Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
ABDULKARIM HAJJ MUSSA, MWINYI MCHENI OMARI NA JULIUS NYERERE KATIKA KUIJENGA TANU KILWA
Abdulkarim Hajj Mussa Jamadar akifahamiana vyema na Julius Nyerere.
Abdulkarim Hajj Mussa Jamadar na Mwinyi Mcheni Omar ni kati ya ya watu waliomuunga mkono Nyerere na kasaidia sana katika kuiingiza TANU Kilwa Mtoni.
Abdulkarim akimpakiza Mwalimu kwenye pikipiki yake BSA 500 wakienda kote sehemu za Kilwa kuhamasisha watu kujiunga na TANU kudai uhuru wa Tanganyika.
Katika harakati hizi Nyerere alikuwa akifikia na kulala nyumbani kwa Mwinyi Mcheni Omari na mikutano yote ya ndani ya TANU ikifanyika katika nyumba hiyo.
Taifa lina deni kubwa sana kwa wazalendo hawa.
Hapo chini ni picha ya pikipiki aliyokuwa akipada Baba wa Taifa na nyumba almbayo alikuwa akifikia na kulala pamoja na kufanya mikutano ya ndani.
(Picha zote kwa hisani ya marehemu Abdulkarim Shah maarufu kwa jina la Bulji mjukuu wa Abdulkarim Hajj Mussa).
Abdulkarim Hajj Mussa Jamadar akifahamiana vyema na Julius Nyerere.
Abdulkarim Hajj Mussa Jamadar na Mwinyi Mcheni Omar ni kati ya ya watu waliomuunga mkono Nyerere na kasaidia sana katika kuiingiza TANU Kilwa Mtoni.
Abdulkarim akimpakiza Mwalimu kwenye pikipiki yake BSA 500 wakienda kote sehemu za Kilwa kuhamasisha watu kujiunga na TANU kudai uhuru wa Tanganyika.
Katika harakati hizi Nyerere alikuwa akifikia na kulala nyumbani kwa Mwinyi Mcheni Omari na mikutano yote ya ndani ya TANU ikifanyika katika nyumba hiyo.
Taifa lina deni kubwa sana kwa wazalendo hawa.
Hapo chini ni picha ya pikipiki aliyokuwa akipada Baba wa Taifa na nyumba almbayo alikuwa akifikia na kulala pamoja na kufanya mikutano ya ndani.
(Picha zote kwa hisani ya marehemu Abdulkarim Shah maarufu kwa jina la Bulji mjukuu wa Abdulkarim Hajj Mussa).