne yaliyotajwa hapo juu ni kwamba, yakibobea katika ndoa yanaweza kutumika kutabiri, kwa usahihi kwa zaidi ya asilimia 80, wanandoa wepi ndoa yao itavunjika.

Majaribio ya kutosha yakifanyika bila mafanikio kujaribu kuokoa ndoa iliyopata dhoruba ya mambo manne yaliyotajwa hapo juu, kuna uwezekano wa zaidi ya asilimia 90 wa ndoa kuvunjika.

Mbinu za kuboresha ndoa na afya yako. Ukizingatia kwamba, kuwa na ndoa imara ni kitu muhimu sana ili kuwa na afya na furaha, italeta mantiki kuelekeza nguvu zenu katika kuifanya ndoa yenu kuwa bora zaidi. Hapa chini kuna vidokezo kwa ajili ya kuifanya ndoa yako kuwa na afya zaidi:

Kwanza lea ndoa yako. Unajua mambo ayapendayo na asiyoyapenda, ndoto, hofu, wasiwasi, na matumaini ya mwenzi wako? Unajua kwa mapana ni nini mwenzi wako alifanya siku nzima ya jana? Unajua aina zipi za shinikizo mwenzi wako anazipata mahali pake pa kazi? Msingi wa ndoa nzuri ni urafiki imara.

Kama ndoa haijajengwa juu ya urafiki imara, itakuwa shida kuishi kwa pamoja kwa muda mrefu. Hakikisha unapata muda kila siku kukaa na mwenzi wako kwa siri ili kumjulia hali na matatizo aliyokabiliana nayo .

Katika vipindi hivi, weka kipaumbele kusikiliza na kujifunza kuhusu fikara, mawazo na hisia za mwenzi wako .

Pili kwa nguvu zote na kwa makusudi, chukua hatua kuboresha mapenzi kwa mwenzi wako. Gottman anasema, hiki ndicho kizuizi kikubwa cha dharau. Kumbuka mambo mazuri ya mpenzi wako.

Ulimpendea nini hadi ukaoana naye? Ni kitu gani kabla hujamuo kilikuvutia kwake kimaumbile? Kwa kurejesha mapenzi kwa mwenzio utakuwa umeboresha mwenendo bora.

Tatu, daima mheshimu mwenzi wako. Katika uhusiano ambao unaporomoka, heshima kamwe haipatikani.

Cha kusikitisha zaidi, wakati mwingine watu wanaishia kuwatendea wenzi wao vibaya zaidi kuliko ambavyo wangewatendea watu wasiowafahamu. Unamgombeza mkeo au mumeo mbele ya rafiki zako au familia?

Nne, mkubali mwenzi wako. Kumbuka kwamba kila mmoja wenu anahitaji kujisikia anakubalika kama binadamu.

Badala ya kumshambulia mkeo au mumeo, jaribu kusikiliza mawazo yake. Ni rahisi kutilia mkazo makosa ya mwenzio na kwa kufanya hivyo tunasahau mema anayofanya.

Tano, sameheaneni, mwenzio anapokuomba msamaha kwa dhati, usimkimbie au usiompe kisogo, wakati mwingine migogoro haikwepeki.

Majaribio ya kurekebisha kasoro zilizojitokeza katika uhusiano yanapopuuzwa, uhusiano unaathirika.
Usifunge milango moja kwa moja kwa mkeo au mumeo anapojaribu kujirekebisha.

Sita, tulia. Unapokuwa umeudhiwa, pumua kwa nguvu. Watu wengi wanahitaji kama dakika 20 kutuliza miili yao baada ya kuudhiwa. Baada ya kutulia chukua nafasi yako, anza upya kulishughulikia tatizo lililo mbele yako, wakati umetulia na utakuwa tayari kumsikiliza mkeo au mumeo vizuri.

Saba, chukulia mambo kirahisi. Ijapokuwa mkeo au mumeo anaweza kufanya mambo ambayo yatakuudhi, kumbuka unaweza kukabiliana nayo.

Si busara kupambana na mkeo au mumeo katika mambo madogomadogo.

Nane, jitazameni upya na kujirekebisha. Uhusiano ni kama dansi. Wewe na mkeo lazima msonge mbele sambamba. Kumbuka kwamba uwe ni mwanamke au mwanaume una udhibiti kwa asilimia 50 wa mambo yote yanayotokea katika uhusiano wenu. Ndio maana wanasema, ndoa ikifa wote mmechangia.

Ni mara chache kupindukia, ambapo mmoja kati ya wanandoa ndiye mwenye mchango.
 
mimi atakayenioa i promise itakuwa vise versa kabisaa mana nitampa mapenzi ya kweli na hatajutia kunioa, nataka mume wangu hata akikaa na rafiki zake aseme jamani nimepata mke mwema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…