Ngongo,
Mimi si ustadhi wala sina uhusiano wowote na Mtaa wa Tandamti.
Nimeishi miaka mingi ya maisha yangu Masaki, Msasani Peninsular na anuani yangu ya Dar es Salaam ndivyo inavyoonyesha hadi sasa.
Hapo ndipo kwetu.
Ningeshukuru sana kama ningejaaliwa nikawa ustadh lakini kuwa ustadh kunahitaji ilm ambayo mie sina.
Mwanangu sasa mtu mzima ananambia,"Baba nikiona tabu sana kukuona wewe unasali nyuma yangu mie mwanao ndiyo imam naongoza sala."
Mie humjibu nikamwambia, "Ndiyo ujue faida ya ilm mimi baba yako nimekuwa chini wewe umekuwa juu sababu ni hiyo ilm ambayo mimi sina; ni hiyo Qur'an uliyohifadhi ndiyo imekunyanyua wewe. Hawawi sawa mwenye kujua na asiyejua."
Ningependa sana kuwa ustadh lakini kunahitaji ilm kuwa ustadh hakuji kirahisi upinde mgongo kwa walimu usomeshwe vitabu na vitabu.
Hakika ningependa kuwa ustadh.
Nilichoambulia ni passages and passages za William Shakespeare, Charles Dickens...
Ngongo unaponiita ustadh ilm niitakayo lakini sina unatonesha kidonda.
Sent using
Jamii Forums mobile app