TANZIA Abdulkarim Shah, umekuja Saigon Sports Club umechelewa na umeondoka kwa haraka

TANZIA Abdulkarim Shah, umekuja Saigon Sports Club umechelewa na umeondoka kwa haraka

..hizo sentensi mbili kwa kweli zimenifurahisha sana.

..zimenifurahisha kwasababu umeweza kueleza jambo kubwa kwa maneno machache, lakini kwa msisitizo mkubwa.

..nimerudia kusoma sentensi hizo tena na tena nikifurahia umahiri wako wa kucheza na maneno.

..THANK YOU!!
JK,
Alhamdulilah.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngongo,
Mimi si ustadhi wala sina uhusiano wowote na Mtaa wa Tandamti.

Nimeishi miaka mingi ya maisha yangu Masaki, Msasani Peninsular na anuani yangu ya Dar es Salaam ndivyo inavyoonyesha hadi sasa.

Hapo ndipo kwetu.

Ningeshukuru sana kama ningejaaliwa nikawa ustadh lakini kuwa ustadh kunahitaji ilm ambayo mie sina.

Mwanangu sasa mtu mzima ananambia,"Baba nikiona tabu sana kukuona wewe unasali nyuma yangu mie mwanao ndiyo imam naongoza sala."

Mie humjibu nikamwambia, "Ndiyo ujue faida ya ilm mimi baba yako nimekuwa chini wewe umekuwa juu sababu ni hiyo ilm ambayo mimi sina; ni hiyo Qur'an uliyohifadhi ndiyo imekunyanyua wewe. Hawawi sawa mwenye kujua na asiyejua."

Ningependa sana kuwa ustadh lakini kunahitaji ilm kuwa ustadh hakuji kirahisi upinde mgongo kwa walimu usomeshwe vitabu na vitabu.

Hakika ningependa kuwa ustadh.

Nilichoambulia ni passages and passages za William Shakespeare, Charles Dickens...

Ngongo unaponiita ustadh ilm niitakayo lakini sina unatonesha kidonda.




Sent using Jamii Forums mobile app
Mashaallah
Haya ni maneno yenye busara kwa mtu mwenye akili.
Mzee wangu Mohamed Said Allah akuzidishie kheri na barka wewe pamoja na familia yako.
Hakika nnavutiwa sana na majibu yako ya upole yaliyojaa busara na hekima,
Watu waliojaa chuki ndani ya mioyo yao wanakuuliza kwa kebehi, dhihaka na dharau, ila mashaallah majibu yako ya upole yalijaa hekima na busara yanazilainisha kidogo nyoyo zao zilizo kakamaa kwa chuki na husda zilizo jificha ndani ya vifua vyao.
Allah azidi kukuweka mzee wetu Ili na sisi wajukuu zako tupate kustafidi kwa ilmu tuipatayo kupitia kwenye makala zako.
 
Mnga'ato,
Allah ndiyo kauli yake katika Qur'an kuwa Muislam nduguye Muislam.

Aya inaendelea kueleza kupatanisha baina ya ndugu waliogombana.

Sikumbuki kichwa cha thread husika, ila nilipata kuandika kwenye hiyo thread ukweli huu uliothibitisha hapa: muislamu wa kweli HAWEZI na hapaswi kuwa rafiki au ndugu wa asie muislamu (especially Wakristo na Wayahudi).
Natamani ungetoa funzo hili siku kwa wale wote waliokuwa wananibishia. Asante sana mzee wetu kwa uthibitisho huu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom