Abiria kulazimishwa kuteremka Kituo cha Mbezi tuliambiwa Wafanyabiashara walilalamika kukosa wateja, leo mmh!

Abiria kulazimishwa kuteremka Kituo cha Mbezi tuliambiwa Wafanyabiashara walilalamika kukosa wateja, leo mmh!

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Hii amri ya abiria toka mikoani kushushwa Mbezi mbona hatupewi ukweli, siku zilizopita ilidaiwa mkuu wa mkoa alilalamikiwa na wafanyabiashara kuwa wanakosa wateja!

Hivi sasa tunaambiwa eti ni usalama kudhibiti wahamiaji! Kwani wahamiaji hawawezi kushuka au kupanda Kibaha au Bagamoyo! Mabasi ni tofauti na ndege Ulaya kwani yanaweza kushusha au kupandisha abiria mahali popote kabla ya kufika Mbezi, hapa hoja ya wafanyabiashara ya kukosa wateja inaipiku ya uhamiaji.

Hivi vituo vya mabasi kusudio lake ni kufanya biashara ya mikate na chipsi? Hakuna msafiri anayesafiri kwa ajili ya kununua chipsi, kama mkuu wa mkoa anawatetea wafanyabiashara akifurahi wasafiri wakiteseka, basi hilo ni tatizo.

Viongozi wanaowajali abiria hawatakuwa tayari kuona abiria wanateseka kwa utashi wa watu binafsi.
 
Aliyekuja na wazo la kujenga hizi public transport hub nje ya miji ni kihiyo mkubwa,mimi ninasafiri kwenda iringa mjini, nishuke igumbiro nitafute usafiri mwingine na bus iende bila abiria iringa mjini, ni mambo ya ajabu sana nchi hii
 
Aliyekuja na wazo la kujenga hizi public transport hub nje ya miji ni kihiyo mkubwa,mimi ninasafiri kwenda iringa mjini, nishuke igumbiro nitafute usafiri mwingine na bus iende bila abiria iringa mjini, ni mambo ya ajabu sana nchi hii
Viongozi wanafurahi wao wakiwapita njiani mkiwa mmebeba kichwani masanduku yenu usiku kwenye giza, angalau anaonekana nani mtawala na nani mtawaliwa.
 
Back
Top Bottom