A new richmond is coming

Tina

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2007
Posts
572
Reaction score
581

Source: THISDAY, November 30, 2009
 
Ngeleja anatuambia nini sasa.........au ni upumbavu tu ule ule kwa nini kampuni za maana zinazojulikana kwa kazi hizo zipo na hazipewi tender hii? Kwa nini SONGAS wasiruhusiwe wakaongeza uzalishaji wa umeme mpaka ije tena kampuni nyingine?? kuna nini hapo TANESCO??

Sasa naanza kuelewa hoja za zitto
 
hoja za zitto zipi?
 
Nadhani hapa sasa tunaaanza kupata picha halisi. Jitihada zilizopo za kuhakikisha kuwa Dk. Rashidi anabaki Tanesco zina uhusiano na tenda hii mpya. Ni dhahiri kuwa Dk. Rashidi ana unfinished business Tanesco. Kazi zilizobaki kwa Dk. Rashidi ni zifuatazo:

1. Ahakikishe kuwa mpango wa kununua mtambo wa Dowans unafufuliwa tena na kupitisha malipo yote yaliyobaki kwa Dowans.

2. Ahakikishe kuwa tenda hii mpya ya mitambo ya umeme ya Dar na Mwanza ipewe kampuni yao.

Sasa naamini zile tetesi kuwa Dk. Rashidi aliwekwa Tanesco 2006 na RA kwa kushirikiana na EL ili kupitisha madili yao kwenye sekta ya nishati.
 
Tz government + RA will never separate.
 
hoja za zitto zipi?


Zitto amekuwa akisema Dr. Rashidi ni best CEO na anaisaidia sana TANESCO kumbe kuna ajenda nyuma yake ambbao kama Tina alivyosema Dr rashidi yuko pale kuhakikisha RA na EL maslahi yao yanalindwa.......sasa na madudu haya mapya ndo connection inaonekana.
 
Kweli JF sasa tumeishiwa halafu hizi episodes za akina Zitto hazijasaidia kitu kwani nowadays tunaspend so much time kuwajadili wanasiasa na kukopi news from other sources

I mean do you guys remember enzi zile JF ilikuwa ni source ya hizi scoops

Invisible inabidi tufanye emergency restructuring hii ya tabloids kutuzidi kete kila kukicha nayo inaboa..unless JF sasa ishakuwa irrelevant
 

Kuchukua information from other sources sodhani kama ni tatizo kwa sababu si wote wanayasoma magazeti yote ya TZ hasa walio nje ya nchi. Kuhusu kuwaongelea wanasiasa, sioni tatizo juu ya hili kwa sababu tunao wazungumzia yao wanatoa hoja zao hapa JF.

Binafsi naona bado JF ni kiungo kikubwa kwa wanajamii na hasa walio nje kupata taarifa muhimu za nyumbani.

Kuna mwanaJF mmoja anafanya kazi USA kwenye kampuni ya kutengeneza Gas turbines hizi ambazo watu wanataka kufanya u-richmonduli tena. Naomba afuatilie bei halisi ya gas turbines ili tujue hawa richmond wanatupiga kiasi gasi.
 
jamani embu tuelimisheni sisi mambumbu wengine; hivi hawa tanesco si ni shirika la kuvua umeme. Sasa inakuaje tena shirika moja ambalo alitimizi mahitaji yake kugawa tenda kwa shirika lingine kutumia hela yao kusaidia majukumu.

Kwani wao wenyewe hawa wezi tafuta hiyo mitambo na kuboresha huduma zao. Au tanesco wamekua a sub part of ministry of energy na wanagawa tenda as if to create a competition. Yaani hii soap opera sisi wengine tulio ikutia kati aina maana so far labda darasa litatusaidia hapa. au ndio capitalism

Maana kila siku tunaona as if the plot recycles sijui richmond; dowans etc. All to do with tanesco tenders ajizi yenyewe tanesco ni shirika la umeme ambalo linahitaji hiyo mitambo. Lakini kila kukicha linagawa tenda kwa wengine kununua hiyo hiyo mitambo ambayo wao wenyewe hawana au nimekosea.

Like I said it dont make sense to me; darasa tafadhali on why Tanesco has to give money to other companies to purchase the machines that wenyewe hawana na wana hiitaji na kwa nini awawezi fanya wenyewe.
 
Sasa naamini zile tetesi kuwa Dk. Rashidi aliwekwa Tanesco 2006 na RA kwa kushirikiana na EL ili kupitisha madili yao kwenye sekta ya nishati.

Sio Dr Rashid pekee, mimi naamini hata waziri (Mh Ngeleja) pia amewekwa na hao hao!
 
Tina yuko interested na rashid tuuu na sio wengine e.g. ngeleja, chairman of the board na big picture of the umeme saga in tz...kwasababu zake ambazo amezi-hide deep inside...werevu wanajua...
 
Tatizo ni pale tulipokubali kama wananchi kudanganywa kwamba sasa serikali haifanyi tena biashara idea ilikuwa kujenga huu ulaji unaoleta utata leo.Kwa kigezo kwamba serikali haifanyi biashara watu wanafanya mambo yao wanapeana tender za bei mbaya ili kujihakikishia majimbo na mambo mengine.

Umefika wakati tuone kwamba hata huko bungeni ni usanii mtupu, kama hii nchi sio ya viongozi waigizaji uliona nchi gani PM anaagiza kwamba sasa ununuzi wa mashangingi basi hapohapo haupiti muda unaambiwa kuna consignment ya mashangingi 800 ordered by the govt! huu ni utani.

Tuchukulie kwamba hapa JF ni chumbani au msituni mahali pa kupangia mikakati/mashambulizi sasa tutoke humo tuende uwanja wa mapambano, bila hivyo mambo yatabaki hivi hivi ya: WENYE NCHI, WALA NCHI, na Wananchi ambao ni sisi. Tutafute namna ya kupambana na hawa watu hatuwezi kushinda vita tukiendelea kuwepo huku chumbani ni lazima muda wa mipango/mikakati uwe na mwisho vinginevyo tutaja toka humu na kukuta hamna kilicho baki.

SUALA NI JE TUTOKE VIPI?
 
Tina yuko interested na rashid tuuu na sio wengine e.g. ngeleja, chairman of the board na big picture of the umeme saga in tz...kwasababu zake ambazo amezi-hide deep inside...werevu wanajua...

Na huu ni mwanzo tu ... ukiwa na mafisadi kama Rashidi, usiwape muda wa kuvuta pumzi.

Fisadi Rashidi lazima akutane na karma mwaka huu kwa kutangaza kuwa atazima umeme ndani ya mwaka mmoja kama ...... (jaza pengo) .... na akafanya kweli wiki chache zilizopita.
 
huna lolote udini wenu hautowasaidia...mwafrica,ak.a tina
 
Tumain
Tina yuko interested na rashid tuuu na sio wengine e.g. ngeleja, chairman of the board na big picture of the umeme saga in tz...kwasababu zake ambazo amezi-hide deep inside...werevu wanajua...
Ngeleja na Rashidi wote walifanya kazi Vodacom hivyo ni watu wa RA, EL pamoja na Tanil wa Shivacom. Kundi hilo la wajasiriamali/wanasiasa ndio haswa lililo husika na Richmond/Dowans na sasa linawinda tenda mpya Tanesco. Hivyo nakubaliana na wewe kabisa kuwa Ngeleja, Rashidi ni moja ya watu wanaotumiwa na mtandao wa kina RA ili kufanikisha miradi yao.
 
Sasa wana JF mnakosa upeo wa kuchanganua hoja. Kama kila tender ni Richomond, basi mbona nyie hamkuomba hiyo tenda ili mfanye kizalendo? Ingependeza mtu atoe mbadala kulalamika tuuuuuuuuuu, ndio maana kiongozi mmoja kasema kelele za milango hazimnyimi mwenye nyumba kulala. Mgao wa umeme keleleeeee, vifaa kununuliwa keleleeeee, mwatakaje!!!!!!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…