Aache upotoshaji: Universal Health Care haimaanishi Bima ya Afya. 'Universal Health Care Coverage' kwa Tanzania tuko 100% tangia enzi za Mwl. Nyerere

Dr. Akili. So Tanzanians, currently can access health services without financial hardship!
 
Hata kumuona Daktari tu nayo ni tiba, cha msingi imani.
 
Well said! Asante.
Tatizo JF siku hizi ilishageuzwa propagandist machine kwa chama fulani.
UHC ni lengo kuu na ni process inayohusisha reforms nyingi ili kufikia lengo. Na kila nchi inafuata mchakato ambao unaendana na mazingira ya nchi husika. Siyo kama ambao wanataka bima ya afya Tanzania ifanane na Swden au Canada! Nafikiri hata rate ya kodi ya individual income ya nchi hizo, mfano Sweden hawaijui. Na wakitajiwa rate wanayolipa huko Sweden ndiyo itumike Tz watakufa kwa butwaa!


Yaani Lissu anatamka tu "nitaleta bima ya afya kwa kila mtanzania", alafu watu wanashangilia bila kujiuliza maswali ya msingi Kama;
-Ukubwa au mipaka ya hiyo bima ni nini?
-Gharama za hiyo bima ni kiasi gani
-Wananchi watachangia kiasi gani ili waweze kugharamia hiyo bima?
-Wananchi kiasi gani watakuwa a uwezo utayari wa kugharamia bima hiyo( Kumbuka NHIF ilivyotangaza gharama za vifurushi vya bima hao hao CHADEMA ndiyo waliongoza kupinga)
-Serikali itagharamia kwa kiasi gani na itagharamiaje?
-Serikali itasacrifice gharama za huduma gani nyingine ili uwezesha kugharamia hiyo bima
-Kama kuna players wengine mzigo watakaobeba ni upi?

Nasisitiza kufikia tunakotaka ni lengo linalohusisha mchakato endelevu na unaochukua muda. Magufuli yuko kwenye "right track" katika hili, na hana janja janja ya maneno, bali anaendeleza michakato yenye matokea chanya kama:-
-Kuelimisha watumishi wa kada ya afya na mabingwa bobezi,
-Kuajiri madaktari na wataalam wengine,
-Kujenga mahospitali, vituo vya afya na zahanati zenye hadhi ya juu,
-Kununua vifaa tiba vya msingi na vifaa tiba vya kisasa vyenye teknolojia ya hali ya juu
-Kuongeza tena kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa dawa
-Jenga miundombinu ya usafiri kurahisha utoaji huduma na kupunguza gharama,
-Zuia kuenea kwa magonjwa kwa;
. Kupeleka maji safi kwa wote - katika hili kasi ya Magu inatisha!
. Sambaza umeme kote hasa vijijini
. Kupatikana kwa elimu ya msingi (na sekondari) bure kwa watu wote

ALAFU kuna mtu anaropoka tu "Nitatoa bima ya afya" na wengine wanashangilia kama mazuzu!
 
Dr. Akili. So Tanzanians, currently can access health services without financial hardship!
That is the truth Mr Zawadini. The government takes care of those with financial hardships by giving them exemptions or subsidies. The procedure to get exemption or subsidy is very simple and is available in every health facility.
 
Yaani Lissu anatamka tu "nitaleta bima ya afya kwa kila mtanzania", alafu watu wanashangilia bila kujiuliza maswali ya msingi Kama;
Yaani huyu jamaa kwa akili yake anafikiri bima ya afya ni bidhaa kama mafuta au mahindi ambayo ataenda kuinunua mahali fulani na kuja kuwagawia watanzania wote bure.

Au anadhani ni mfumo (system) au application fulani ambayo anaweza kwenda kui copy Ubeligiji au Amerika na kuja kui paste and install hapa kwetu Tanzania akifikiri itafanya kazi! Halafu eti anajigamba ni msomi kwa sababu anakijua sana kiingereza. Kwa taarifa yake kabibi kangu kalikuwa kanajua kiingereza kuliko yeye kwa sababu kalikuwa ka housegirl ka waingereza kwa miaka arobaini.

Yaani aje ku install Obamacare hapa Tanzania si itakuwa kiama. Halafu kama bima ya afya itatolewa bure na serikali kwa watanzania wote, kuna sababu gani ya kuwa na hiyo bima? Si serikali ingetoa tu matibabu bure kwa watanzania wote kama ilivyokuwa enzi za Mwalimu Nyerere.
 
Yaaani umeandika muda mrefuu huku ukikumbuka ndugu zako wanavyoteseka kwa gharama za matibabu, lakini njaaa inakuuma huna namna
 
MATAGA wala hayajifichi!
 
Dr Tacor definition ya UHC umeikosea,sio ulichoandika!

Thats aside....

Wewe na Tundu Lissu,na Nyerere na wengine wanaoendekeza u-communism ni wa kukemea kabisa..

Wewe umekuja duniani unategemea serikali ikutibu for free?

Yaani umekuja kwenye hii dunia,zinachukuliwa kodi za class fulani ya wanadamu unatibiwa wewe for free?

Huu ndio upuuzi wa sera za ki-komunisti,hovyo sana...

Umekuja duniani,jitibu mwenyewe kwa kipato chako,jilishe mwenyewe kwa kipato chako,jisomeshe kwa kipato chako,somesha watoto wako kwa kipato chako,ni jukumu lako kuhakikisha una survive kadiri unavyoweza..

Huwezi jitibia,kufa!

Serikali kutoa welfare kiasi hiki hakisaidii zaidi ya kuongeza tatizo..

Wanaopewa vitu vya bure huwa hawapungui hua wanaongezeka kila siku,solution ni ku-apply pure capitalism,kila mtu ajitegemee,akishindwa AFE!

Huu ndio ujinga wa poor class kutumia government kuibia wenye kipato ili wapate huduma za BURE!

Nonsense!
 

Mbona Rwanda wameweza.
 
Kweli msomi Dr. unaweza kusema hamna mTanzania anakufa au anakosa huduma ya afya kwa sababu hana pesa? Huduma inayojumuisha pia dawa? Unasema haya with a straight face bila chembe la aibu! Kweli wasomi mna shida.

Amandla...
Acha kuamini majungu. Ni mtanzania yupi aliyeachwa akafa akiwa kwenye hospitali, kituo cha afya au zahanati zetu za serikali kwa sababu hana pesa?

Uhaba wa madawa na vifaa tiba ni suala tofauti. Hili linatokana na mzigo mkubwa ambao serikali inaendelea kuubeba katika hiyo cost sharing kati ya mgonjwa na serikali. Hata hivyo kupitia fedha za mafisadi ambao serikali imewabana pamoja na kuongeza makusanyo ya kodi kutoka Tsh 800 billion kwa mwezi mwaka 2015 hadi Tsh 1.5 trillion kwa mwezi mwaka 2020, uhaba wa dawa na vifaa tiba umepungua kwa kiasi kikubwa sana. Serikali imeweza kuongeza bajeti ya madawa MSD kutoka Tsh 28 billion hadi Tsh 280 billion. Imeongeza wataalamu wa afya kwenye vituo tiba kwa kiasi kikubwa nk. Hata yale magonjwa yaliyohitaji kutibiwa nje ya nchi mengi yake sasa yanatibika hapa hapa. Kwa kasi hii uhaba wa dawa, vifaa tiba na watalaamu wa afya muda si mrefu litakuwa historia. Tumefanya yote haya kwa pesa zetu za ndani. Hakuna cha mikopo wala cha misaada ya wajomba. Lissu haya hayajui. Yeye anadhani haya yanafanywa na bima ya afya. Eti anasema akichaguliwa kuwa rais bima ya afya itawapandisha mishahara madaktari na manesi mara dufu!
 
Mnapolinganisha Tanzania na nchi kama Canada ni vyema mlinganishe na pato la taifa ( GDP), uwiano wa kodi kwa GDP na idadi ya watu.

Canada GDP yake ni 1.7 Trillion US Dollar, uwiano wa kodi kwa GDP ni asilimia 33 na population ni milioni 37.6. Tanzania GDP ni kama 60 Billion US Dollar, uwiano wa kodi kwa GDP ni asilimia 12.9 na pupulation ni miliini 56.

Hivyo Lissu wenu ambaye anadai atashusha zaidi kodi hawezi kutoa huduma bora za afya hata kwa kiwango cha sasa kinachotolewa Tanzania sembuse kama Canada au nchi za OECD ambazo wastani wa uwiano wa kodi kwa GDP ni asilimia 34.3.

Mtu yeyote mkweli angeanza na kuonyesha namna atakavyokuza pato la nchi kwa sababu ndilo litakalomuwezesha kutoa huduma bora.
 

Tumekubaliana na upotoshaji wake, unasemaje?
 
Kwa hiyo unakubali kwamba uwanja wa cha ulikua uamuzi wa kijinga?

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
 
Reactions: BAK
LISSU NI MROPOKAJI TU KAMA WENDAWAZIMU WENGINE HANA WATAALAMU WAKUMSHAURI TATIZO ANAJIONA YEYE ANAAKILI KULIKO WATANZANIA WOTE MAPAKA ANASEMA HAKUNA MTANZANIA ANAYEJUWA ENGLISH HATA MIMI NAJUA ENGISH BANA ASITUDHARIRISHE

=Asitu dhalilishe.

Unajua english lakini Kiswahili hujui.

Hopeless.

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
 
Reactions: BAK
Nimekuambia hizi bima ni kwa ajili ya kumrahisishia mtanzania kulipia hiyo cost share yake atakapokuwa mgonjwa na kulazimika kwenda kutibiwa.

Nimekuambia hadi sasa zipo bima za afya nne zinazomilikiwa na serikali (publically owned) kila moja ikiwa na target population yake kwa ifuatavyo:
1. NIHF - target population yake ni watumishi wa umma na wategemezi wao (compulsory). Mtu mwingine anaruhusiwa kujiunga (voluntary). Bima hii ni comprehensive na gharama ya premium zake ni kubwa - Tsh 1.5 million kwa mwaka lakini serikali imeruhusu watoto na wanafunzi kulipa TSh 50,000 tu kwa mwaka. Kumbuka kuwa watoto na wanafunzi idadi yao ni 40% of the total population of Tanzania.

2. CHF: target population ni rural population households. Ni bima ya hiari. Kila household hulipia Shs 10,000 tu kwa mwaka ambayo huwezesha wote walio kwenye house hold hiyo kupata tiba kwenye ngazi ya zahanati, kituo cha afya na hospitali ya wilaya. Kumbuka kuwa rural population is about 70% of the total population of Tanzania.

3. TIKA: mfumo wake ni sawa na wa CHF ila target population yake ni urban household.

4. SHIB: Target population ni wanachama wote wa mfuko wa pensheni ya NSSF pamoja na wategwmezi wao. Kumbuka kwamba ni takwa la kisheria wote walio kwenye ajira rasimu wanapaswa kukatwa asilimia fulani ya mishahara yao na mwajili kutoa kiasi hicho ambazo hupelekwa kwenye mfuko wa NSSF kama pensheni ya uzeeni. Kiasi fulani cha pesa hiyo NSSF hutumika kama bima yao ya afya pamoja na wategemezi watu. Halafu mijitu mingine inataka fao la kujitoa. Ukijitoa na hiyo ba yako ya afya utakuwa umejitoa.

5. Sasa kuna ubaya gani kuongeza wigo wa bima hizi za afya? Kuna ubaya gani kuwa pia na bima ya afya ya wakulima ambayo target population yake ni wakulima wanaokuja kuuzaazao yao ya biashara kama pamba, kahawa na korosho? Premium ya bima yao inakatwa kwenye gharama ya mazao yao kwa hiari yao? Vivyo hivyo kwa makundi mengine eg bodaboda, wafanyabiashara na wajasiliamali wengine kwa hiari yao?

Hizi ndizo mbinu pekee zitakazowezesha kila mtanzania kuwa na bima ya matibabu. Si zile mbinu za huyu mgombea za kuenda ku copy ubelgiji na ku paste tanzania.
 
Mifuko yote uliyoitaja ipo kwenye makaratasi tu, siku ukiugua au ukiuguza ndio utajua kuwa kuna usanii wa mifuko kama CHF n.k.
Hata Stiglers gauge ilikaa kwenye makaratasi miaka zaidi ya 30 hadi alipopatikana Ngosha na mambo yakawa reality. Huyo Ngosha akipewa miaka mingine 5 haya yote yaliyomo kwenye makaratasi lakini utekelezaji wake unasuasua yatakuwa reality. Hao wengine hamna kitu.

Kumbuka kuwa Kagame ali copy makaratasi yetu haya akaenda kuyatekeleza kwake Rwanda na sasa Rwanda inasifika kuwa na mfumo bora wa bima ya afya na Universal healthcare.
 
Katika tafiti nyingi ni Rwanda kwa hapa EA ambayo walau imefika 90% ya coverage ya bima na pia vituo vya afya kuwa meter chache kutoka kwa mgonjwa na ratio ya wahudumu kwa wagonjwa etc sasa unaposema 100% Tanzania ni indicators gani umetumia kupima?

Pamoja na maelezo marefu ila hujaeleza ni jinsi gani informal sector wengi hawapo kwenye skimu za bima kabisa. Wamachingwa wangapi wana bima? Wakulima wa vijijini huko? Kiukweli bima hapa Tz ni common kwa formal sector pekee ambao sio tu wana bima ila wana hifadhi zingine za jamii. Sasa Lissu anataka hao 70% walio kwenye informal sector nao wawe kwenye skimu za bima tena kwa unafuu maana mkiwa wengi pool inakua kubwa hivyo michango ni inakua nafuu kuliko sasa ambapo hizo bima ulizotaja haziwezi tibu magonjwa mengi. Hiyo ya elfu 50 inatibu magonjwa yote? Like serious? Au unataka tu kupinga for the sake?

Tuache siasa, Nakumbuka takwimu za TIRA 2019 insurance penetration as percentage to GDP ilishuka alafu mtu anakuja hapa anadai Tz tupo insured 100%.

So weird
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…