A shock of my life, furaha yageuka shubiri. Be good to people on your way up, you might meet them on your way down, mwenzenu leo yamenikuta!

vijana wanapenda sana kupandisha mabega!
unajua raha sana kupandisha mabega km unayo!!......Lool mie waniumize tuu ikifika zamu yao lkn nitapandisha kwa raha zangu!.....siku ukinikamata nashusha mabega!wala sijipendekezi kazi kwako sasa........

lkn nikikamata tena mabega juu km kawa....sina habari kasimu mpaka kifo...haiwezekani wengine wapandishe mie nishushe mweee! utaniua tu......lazima yaende juu
 

Na bado karma ile ya kumchongea Erick Kabendera....!!!!
 
Sometimes unaweza usiwe mwema lakini kuna vitu vinakuwa havina faida wala umuhimu wa kuvifanya, especially linapokuja swala la utu wa wengine mbele ya maslahi yako binafsi. unaweza usiitwe wema lakini ni normal human empathy and instincts.
Tuseme sawa ungeenda kumuuliza kuhusu uhakika na credibility ya hizo taarifa na kumuomba favors za mambo ya kawaida ya kibinadamu lakini kama angekataa wala usingemlipua sababu bila shaka kulikuwa hakuna ulazima wa kufanya hivyo na leo angekumbuka siku ile basi bila shaka kusingekuwa na tension ya kisasi na labda angekuona mwema zaidi kwamba aliona taarifa fulani na akaniambia lakini akapuuza na hakunilipua.

Tatizo sio kuwa mtu mwema bali ni kukosa empathy sababu kila mtu anaweza kuwa mwema, na mkuu bila shaka ulikosa empathy.
Ukiwa na empathy automatically unakuwa mwema hata kama hauonekani mbele ya watu na kiwa unafanya mambo ya ajabu ikiwemo blackmailing.

Wema mtu atafanya ili kuonekana mbele za watu kwa maana hiyo yoyote anaweza kuwa mwema, lakini empathy sio kila mtu anaweza kuwa nayo, wema ni fake na empathy is real.
 
Is not an end of the world Pasi. Relax. It happens sometimes in lifetime
 
Mkuu Chris Hemsworth , kwanza asante, na hii ndio faida ya jf, unapata waalimu wa humility humu. Hapa umenifundisha somo moja kubwa sana na zuri sana!. Somo la wema vs empathy, kuna watu wanafanya wema wa kuonekanika na watu, hivyo machoni kuonekana kama watu, lakini mioyoni wana roho mbaya za ajabu!. Ni kweli katika tukio hilo nilifanya makosa, nilikosa kabisa empathy, tena enzi hizo, kijana shababi foleni toka Tegeta mpaka Feri!, sikupaswa kufanya nilio yafanya, acheni tuu karma i take its toll, tunahukumiwa kwa matendo yetu ndio maana sasa going to 60, nawasisitiza sana watu tutende wema, kumbe ni tunatakiwa tuwe na empathy.
Kiukweli kuna fani na fani, fani nyingine mtu ukikosa kabisa empathy ndio unaonekana shujaa. Mimi nikiwa JKT Makotupora kwenye somo la range, kila mtu anapewa risasi 10 to hit the bull. Dada mmoja ndio aliongoza kwa kuhit 10/10 mimi nikawa wa pilo nili hit 9/10 nadhani hadi 8/10 tulikuwa listed. Baada ya miezi 6 tukahamishiwa MMJKT pale Mlalakuwa kuja kumalizia. Baada tuu ya kumaliza JKT sisi tuliokuwa listed kwa kufanya vizuri range, tukapelekwa moja moja JWTZ, wenzetu wengine wakapelekwa CCP Moshi na wale jamaa zetu wa Mbweni, wakachukua watu wao.

Tukapangwa kufanya upya deppp ya JWTZ kwa miezi 6 pale Air wing Ukonga, kabla ya kwenda Monduli kwenye Officer Cadet. Kwenye Deppo ya JW range nikapiga 10/10!. Instructer wetu Sajini Meja Kahamba, akanisifu kwa kulenga shabaha, jina langu likaondolewa kwa watu wa kwenda Cadet, natakiwa kwenda kwenye kozi ya udunguaji, yaani snipers, nikaelezwa kazi yangu itakuwa ni moja tuu, kulenga kichwa!. Ndipo nikaelezwa kazi ya jeshi la polisi ni kulinda usalama wa raia na mali zao, wale wa Mbweni ni kulinda usalama wa nchi na wa serikali, kazi ya JWTZ ni kulinda nchi na mipaka yake hivyo kazi ya mwanajeshi anafundishwa ku ...tuu!. Tena kwenye mafunzo hayo ndio mnafundishwa mkiwa front line, amri ya ku "charge" ikitoka ni macho mbele, mbele kwa mbele, atakaye geuka tuu nyuma, wenzake ni 'hapo hapo' mnamalizana nae!. (Yule Jamaa aliyekuwa CinC aliposema "vita ya uchumi ni mbaya sana, afadhali vita ya kawaida, mkiwa front line wasaliti huwa wanafanywa nini!, huwezi kuwasaliti wenzako ukaachwa hivi hivi una survive!", we all know what happened!, (zile pyu pyu!).

Baada ya kujua kumbe mimi kazi yangu jeshini itakuwa ni hiyo!. Dhamira yangu ikanigomea!. Nikaacha jeshi na kujiunga TSJ kusomea uandishi wa habari!.

Huku kwenye uandishi, ukifanya Investigative Stories za uchunguzi na kuwalipua watu ndio unaonekana shujaa kumbe bila kujua una accumulates bad karma ya kutosha due to kukosa empathy na mwisho wa siku zetu waandishi wengi wa IJ wana end up horribly Waandishi wa Habari na Kupotea/Vifo vya Kutatanisha, Toka Katabalo, Saanane, Gwanda, Mwangosi, Isango. Ni Ama Tuombe Mungu Atunusuru ama...
Wema mtu atafanya ili kuonekana mbele za watu kwa maana hiyo yoyote anaweza kuwa mwema, lakini empathy sio kila mtu anaweza kuwa nayo, wema ni fake na empathy is real.
Namuomba sana Mungu, sio tuu anafundishe kunyamaza, bali pia anijalie empathy kwa hizi siku zangu zilizobakia!.
Asante tena, post yako hii, imekuwa ni darasa kubwa kwangu kwa somo la wema, empathy na karma!. Ubarikiwe sana!.
P
 
Mkuu Chris Hemsworth , kwanza asante, na hii ndio faida ya jf, unapata waalimu wa humility humu. Hapa umenifundisha somo moja kubwa sana na zuri sana!. Somo la wema vs empathy, kuna watu wanafanya wema wa kuonekanika na watu, hivyo machoni kuonekana kama watu, lakini mioyoni wana roho mbaya za ajabu!. Ni kweli katika tukio hilo nilifanya makosa, nilikosa kabisa empathy, tena enzi hizo, kijana shababi foleni toka Tegeta mpaka Feri!, sikupaswa kufanya nilio yafanya, acheni tuu karma i take its toll, tunahukumiwa kwa matendo yetu ndio maana sasa going to 60, nawasisitiza sana watu tutende wema, kumbe ni tunatakiwa tuwe na empathy.
Kiukweli kuna fani na fani, fani nyingine mtu ukikosa kabisa empathy ndio unaonekana shujaa. Mimi nikiwa JKT Makotupora kwenye somo la range, kila mtu anapewa risasi 10 to hit the bull. Dada mmoja ndio aliongoza kwa kuhit 10/10 mimi nikawa wa pilo nili hit 9/10 nadhani hadi 8/10 tulikuwa listed. Baada ya miezi 6 tukahamishiwa MMJKT pale Mlalakuwa kuja kumalizia. Baada tuu ya kumaliza JKT sisi tuliokuwa listed kwa kufanya vizuri range, tukapelekwa moja moja JWTZ, wenzetu wengine wakapelekwa CCP Moshi na wale jamaa zetu wa Mbweni, wakachukua watu wao.

Tukapangwa kufanya upya deppp ya JWTZ kwa miezi 6 pale Air wing Ukonga, kabla ya kwenda Monduli kwenye Officer Cadet. Kwenye Deppo ya JW range nikapiga 10/10!. Instructer wetu Sajini Meja Kahamba, akanisifu kwa kulenga shabaha, jina langu likaondolewa kwa watu wa kwenda Cadet, natakiwa kwenda kwenye kozi ya udunguaji, yaani snipers, nikaelezwa kazi yangu itakuwa ni moja tuu, kulenga kichwa!. Ndipo nikaelezwa kazi ya jeshi la polisi ni kulinda usalama wa raia na mali zao, wale wa Mbweni ni kulinda usalama wa nchi na wa serikali, kazi ya JWTZ ni kulinda nchi na mipaka yake hivyo kazi ya mwanajeshi anafundishwa ku ...tuu!. Tena kwenye mafunzo hayo ndio mnafundishwa mkiwa front line, amri ya ku "charge" ikitoka ni macho mbele, mbele kwa mbele, atakaye geuka tuu nyuma, wenzake ni 'hapo hapo' mnamalizana nae!. (Yule Jamaa aliyekuwa CinC aliposema "vita ya uchumi ni mbaya sana, afadhali vita ya kawaida, mkiwa front line wasaliti huwa wanafanywa nini!, huwezi kuwasaliti wenzako ukaachwa hivi hivi una survive!", we all know what happened!, (zile pyu pyu!).

Baada ya kujua kumbe mimi kazi yangu jeshini itakuwa ni hiyo!. Dhamira yangu ikanigomea!. Nikaacha jeshi na kujiunga TSJ kusomea uandishi wa habari!.

Huku kwenye uandishi, ukifanya Investigative Stories za uchunguzi na kuwalipua watu ndio unaonekana shujaa kumbe bila kujua una accumulates bad karma ya kutosha due to kukosa empathy na mwisho wa siku zetu waandishi wengi wa IJ wana end up horribly Waandishi wa Habari na Kupotea/Vifo vya Kutatanisha, Toka Katabalo, Saanane, Gwanda, Mwangosi, Isango. Ni Ama Tuombe Mungu Atunusuru ama...
Wema mtu atafanya ili kuonekana mbele za watu kwa maana hiyo yoyote anaweza kuwa mwema, lakini empathy sio kila mtu anaweza kuwa nayo, wema ni fake na empathy is real.
Namuomba sana Mungu, sio tuu anafundishe kunyamaza, bali pia anijalie empathy kwa hizi siku zangu zilizobakia!.
Asante tena, post yako hii, imekuwa ni darasa kubwa kwangu kwa somo la wema, empathy na karma!. Ubarikiwe sana!.
P
 
Pasco for the first time nimesoma habari yote. Inahuzunisha, kuelimisha na kuelekeza. Pia nimeelewa kwanini umekuwa ukitumia sana neno 'karma'.
 
Kwanza nikupe pol Kwa yaliyokukuta,lakini pia unapaswa kutambua kwamba malipo ni hapahapa duniani, pili huyo mtu kwa sisi tunaomjua hanaga shida na mtu wala visasi ,kama utapata basi Mungu atakuwa kakupa na kama utakosa basi siyo ridhiki yako ila huyo mtu uliyemwelezea ni mtu safi sana,hana shida na mtu,binafsi kanilea, ulitumia kalamu yako vibaya sana kumhukumu pasipo makosa, sasa nafikiri utakuwa umejifunza kitu.
 
Uliyataka mwenyewe Poti.
 
Nimesoma Uzi wako huu, nimegundua una akili na maarifa mengi sana. Mwenyezi Mungu aubariki uzao wako pascha
Good boy...kujitambua Raha sana....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…