Absalom Kibanda (Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri) avamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa

Absalom Kibanda (Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri) avamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa

Tina

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2007
Posts
572
Reaction score
581
Kibanda.jpg

Mwanahabari Absalom Kibanda

TAARIFA ZA AWALI
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya New Habari wachapishaji wa magazeti ya Mtanzania, Dimba, Bingwa na Dimba, Absalom Kibanda amevamiwa na watu wasiojulikana akiwa ndani ya gari lake wakati akiingia nyumbani kwake Mbezi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Kibanda alivamiwa majira ya saa sita usiku wa kumkia leo Tar March 6 2013, akitokea kwenye majukumu yake ya kila siku. Inadaiwa kuwa alichomolewa kwene gari, akapigwa na vitu vyenye ncha kali kichwani, ametobolewa jicho lake la kushoto pamoja na kunyofolewa kucha na baadhi ya vidole na hatimaye kutupwa mbali kidogo kutoka nyumbani kwake.

Baada ya hapo wasamalia wema walijitokeza na kumkimbiza katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, ambako alipokelewa vizuri na madaktari na kumpatia tiba ya awali na baadaye kumhamishia Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) ambako mpaka sasa anaendelea na matibabu.

Watu waliomfanyia madhara hayo, hawakuweza kuchukua kitu chochote kwenye gari ambapo kulikuwemo Laptop, simu na nyaraka zingine.

kibanda-hosp.jpg
makamu-kibanda.jpg

Absalom Kibanda akiwa hospitali.
----------
APELEKWA AFRIKA KUSINI
Tasnia ya habari nchini Tanzania kwa mara nyingine imetingishwa baada ya mwenyekiti wa jukwaa la wahariri nchini humo, Absalom Kibanda kutekwa, kupigwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jumatano nje kidogo ya jiji la dara es salaam.

Kibanda tayari amesafirishwa jioni hii kwa ndege maalum kwenda nchini Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu ambapo kwa mujibu wa taarifa za awali za kitabibu, amejeruhiwa kichwani ambako alipigwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni nondo. Jicho lake la upande wa kushoto limeathirika kwa kudhaniwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali, kucha katika kidole cha mkono wa kulia kung’olewa na meno mawili kung’olewa pia huku washambuliaji wakiwa hawajaondoka na kitu chochote.

Tukio la kujeruhiwa mweyekiti Kibanda limekumbusha tukio zito lililowahi kutoke akatika tasnia ya habati nchini Tanzania mwishoni mwa mwaka jana baada ya mwandishi wa habari wa kituo cha Televisheni cha channel ten kuuwawa katika mkutano wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema mkioani Iringa.

Neville Meena ni katibu mkuu wa jukwaa la wahariri amekemea kuhusu tukio hilo akisema kuwa linatishia waandishi wa habari kufanya kazi zao kwa uhuru.

Katika hospitali ya taifa ya Muhimbili ambako Kibanda alikuwepo kabla ya kusafirishwa kwa matibabu, nje ya nchi viongozi mbalimbali wa serikali vyombo vya habari na wanasiasa walifika kumjulia hali akiwemo bwana Reginald Mengi ambaye ni mwenyekiti wa Chama cha wamiliki wa vyombo vya habari Tanznania, MOAT.

Kibanda.jpg

Bwana Kibanda ambaye kwa sasa ni mhariri mtendaji mkuu wa kampuni ya New Habari inayomiliki magazeti kadhaa hapa nchini miezi michache iliyopita alikuwa mhariri mtendaji katika gazeti la Tanzania daima linalomilikiwa na familia ya mwenyekiti wa chama cha demokrasai na maendeleo CHADEMA, bwana Freeman Mbowe.

Mkurugenzi wa idara ya habari, maelezo hapa nchini Bwana Assah Mwambene alikuwepo pia hospitalini muhimbili.

Kamanda wa kanda maalum Suleimano Kova katika mkutano wake na waandishi wa habari amesema kwa kushirikiana makao makuu ya polisi wameunda jopo la wapelelezi kumi kwa ajili ya kuchunguza kuvamiwa na kushambuliwa na hatimaye kujeruhiwa kwa mwenyekiti huyo wa jukwaa la wahariri Absalom Kibanda ambapo amekiri kwamba vitendo vya mashambulizi yanayoonekana ya kulipiza kisasi vimeshamiri kwa sasa.

Makamu wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dakta Gharib Bilal naye alikuwa miongoni mwa viongozi wa ngazi za juu aliyefika kumjulia hali bwan Kibada akiwa muhimbili kabla ya kusafirishwa nchini Afrika Kusini.

PIA, SOMA:
VISA DHIDI YA WANAHABARI WENGINE WA TANZANIA:
PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Polisi waanze uchunguzi na gazeti la tanzania daima na chadema. kwani hatuelewi ni kwanini alikimbia huko alipokuwa mhariri wa hilo gazeti la mwenyekiti wa chama.
 
Polisi waanze uchunguzi na gazeti la tanzania daima na chadema. kwani hatuelewi ni kwanini alikimbia huko alipokuwa mhariri wa hilo gazeti la mwenyekiti wa chama.
Ili uwapoteze lengo polisi, waache kuchunguza na kukugundua, unashauri waanzie mahala pengine ili wewe uendelee kufaidi fedha uliyolipwa kwa ufedhuli huo.
 
Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri, Abdalom Kibanda, amekimbizwa Muhimbili baada ya kuvamiwa na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi wakamteka na kumjeruhi akiwa nyumbani kwake na sasa amekimbizwa Muhimbili kwa matibabu.

Taarifa zaidi baadae.
Mambo ya ulimboka yameanza Tena
 
Kwa hali ya kisiasa ya nchi yetu, na ukinzani uliokuwepo baina ya serikali na Wanahabari, sidhani hapa kuna sababu nyingine zaidi ya hiyo. Absalom Kibanda, amekuwa msumari mkali kwa serikali, tangu alipokuwa Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima na sasa New Habari Coorporation.

Ikumbukwe kuwa, hadi sasa ana kesi iliyoko mahakamani, kesi ya uchochezi kwa sababu ya makala iliyoandikwa na kamanda Samson Mwigamba na kuchapwa katika gazeti la Tanzania Daima wakati Bwana Kibanda akiwa bado Mhariri wa Tanzania Daima.

Ngoja tuwasikie watakavyokuja na majibu ya upelelezi wao. Ila Tanzania kwa sasa, si mahali salama sana kwa wanahabari wanaojali uzalendo na weledi wa kazi zao
 
Wee mleta habari, hebu weka mambo sawa. Ametekwa au amevamiwa na majambazi nyumbani kwake? Tuambie wamechukua nini? Ukisema ametekwa ina maana walimpeleka kusikojulikana na kuanza kumshambulia? Hebu toa maelezo yanayojitosheleza bwana.
 
Amevamiwa nyumbani kwake, akatekwa na kukimbizwa hosp.???? Should we wait for another repenting 'Muhindi'?????
 
Kwa nchi yetu ilivyo sasa hivi kuna uwezekano mkubwa kwamba sababu kubwa ya kutekwa kwake inahusiana na kazi zake. Tusubiri tufahamu sababu, lakini inaweza kabisa isijulikane. Mungu amponye haraka.

Ooh boy.. tunamuombea apone.. ni matumaini yangu kuwa hili halihusiani na kazi yake ya uandishi.
 
Hili la kutekwa nyumbani kwake linanipa shida..huyu atakuwa mnyatiati wa mashine za watu
 
Yule Mkenya Amerudi tena kuwadhulu na kuwateka watu @ kova
 
Mungu akujalie upone haraka utueleze kilichotokea Absolom. Haya mambo ya utekwaji na kujeruhiwa yanachefua sana nchini mwetu kwa sasa.
 
Back
Top Bottom